bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Jeremiah 42
Jeremiah 42
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 41
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 43 →
1
Kisha wakubwa wote wa waaskari, Yohanani mwana wa Karea, na Azaria mwana wa Hosaya pamoja na watu wote, wadogo kama vile wakubwa,
2
wakamwendea Yeremia, wakamwambia: Tafazali sikiliza maombi yetu na kutuombea kwa Yawe, Mungu wako, sisi wote tuliobaki, kwa maana tulikuwa wengi, lakini sasa tumebaki wachache tu, kama unavyoona.
3
Yawe, Mungu wako, atuonyeshe njia anayotaka tuifuate, na kile anachotaka tufanye.
4
Yeremia akawajibu: Vema; nimesikia. Nitamwomba Yawe, Mungu wenu, kama mulivyonisihi; jibu lolote Yawe atakalonipa, nitawaambia; sitawaficha kitu chochote.
5
Kisha, watu wakamwambia Yeremia: Yawe akuwe mushuhuda wa kweli na mwaminifu juu yetu ikiwa hatutafanya jinsi Yawe, Mungu wako atakavyokuagiza utuambie.
6
Ikuwe ni jambo la kupendeza au hapana, sisi tutaitii sauti ya Yawe, Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake kusudi mambo yatuendekee vizuri tutakapomutii Yawe, Mungu wetu.
7
Nyuma ya siku kumi, neno la Yawe lilimufikia Yeremia.
8
Basi, Yeremia akamwita Yohana mwana wa Karea, na wakubwa wote wa waaskari pamoja na watu wote, wadogo kama vile wakubwa, akawaambia:
9
Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninyi mulinituma kwake nipeleke maombi yenu, anasema hivi:
10
Kama ninyi mutabaki katika inchi hii, basi, nitawasimamisha, wala sitawaharibu; nitawaotesha wala sitawaongoa; kwa maana nitabadilisha nia kwa sababu ya hasara niliyowatendea.
11
Musimwogope mufalme wa Babeli munayemwogopa; musimwogope hata kidogo. Mimi niko pamoja nanyi kwa kuwaokoa na kuwaponyesha kutoka katika mikono yake.
12
Nitawahurumia na kumufanya mufalme awahurumie na kuwaacha katika inchi yenu. –Ni ujumbe wa Yawe.
13
Lakini mukisema: Hatutaki kubaki katika inchi hii, na hivyo mukiacha kutii sauti ya Yawe, Mungu wenu,
14
na kusema kwamba mutakwenda kukaa katika inchi ya Misri, ambako hamutaona vita wala kusikia sauti ya baragumu wala kukosa chakula,
15
basi, musikilize jinsi Yawe anavyosema enyi mabaki ya Yuda. Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama mumekusudia kwenda katika inchi ya Misri na kukaa huko,
16
basi, vita munavyoviogopa vitawakuta kulekule Misri, na njaa munayoogopa itawaandama vikali mpaka Misri, na mutakufia kulekule.
17
Watu wote wenye nia ya kwenda kukaa Misri watakufa kwa njaa na ugonjwa mukali wala hakuna hata mumoja wao atakayebaki au kuponyoka kutokana na hasara nitakayowaletea.
18
Maana Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama vile hasira yangu na kasirani yangu ilivyowapata wakaaji wa Yerusalema, ndivyo kasirani yangu itakavyowapata ninyi, kama mutakwenda Misri. Mutakuwa kitu cha kutukaniwa, kitisho, laana na haya. Hamutaona tena nafasi hii.
19
Yeremia akawaambia watu: Enyi Wayuda muliobaki, Yawe aliwaambia musiende Misri. Mujue wazi kwamba leo nimewaonya kwamba
20
mumepotoka, mumeyahatarisha maisha yenu. Maana mulinituma kwa Yawe, Mungu wenu, mukiniambia: Utuombee kwa Yawe, Mungu wetu kwamba kitu chochote Yawe, Mungu wetu, atakachosema, utuambie, nasi tutatimiza.
21
Leo mimi nimewaambia, lakini hamukutii neno lolote ambalo Yawe, Mungu wenu amenituma niwaambie.
22
Basi, mujue hakika kwamba mutauawa kwa vita, kwa njaa na kwa ugonjwa mukali katika inchi ile munayotaka kwenda kukaa ndani yake.
← Chapter 41
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 43
Chapter 44
Chapter 45
Chapter 46
Chapter 47
Chapter 48
Chapter 49
Chapter 50
Chapter 51
Chapter 52
Chapter 43 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42
43
44
45
46
47
48
49
50
51
52