bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Jeremiah 40
Jeremiah 40
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 39
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 41 →
1
Huu ni ujumbe uliotolewa kwa Yeremia kutoka kwa Yawe wakati Nebuzaradani mukubwa wa walinzi wa mufalme alipomuruhusu Yeremia aondoke Rama. Huyo mukubwa alimukamata Yeremia akifungwa minyororo, pamoja na wafungwa wengine wote wa Yerusalema na Yuda ambao walikuwa wamepelekwa katika uhamisho kule Babeli.
2
Mukubwa wa walinzi alimukamata Yeremia, akamwambia: Yawe, Mungu wako, alitangaza hasara juu ya pahali hapa.
3
Na sasa Yawe ametimiza jambo hilo na kutenda kama alivyosema. Kwa sababu ninyi wote mulimukosea Yawe na kukataa kumutii, jambo hilo limewapata.
4
Basi! Leo ninafungua minyororo toka mikono yako. Kama unaona ni vizuri kwenda pamoja nami mpaka Babeli, basi tuende pamoja; mimi nitakutunza vizuri. Lakini kama unaona si vizuri kwako kwenda pamoja nami mpaka Babeli, basi, usikuje. Ujue kwamba unaweza kwenda popote katika inchi hii. Basi kwenda kwenye unaona ni vizuri kwenda.
5
Kama ukiamua kubaki, basi rudi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, ambaye mufalme wa Babeli amemusimika kuwa mutawala wa miji yote ya Yuda, ukae naye kati ya wanainchi wengine. Kama sivyo, kwenda kwenye unaona unastahili kwenda. Basi, mukubwa wa walinzi akamupa Yeremia vyakula na zawadi, kisha akamwacha ajiendee.
6
Kisha Yeremia akaenda Misipa kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, akakaa naye pamoja na wanainchi waliobaki katika inchi.
7
Wakubwa wote wa waaskari kutoka katika pori pamoja na watu wao, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli alikuwa amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, kuwa mutawala wa inchi, na kwamba alikuwa amewaweka chini ya usimamizi wake wanaume, wanawake na watoto, ni kusema watu wakosefu kabisa katika inchi ambao hawakupelekwa katika uhamisho kule Babeli,
8
walimwendea Gedalia kule Misipa. Watu hao walikuwa Isimaeli mwana wa Netania, Yohana na Yonatani wana wa Karea, Seraya mwana wa Tanumeti, nao wana wa Efai kutoka muji Netofa, na Yezania wa muji wa Makati; wote pamoja na watu wao.
9
Gedalia aliapa mbele yao na mbele ya waaskari wao akisema: Musiogope kuwatumikia Wakaldea. Mukae katika inchi mumutumikie mufalme wa Babeli, na mambo yote yatawaendekea vema.
10
Mimi nitakaa Misipa nipate kuwa musimamizi wenu mbele ya Wakaldea watakaofika kwetu; lakini ninyi muvune matunda na mukamue divai na mafuta, mujiwekee akiba ya vitu hivyo, mukae katika miji mutakayoirizi.
11
Vilevile Wayuda waliokuwa katika inchi ya Moabu na kati ya Waamoni na katika inchi ya Edomu na inchi zingine, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli amewaruhusu Wayuda wengine kubaki katika inchi ya Yuda na kwamba amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu kuwa mutawala wao,
12
wote walirudi kutoka pahali pote walipokuwa wametawanyika na kwenda katika inchi ya Yuda kwa Gedalia kule Misipa. Walichuma zabibu na matunda mengine kwa wingi sana.
13
Basi, Yohana mwana wa Karea pamoja na wakubwa wote wa waaskari kutoka katika pori, walifika kwa Gedalia, kule Misipa, wakamwambia:
14
Uko na habari kwamba Balisi mufalme wa Waamoni, amemutuma Isimaeli mwana wa Netania, akuue? Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu hakuamini maneno yao.
15
Kisha, Yohana mwana wa Karea akazungumuza na Gedalia kwa siri kule Misipa, akamwambia: Uniruhusu niende nimwue Isimaeli mwana wa Netania, na hakuna mutu yeyote atakayejua. Kwa nini kumwachilia yeye akuue na Wayuda wote waliokusanyika hapa watawanyike na Wayuda waliobaki waangamie?
16
Lakini Gedalia mwana wa Ahikamu akamwambia Yohana mwana wa Karea hivi: Usifanye jambo hilo! Mambo unayosema juu ya Isimaeli si ya kweli!
← Chapter 39
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 41 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52