bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Jeremiah 6
Jeremiah 6
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 7 →
1
Enyi watu wa kabila la Benjamina, muondoke Yerusalema, mukimbie! Mupige baragumu katika muji Tekoa! Muonyeshe kitambulisho cha vita huko Beti-Keremu, maana hasara na maangamizi makubwa vinakuja kutoka upande wa kaskazini.
2
Muji wa Sayuni ni muzuri na wenye kupendeza, lakini utaharibiwa.
3
Watu wataufikia kama vile wachungaji na makundi yao, watasimamisha hema zao kandokando yake, kila wamoja upande wao kwa kulisha makundi yao.
4
Halafu watasema: Mujitayarishe, tupigane vita na Sayuni. Musimame, tuushambulie pa saa sita za muchana! Bahati mbaya kwetu, maana jua linatua! Saa za magaribi zinakaribia.
5
Basi, tutaushambulia usiku; tutaziharibu nyumba zake nzuri zote.
6
Yawe wa majeshi anasema hivi: Mukate miti na kulundika udongo, kwa kuweza kupandia ndani ya Yerusalema. Muji huu unapaswa uazibiwe, maana hamuna lolote ndani yake isipokuwa ukorofi tu.
7
Kama vile maji yanavyotiririka toka ndani ya kisima, ndivyo maovu yanavyotiririka katika Yerusalema. Mateso makali na maangamizi yanasikilika ndani yake. Ninaona magonjwa na vidonda mbele yangu kila siku.
8
Basi usikilize maonyo, ee Yerusalema. Kama sivyo nitakutupilia mbali; nitakufanya ukuwe jangwa, kuwa pahali pasipokaliwa na mutu.
9
Yawe wa majeshi anasema hivi: Muwakusanye watu wote wa Israeli waliobaki kama vile watu wanavyookotesha zabibu katika shamba; kama vile muchumaji wa zabibu, mupitishe mikono katikati ya matawi yote.
10
Nitaongea na nani nipate kumwonya, kusudi wapate kunisikia? Angalia, masikio yao yameziba, hawawezi kusikia ujumbe wako. Maneno ya Yawe, yamegeuka kwao jambo la kuchekelea. Hawalifurahii hata kidogo.
11
Nimejaa hasira ya Yawe nami ninachoka kwa kuizuia. Kwa hiyo Yawe akaniambia: Umwange hasira ile katika barabara juu ya watoto na vilevile juu ya makundi ya vijana; nayo itawaangukia wote, mume na muke, nao wazee na hata wale ambao wamezeeka sana.
12
Nyumba zao zitapewa watu wengine, nayo mashamba yao na wake zao vilevile; maana nitaunyoosha mukono wangu, kuwaazibu wakaaji wa inchi hii. –Ni ujumbe wa Yawe.
13
Wote, tangu mudogo mpaka mukubwa kabisa, kila mumoja anatamani kupata faida isiyokuwa ya haki. Tangu manabii mpaka makuhani, kila mumoja wao ni mudanganyifu.
14
Wanatunza vidonda vya watu wangu juujuu, wakisema: “Kuna amani, kuna amani”, ingawa hakuna amani yoyote!
15
Wao walisikia haya walipofanya machukizo hayo? Hapana! Hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo wataanguka pamoja na wale wanaoanguka; wakati nitakapowaazibu, wataangamizwa kabisa. –Ni Yawe anayesema hivyo.
16
Yawe anasema hivi: Musimame katika masanganjia, muangalie. Muulize juu ya matukio ya zamani. Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri muifuate, nanyi mutaweza kupumzika. Lakini wao wakasema: Hatutafuata njia hiyo.
17
Kisha nikawawekea walinzi kwa kuwaarifu nikawaambia: Musikilize mulio wa baragamu. Lakini wao wakasema: Hatutausikiliza.
18
Kwa hiyo, musikilize, enyi mataifa; enyi makundi ya watu, mujue yale yatakayowapata.
19
Sikiliza, ee dunia! Mimi nitawaletea watu hawa hasara kulingana na nia zao mbaya. Maana hawakuyajali maneno yangu, na mafundisho yangu nayo wameyakataa.
20
Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba, na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki, wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.
21
Kwa hiyo Yawe anasema hivi: Nitawawekea watu hawa vikwazo, ambavyo vitawaangusha chini. Wababa na wana wataangamia, na jirani na rafiki vilevile.
22
Yawe anasema hivi: Muangalie, watu wanakuja toka inchi ya kaskazini; taifa kubwa linajitayarisha kutoka mbali kwa mwisho wa dunia.
23
Wameshika pinde zao na mikuki; ni watu wakali wasiokuwa na huruma. Vishindo vyao ni kama uvumi wa bahari. Wamepanda juu ya farasi, wamejipanga tayari kwa vita na wewe Sayuni!
24
Waisraeli wanasema: Tumesikia habari zao. Kwa hiyo mikono yetu imeregea; tumeshikwa na huzuni na uchungu, kama mwanamuke anayezaa.
25
Hatuwezi kwenda katika mashamba, wala kutembea katika barabara; waadui wameshika silaha katika mikono, vitisho vimejaa kila pahali.
26
Yawe anasema: Muvae magunia, enyi watu wangu na kugaagaa katika majivu. Muomboleze kwa uchungu, kama mutu anayemulilia mwana wake wa pekee, maana mwangamizaji atakuja, na kuwashambulia kwa rafla.
27
Yeremia, wewe nimekuweka kuwa muchunguzi na mupimaji wa watu wangu, kusudi uchunguze na kuzijua njia zao.
28
Wote ni waasi na wagumu, ni watu wanaopitapita wakisengenya wengine, ni wagumu kama shaba au chuma. Wote wanatenda mabaya.
29
Moto wa kufua vyuma unawaka kwa nguvu, risasi inayeyukia humohumo katika moto; ni bure kuendelea kuwatakasa watu wangu, waovu hawawezi kuondolewa uchafu wao.
30
Basi wataitwa “takataka za feza”, maana mimi Yawe nimewakataa.
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 7 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52