bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Song of Solomon 5
Song of Solomon 5
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 6 →
1
Ninaingia katika bustani yangu, dada yangu, muchumba wangu. Ninakusanya manemane na majani yenye harufu, ninakula sega langu la asali, ninakunywa divai yangu na maziwa yangu. Mukule, enyi warafiki, mukunywe; mukunywe sana, wapendwa wangu.
2
Nililala usingizi, lakini moyo wangu ulikesha. Nikasikia mupenzi wangu akipiga hodi. Unifungulie dada, ee mupenzi wangu, muchumba wangu, njiwa yangu, usiyekuwa na kilema chochote. Kichwa changu kimelowana na umande na nywele zangu na manyunyu ya usiku.
3
Nimekwisha kuvua nguo zangu, nitazivaa namna gani tena? Nimekwisha kunawa miguu yangu, niichafue namna gani tena?
4
Halafu mupenzi wangu akaugusa mulango, moyo wangu ukajaa furaha.
5
Nikasimama kwa kumufungulia mupenzi wangu. Mikono yangu ikajaa manemane, na vidole vyangu vikadondosha manemane, nikashika kifungio kwa kufungua mulango.
6
Nikamufungulia mupenzi wangu mulango, lakini kumbe, alikuwa amekwisha kutoweka. Moyo wangu ulifurahi alipokuwa akizungumuza! Nikamutafuta, lakini sikumupata; nikamwita, lakini hakuniitikia.
7
Walinzi wa muji walinikuta, walipokuwa wakizunguka katika muji. Wakanipiga na kuniumiza; nao walinzi wa mulango wakaninyanganya ushungi wangu.
8
Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema, mukimwona mupenzi wangu, mumwelezee kwamba ninaugua kwa ajili ya mapenzi!
9
Ewe unayependeza kuliko wabinti wote, huyo mupenzi wako ana nini cha zaidi ya mupenzi mwingine, hata utusihi kwa moyo mpaka pale?
10
Mupenzi wangu ni muzuri na ni mwekundu, anatambulikana kati ya wanaume elfu kumi.
11
Kichwa chake ni kizuri kama zahabu safi, nywele zake ni zenye kulembelea, nyeusi sana kama kibombobombo.
12
Macho yake ni kama ya njiwa kandokando ya kijito, ni kama njiwa waliooga maziwa pembeni ya kijito.
13
Mashavu yake ni kama bustani inayojaa marasi, yenye harufu nzuri. Midomo yake ni kama yungiyungi, inatonatona manemane kwa wingi.
14
Mikono yake ni kama pete za zahabu, amevaa mawe ya bei kali. Kiwiliwili chake ni kama pembe za tembo zilizopambwa kwa mawe ya yakuti ya rangi ya samawi.
15
Miguu yake ni kama nguzo za mawe meusi, zilizosimikwa katika misingi ya zahabu. Umbo lake ni kama mulima Lebanoni, ni bora kama miti ya mierezi.
16
Kinywa chake kinajaa maneno matamu. Yeye wote anapendeza. Basi, hivi ndivyo mupenzi wangu anavyokuwa, ndivyo rafiki yangu anavyokuwa, enyi wabinti wa Yerusalema.
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 6 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8