bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Song of Solomon 8
Song of Solomon 8
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 7
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
1
Heri ungekuwa kaka yangu, ambaye amenyonyeshwa na mama yangu! Hivyo, hata kama ningekutana nawe inje, ningekubusu na hakuna ambaye angenizarau.
2
Ningekuongoza na kukufikisha ndani ya nyumba ya mama muzazi, pahali ambapo ungenifundisha upendo. Ningekupa divai nzuri iliyokolezwa, ningekupa divai yangu ya makomamanga yangu.
3
Mukono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu, mukono wake wa kuume unanikumbatia.
4
Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema, musichochee wala kuamusha mapenzi, mpaka wakati wake utakapofika.
5
Ni nani huyu anayekuja kutoka katika jangwa, akimwegemea mupenzi wake? Mimi nilikuamusha chini ya muti wa mutofaa, pale ambapo mama yako aliona uchungu, pale ambapo mama yako alikuzaa.
6
Unipige kama muhuri ndani ya moyo wako, kama muhuri katika mikono yako. Maana mapendo yana nguvu kama kifo, nao wivu ni mukali kama kaburi. Kuwaka kwake ni kama kuwaka kwa moto, unawaka kama ulimi wa moto.
7
Maji mengi hayawezi kuyazimisha hata kidogo, mafuriko hayawezi kuyazimisha. Mutu akijaribu kununua mapenzi, na kutoa mali yake yote, atakachopata ni mazarau mutupu.
8
Tuna dada mudogo, ambaye bado hajaota maziba. Basi, tutamufanyia dada yetu nini siku atakapochumbiwa?
9
Kama angalikuwa ukuta, tungalimujengea munara wa feza; na kama angalikuwa mulango, tungaliupigilia kwa mbao za mierezi.
10
Mimi nilikuwa ukuta, na maziba yangu kama minara yake. Mbele yake nilikuwa kama mwenye kupata amani.
11
Solomono alikuwa na shamba la mizabibu, pahali panapoitwa Bali-Hamoni. Alilipangisha kwa walinzi; kila mumoja wao alilipa vikoroti elfu moja vya feza.
12
Shamba langu la mizabibu ni shamba langu mwenyewe. Basi, Solomono, wewe ukae na elfu zako za feza, na kila mulinzi wa matunda akae na mia mbili zake.
13
Ewe unayekuwa katika shamba, warafiki zangu wanasikiliza sauti yako; basi nami niisikilize tafazali!
14
Kuja mbio, ewe mupenzi wangu, kama paa au kitoto cha pongo juu ya milima ya marasi.
← Chapter 7
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8