bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Song of Solomon 7
Song of Solomon 7
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 6
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 8 →
1
Rudia, rudia ewe binti Musulami. Rudia, rudia tupate kukuangalia. Kwa nini munataka kumwangalia Musulami sawa vile munaangalia muchezo wa ngoma kati ya makundi mawili?
2
Miguu yako inapendeza sana katika viatu, ewe binti wa kifalme. Mizunguko ya kiuno chako ni kama ushanga, kazi ya fundi hodari.
3
Kitofu chako ni kama bakuli lisilokosa divai iliyokolezwa. Tumbo lako ni kama lundo la ngano lililozungushiwa mayungiyungi pembeni.
4
Maziba yako ni kama paa mapacha, ni kama swala wawili.
5
Shingo yako ni kama munara wa pembe za tembo. Macho yako ni kama visima vya muji wa Hesiboni, karibu na mulango wa Beti-Rabi. Pua yako ni kama munara wa Lebanoni, ambao unauelekea muji wa Damasiki.
6
Kichwa chako ni kama mulima Karmeli. Misuko ya nywele zako ni nyekundu-nyeusi. Uzuri wako unaweza kumuvuta hata mufalme.
7
Angalia jinsi sura yako ni nzuri na ya kuvutia, ewe mupenzi, binti unayependeza!
8
Umbo lako linapendeza kama muti wa ngazi, maziba yako ni kama shada za ngazi.
9
Nilisema nitapanda muti wa ngazi na kuchuma shada za ngazi. Kwangu maziba yako ni kama shada za zabibu, harufu nzuri ya pumzi yako ni kama matunda ya mutofaa;
10
na kinywa chako ni kama divai tamu. Basi, divai itiririke mpaka kwa mupenzi wangu, ipite juu ya midomo yake na meno yake!
11
Mimi ni wa mupenzi wangu, naye ananisikilia hamu sana.
12
Kuja, ewe mupenzi wangu, tuende katika mashamba, tuende tulale kule katika vijiji.
13
Tutaamuka mapema, tuende kwenye mashamba ya mizabibu, tuone kama imeanza kuchipuka, na kama maua ya zabibu yamekwisha kuchanua, vilevile kama mikomamanga imeanza kutoa maua. Kule ndiko nitakapokupatia pendo langu.
14
Harufu nzuri ya dudai imejaa katika hewa. Karibu na milango yetu kuna kila aina ya matunda bora, yote mapya na ya siku za nyuma, ambayo nimekuwekea wewe mupenzi wangu.
← Chapter 6
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 8 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8