bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Song of Solomon 3
Song of Solomon 3
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 4 →
1
Usiku nikiwa kwenye kitanda changu, nilimutafuta yule ninayemupenda. Nilimutafuta, lakini sikumupata.
2
Nikaamuka, nikazunguka katika muji, katika barabara na nafasi za makutano, nikimutafuta yule wangu wa moyo. Nilimutafuta, lakini sikumupata.
3
Walinzi wa muji waliniona walipokuwa wanazunguka katika muji. Basi nikawauliza: Mumemwona mupenzi wangu wa moyo?
4
Mara tu nilipoachana nao, nikamwona mupenzi wangu wa moyo. Nikamushika wala sikumwacha aondoke, mpaka nilipomupeleka katika nyumba kwa mama yangu, mpaka ndani ya chumba cha yule aliyenizaa.
5
Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema, kama vile paa au swala wanavyokuwa katika pori, musichochee wala kuamusha mapenzi, mpaka pale wakati wake utakapofika.
6
Ni kitu gani kile kinachotoka katika jangwa kama munara wa moshi, kinachotoa harufu ya manemane na ubani, manukato yanayouzishwa na wachuuzi?
7
Angalia! Ni kipoyi cha Solomono, akibebwa juu ya kiti chake cha kifalme, akizungukwa na walinzi makumi sita, mashujaa bora wa Israeli.
8
Kila mumoja wao ameshika upanga, kila mumoja wao ni hodari wa vita. Kila mumoja ana upanga wake kwenye kiuno, tayari kupambana na adui usiku.
9
Mufalme Solomono alijitengenezea kipoyi, kwa mbao nzuri kutoka Lebanoni.
10
Nguzo zake zilitengenezwa kwa feza, nafasi ya kuegemea imefunikwa kwa zahabu, nafasi ya kuikalia imefunikwa na vitambaa vya nyekundu-nyeusi. Katikati yake kilipambwa na wabinti wa Yerusalema waliokishonea vitambulisho vya upendo.
11
Mukuje basi enyi wabinti wa Sayuni, mumwone mufalme Solomono. Amevaa taji aliyovalishwa na mama yake, siku alipofanya ndoa yake, siku ambayo moyo wake ulijaa furaha.
← Chapter 2
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 4 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8