bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Proverbs 1
Proverbs 1
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 2 →
1
Hizi ni mezali za Solomono mwana wa Daudi mufalme wa Israeli.
2
Zitawawezesha watu kujua hekima na mafundisho, na kufahamu misemo yenye maana kubwa.
3
Zitawafundisha watu matendo ya hekima, haki, usawa, na sheria ya Mungu.
4
Zitawaerevusha wajinga, zitawapa vijana maarifa na akili.
5
Mwenye hekima akizisikiliza, zitamwongezea elimu; na mwenye ufahamu zitamupatia ujuzi.
6
Wataweza kuelewa mezali na maana iliyofichwa, watayaelewa maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.
7
Kumwogopa Yawe ni musingi wa maarifa, lakini wapumbafu wanazarau hekima na mafundisho.
8
Mwana wangu, sikiliza mafundisho ya baba yako, wala usizarau mashauri ya mama yako;
9
hayo yatakupamba kilemba cha neema juu ya kichwa chako, kama mukufu katika shingo yako.
10
Mwana wangu, usikubali kushawishiwa na wenye zambi.
11
Wakisema: “Twende kuvizia mutu na kumwua; kuja tuwashambulie wasiokuwa na kosa!
12
Tutawameza wakiwa wazima kama kuzimu, watakuwa kama wale wanaoshuka katika shimo.
13
Tutajitwalia mali zote za bei kali, tutazijaza nyumba zetu vitu tulivyonyanganya.
14
Kuja na ushirikiane nasi, vyote tutakavyopata tutagawanyana.”
15
Wewe mwana wangu usiandamane nao, uzuie muguu wako usifuatane nao.
16
Maana wao wako mbio kutenda maovu, haraka zao zote ni za kumwanga damu.
17
Mutego unaotegwa na ndege akiona, mutego ule unategwa bure.
18
Wao wanavizia na kujiangamiza wao wenyewe, wanatega mutego wa kujinasa wao wenyewe.
19
Ndizo njia za wanyanganyi; maisha yao yananyanganywa.
20
Hekima inapiga kelele katika barabara, inaita kwa sauti kubwa katika viwanja;
21
inaita kwenye masanganjia, inaita kwenye milango ya muji:
22
“Enyi wajinga! Mpaka wakati gani mutapenda kuwa wajinga? Mpaka wakati gani wenye kuzarau watafurahia mazarau yao, na wapumbafu kuchukia maarifa?
23
Musikilize maonyo yangu; nitawamiminia mawazo yangu, nitawajulisha maneno yangu.
24
“Nimewaita nanyi mumekataa kusikiliza, nimewanyooshea mukono mukuje nanyi hamukujali,
25
mumetupilia mashauri yangu yote, mumezarau maonyo yangu.
26
Kwa sababu hiyo, woga utakapowapata kama zoruba, hasara yenu itakapowatokea kama upepo mukali, taabu na huzuni vitakapowapata, nitachekelea hasara yenu na kuwasimanga.
28
Halafu mutaniita lakini sitaitika; mutanitafuta kwa bidii lakini hamutanipata.
29
“Muliyachukia maarifa, wala hamukuchagua kumwogopa Yawe,
30
mulikataa shauri langu, mukazarau maonyo yangu yote.
31
Basi, mutakula matunda ya mienendo yenu, mutageukiwa na mashauri yenu wenyewe.
32
Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao, wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.
33
Lakini mutu anayenisikiliza atakaa salama, atatulia bila kuogopa mabaya.”
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 2 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31