bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Jeremiah 37
Jeremiah 37
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 36
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 38 →
1
Mufalme Nebukadneza wa Babeli alimusimika Zedekia mwana wa Yosia kuwa mufalme wa Yuda pahali pa Konia mwana wa Yoyakimu.
2
Lakini Zedekia na wakubwa wake pamoja na wanainchi wa Yuda hawakusikiliza maonyo Yawe aliyotoa kwa njia ya nabii Yeremia.
3
Mufalme Zedekia aliwatuma Yehukali mwana wa Selemia, pamoja na kuhani Zefania mwana wa Maseya, kwa nabii Yeremia kusema awaombee kwa Yawe, Mungu wao.
4
Wakati huo, Yeremia alikuwa angali na uhuru wa kutembea kati ya watu, maana alikuwa hajatiwa katika kifungo.
5
Tena waaskari wa mufalme wa Misri walikuwa wameondoka Misri, na waaskari wa Wakaldea walikuwa wameuzunguka Yerusalema waliposikia habari hizo waliondoka.
6
Halafu neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:
7
Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Utamwambia mufalme wa Yuda hivi ambaye amekutuma uniombe kwa ajili yake: Waaskari wa Mufalme wa Misri waliokuja kukusaidia, wako karibu kurudia kwao Misri.
8
Na Wakaldea watarudi kuushambulia muji huu. Watauteka muji na kuuteketeza kwa moto.
9
Yawe anasema hivi: Musijidanganye wenyewe na kusema kwamba waaskari wa Wakaldea wataondoka. Kweli hawataondoka.
10
Hata kama mukiwashinda waaskari wote wa Wakaldea wanaopigana nanyi na kunabaki tu katika mahema yao wale walioumizwa, hao watasimama na kuuteketeza muji huu kwa moto.
11
Kundi la waaskari wa Wakaldea lilipoondoka Yerusalema kwa kulikimbia kundi la waaskari wa mufalme wa Misri lililokuwa linakaribia,
12
Yeremia aliondoka Yerusalema kwenda katika inchi ya Benjamina kwa kupokea sehemu ya urizi wake.
13
Alipokuwa katika mulango wa Benjamina, mulinzi mumoja anayeitwa Iria mwana wa Selemia, mujukuu wa Hanania, alimukamata Yeremia na kumwambia: Wewe unatoroka kusudi uende kujiunga na Wakaldea!
14
Yeremia akamwambia: Huo ni uongo! Mimi sitoroki na kwenda kujiunga na Wakaldea. Lakini Iria hakusadiki maneno ya Yeremia. Basi akamutia katika kifungo na kumupeleka kwa wakubwa.
15
Wakubwa hao walimukasirikia sana Yeremia wakamupiga, kisha wakamufunga katika kifungo katika nyumba ya katibu Yonatani iliyokuwa imegeuzwa kuwa gereza.
16
Yeremia alipokuwa amefungwa katika gereza kwa muda wa siku nyingi,
17
mufalme Zedekia alimwita na kumukaribisha kwake. Mufalme akamwuliza kwa siri wakiwa katika nyumba yake: Kuna neno lolote kutoka kwa Yawe? Yeremia akamujibu: Ndiyo, kuko. Kisha akaendelea kusema: Wewe utatiwa katika mikono ya mufalme wa Babeli.
18
Halafu Yeremia akamwuliza mufalme Zedekia: Nimekukosea nini, au nimewakosea nini watumishi wako au watu hawa, hata unitie katika kifungo?
19
Wako wapi manabii waliokutabiria wakisema: Mufalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala inchi hii?
20
Sasa ninakuomba unisikilize, ee bwana wangu mufalme. Ninakusihi sana ulikubali ombi langu. Tafazali usinirudishe tena katika kifungo katika nyumba ya katibu Yonatani, nisipate kukufia humo.
21
Basi, mufalme Zedekia akatoa amri Yeremia awekwe katika chumba cha walinzi na kupewa mukate kila siku kutoka kwa wapikaji wa mukate mpaka mikate ilipotoweka kabisa huko katika muji. Basi, Yeremia alibaki katika chumba cha walinzi.
← Chapter 36
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 38 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52