bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Song of Solomon 6
Song of Solomon 6
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 7 →
1
Ewe mwanamuke unayekuwa muzuri sana, amekwenda wapi yule mupenzi wako? Ameelekea wapi mupenzi wako, kusudi tupate kushirikiana nawe kwa kumutafuta?
2
Mupenzi wangu amekwenda katika bustani yake, pahali ambapo miti ya marasi inastawi. Yeye anakulisha kondoo wake na kukusanya mayungiyungi.
3
Mimi ni wa mupenzi wangu, naye ni wangu; yeye anawakulisha kondoo wake kwenye mayungiyungi.
4
Mupenzi wangu, sura yako ni nzuri kama muji wa Tirza, unapendeza kama Yerusalema, unatisha kama jeshi lenye bendera.
5
Usiniangalie, tafazali; maana macho yako yananitisha. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi wanaoshuka kwenye milima ya Gileadi.
6
Meno yako ni kama kundi la kondoo dike wanaotoka kwenye maji kisha kuogeshwa, kila mumoja akiwa na pacha lake, na hakuna yeyote aliyekufiwa.
7
Mashavu yako ni kama nusu mbili za makomamanga ndani ya ushungi wako.
8
Kuna malkia makumi sita, wahabara makumi nane, na wabinti wasiohesabika!
9
Hakuna anayekuwa sawa njiwa yangu. Anaenea kabisa. Ni kipenzi cha mama yake, ni binti wake pekee. Wabinti wanamwangalia na kumwita mwenye heri, nao malkia na wahabara wanaimba sifa zake.
10
Ni nani huyu anayeonekana kama mapambazuko, muzuri kama mwezi, mwenye kungaa kama jua, na anatisha kama jeshi lenye bendera?
11
Nimeingia katika bustani ya miti ya lozi, kuangalia vichipukizi katika bonde, kuona kama mizabibu imechanua, na mikomamanga imechanua maua.
12
Bila kutazamia, mupenzi wangu akanitia katika gari la mukubwa.
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 7 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8