bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Proverbs 23
Proverbs 23
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 22
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 24 →
1
Ukikaa kwa kula pamoja na mutawala, usisahau hata kidogo uko pamoja na nani.
2
Zuia sana hamu yako, ikiwa wewe unapenda sana kula.
3
Usitamani vyakula vyake vizuri, maana vinaweza kukudanganya.
4
Usijichokeshe na kutafuta utajiri; acha kufikiri juu yake.
5
Macho yako yatakapokuwa yanaanza tu kuuona, nao utatoweka mara moja. Maana hakika utajiri unaota mabawa, unaruka na kutoweka katika anga kama tai.
6
Usikule chakula cha mutu muchoyo, wala usitamani vyakula vyake vizurivizuri,
7
maana ndani ya moyo wake anahesabu unachokula. Atakuambia: “Kula, kunywa!” Lakini ndani ya moyo wake hayuko pamoja nawe.
8
Utatapika vipande ulivyokula; shukrani zako zote zitakuwa za bure.
9
Usiseme maneno yako mbele ya mupumbafu, maana atazarau hekima ya maneno yako.
10
Usiondoe kitambulisho cha mupaka wa zamani, wala usinyanganye mashamba ya wayatima,
11
maana Mungu, Mukombozi wao, ni mwenye nguvu, naye atatetea haki yao nawe utaonekana kuwa na kosa.
12
Tumia akili yako kwa kufuata mafundisho; tumia masikio yako kwa kusikiliza maarifa.
13
Usiache kufundisha mutoto; ukimupiga fimbo hatakufa.
14
Ukimupiga fimbo, utayaokoa maisha yake na kuzimu.
15
Mwana wangu, moyo wako ukiwa wenye hekima, moyo wangu vilevile utakuwa wenye furaha.
16
Moyo wangu utashangilia, midomo yako itakaposema maneno ya usawa.
17
Moyo wako usiwaonee wivu wenye zambi, lakini endelea kumwogopa Yawe siku zote.
18
Hakika siku nzuri zitafika na tumaini lako halitakuwa la bure.
19
Sikia, mwana wangu, ukuwe na hekima; fikiri sana jinsi unavyoishi.
20
Usikuwe mumoja kati ya walevi wa divai, wala walafi wenye kupenda nyama,
21
maana walevi na walafi wataishia kuwa wamasikini. Usingizi utawavalisha nguo za kupasukapasuka.
22
Umusikilize baba yako aliyekuzaa, wala usimuzarau mama yako akizeeka.
23
Nunua ukweli, wala usiuuzishe; nunua hekima, mafundisho na akili.
24
Baba wa mutoto mwenye haki atajaa furaha; anayezaa mutoto mwenye hekima atamufurahia.
25
Uwafurahishe baba na mama yako; mama yako aliyekuzaa afurahi.
26
Mwana wangu, unisikilize kwa uangalifu, ufuate mwenendo wa maisha yangu.
27
Kahaba ni kama shimo refu; mwanamuke mugeni ni kama kisima chembamba.
28
Yeye anavizia kama munyanganyi, anasababisha wanaume wengi kukosa uaminifu.
29
Ni nani wenye taabu? Ni nani wenye huzuni? Ni nani wenye ugomvi? Ni nani wenye malalamiko? Ni nani wenye vidonda bila sababu? Ni nani wenye macho mekundu?
30
Ni wale ambao hawabanduki penye divai, wale ambao wanatafuta divai iliyochanganywa.
31
Usiitamani divai hata kwa wekundu wake, hata kama inametameta katika kilauri, na kushuka vizuri unapoikunywa.
32
Kwa mwisho inauma kama nyoka; inachoma kama fira mwenye sumu.
33
Macho yako yataona mambo ya ajabu, moyo wako utatoa mambo yaliyopotoka.
34
Utakuwa kama mutu anayelala katikati ya bahari, kama mutu anayelala juu ya mulingoti wa mashua.
35
Utasema: “Nimepigwa, lakini sikuumia; wamenipondaponda, lakini sikusikia kitu. Nitaamuka saa gani kusudi nitafute kinywaji kingine?”
← Chapter 22
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 24 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31