bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Song of Solomon 2
Song of Solomon 2
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 1
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 3 →
1
Mimi ni kama ua la Saroni, ni yungiyungi ya mabonde.
2
Kama yungiyungi kati ya michongoma, ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa kati ya wabinti.
3
Kama muti wa matunda kati ya miti ya pori, ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa kati ya vijana. Ninafurahia kuikaa chini ya kivuli chake, na tunda lake tamu sana kwangu.
4
Alinipeleka mpaka katika chumba cha karamu, akapandisha bendera ya mapenzi juu yangu.
5
Munishibishe na zabibu kavu, munifurahishe kwa matunda, maana ninaugua kwa mapenzi!
6
Mukono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu, mukono wake wa kuume unanikumbatia.
7
Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema, kama vile paa au swala wanavyokuwa katika pori, musichochee wala kuamusha mapenzi, mpaka pale wakati wake utakapofika.
8
Hiyo ni sauti ya mupenzi wangu, yeye anakuja mbio, anaruka milima, vilima anavipita haraka!
9
Mupenzi wangu ni kama paa, ni kama swala muchanga. Anasimama karibu na ukuta wetu, anachungulia kwenye dirisha, anaangalia kwenye wavu.
10
Mupenzi wangu ananiambia, akisema: Simama basi, ewe mupenzi wangu, unayependeza, kuja tuende zetu.
11
Wakati wa baridi umepita, nazo mvua zimekwisha kukoma;
12
maua yamechanua kila pahali. Wakati wa kuimba umefika; sauti za njiwa zinasikilika katika mashamba yetu.
13
Miti ya tini imeanza kuzaa na mizabibu imechanua. Inatoa harufu nzuri. Kuja, basi, ewe mupenzi wangu unayenipendeza, kuja tuende.
14
Ee njiwa yangu, uliyejificha katika matundu kwenye mulima, uniache kuona uso wako na kusikia sauti yako, maana sauti yako ni nzuri na uso wako unapendeza.
15
Mutukamatie mbweha, wale mbweha wadogowadogo, wanaoharibu mizabibu yetu inayochanua.
16
Mupenzi wangu ni wangu, nami ni wake. Yeye anakulisha kondoo wake penye yungiyungi.
17
Mpaka pale jua linapochomoza na vivuli kutoweka, rudi kama paa, mupenzi wangu, kama swala mudogo juu ya milima ya Beteri.
← Chapter 1
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 3 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8