bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Song of Solomon 1
Song of Solomon 1
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 2 →
1
Wimbo wa Solomono unaokuwa bora kuliko nyimbo zote.
2
Heri midomo yako ingalinibusu, maana mapendo yako ni bora kuliko divai.
3
Manukato yako yananuka vizuri, na jina lako ni kama marasi yenye harufu nzuri. Kwa hiyo wabinti wote wanakupenda!
4
Unipeleke, tuende haraka, mufalme amenileta katika chumba chake. Tutafurahi na kukushangilia pamoja, tutasifu mapenzi yako kuliko divai. Wabinti wana haki ya kukupenda!
5
Enyi wabinti wa Yerusalema, mimi ni mweusi. Ninapendeza kama mahema ya Kedari, kama mapazia ya nyumba ya Solomono.
6
Musinishangae kwa sababu mimi ni mweusi. Ni kwa sababu jua limenichoma. Wandugu zangu walinikasirikia, wakanifanya kuwa mutumishi katika mashamba ya mizabibu. Lakini sikuchunga shamba langu la mizabibu.
7
Basi uniambie ee wangu wa moyo, utawakulishia kondoo wako wapi? Ni wapi watakapopumzikia pa saa sita? Kwa nini mimi nikutafute kati ya makundi ya wenzako?
8
Ewe unayependeza kuliko wanawake wote; kama haujui, fanya hivi: ufuate nafasi kondoo walipopita; basi, uwakulishie mbuzi wako karibu na hema za wachungaji.
9
Wewe ee mupenzi wangu, ninakulinganisha na farasi dume wa magari ya Mufalme wa Misri.
10
Pete za masikio zinapendeza mashavu yako. Mikufu ya mawe ya bei kali inapendeza shingo yako.
11
Tutakufanyizia mikufu ya zahabu, iliyopambwa vizuri kwa feza.
12
Mufalme alipokuwa akiikaa kwenye meza yake, marasi yangu ya nardo yalisambaa kila pahali.
13
Mupenzi wangu ni kama mufuko wa ubani kwangu, kati ya maziba yangu.
14
Mupenzi wangu ni kama maua ya hina yanayochanua kwenye mashamba ya mizabibu kule Engedi.
15
Hakika sura yako ni nzuri, ee mupenzi wangu, hakika sura yako ni nzuri! Macho yako ni kama ya njiwa!
16
Hakika sura yako ni nzuri, ewe ninayekupenda, sura yako ni nzuri kweli! Majani mabichi yatakuwa kitanda chetu;
17
miti ya mierezi itakuwa nguzo za nyumba yetu, na miti ya miberoshi itakuwa dari yake.
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 2 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8