bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Proverbs 8
Proverbs 8
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 7
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 9 →
1
Musikilize! Hekima inaita! Akili inapiga kelele yake!
2
Juu kwenye vilima karibu na njia na katika masanganjia ndipo ilipojiweka.
3
Karibu na milango ya kuingilia katika muji, pahali wanapoingilia watu inaita kwa sauti:
4
“Enyi watu wote, ninawaita ninyi! Wito wangu ni kwa ajili ya wanadamu.
5
Enyi wajinga, mujifunze kuwa na akili; musikilize kwa uangalifu, enyi wapumbafu.
6
Musikilize maana nitakachosema ni jambo la lazima; katika midomo yangu mutatoka mambo ya haki.
7
Kinywa changu kitasema kweli mutupu; uovu ni chukizo katika midomo yangu.
8
Kinywa changu kitasema maneno ya haki, hakuna udanganyifu wala upotevu katika midomo yangu.
9
Kwa mutu mwenye ufahamu kila kitu ni wazi, kwa mwenye maarifa yote imesawanishwa.
10
Chagua mafundisho yangu pahali pa feza; na maarifa pahali pa zahabu safi.
11
“Hekima ina maana sana kuliko mawe ya bei kali; kitu chochote unachotamani hakiwezi kulingana nayo.
12
Mimi Hekima nina ujuzi; nina maarifa na akili.
13
Kumwogopa Yawe ni kuchukia uovu. Ninachukia kiburi, majivuno maisha mabaya, na luga mbaya.
14
Nina uwezo wa kushauri na kuamua vizuri. Nina ufahamu na nina nguvu.
15
Kwa musaada wangu watawala wanatawala na wakubwa wanaagiza kwa haki.
16
Kwa musaada wangu viongozi wanaongoza na wakubwa wanaamua.
17
Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.
18
Utajiri na heshima viko kwangu, mali ya kudumu na fanaka.
19
Matunda yangu ni mazuri kuliko zahabu safi, na faida yangu inashinda ya feza bora.
20
Ninatembea katika njia ya haki; ninafuata sheria ya Mungu.
21
Ninawatajirisha wale wanaonipenda, ninajaza tele hazina za wanaonipenda.
22
“Yawe aliniumba kwa mwanzo wa kazi yake, zamani za kale mbele ya kuumbwa kwa kitu chochote.
23
Nilifanywa kwa mwanzo wa nyakati, nilikuwa niko mbele ya dunia kuanza.
24
Nilizaliwa mbele ya vilindi vya bahari, mbele ya chemichemi zinazobubujika maji.
25
Nilizaliwa mbele milima na vilima havijaumbwa,
26
mbele Mungu hajaumba dunia na mashamba yake, wala chembe za kwanza za mavumbi ya dunia.
27
Nilikuwa niko wakati alipoweka mbingu, wakati alipofanya muviringo juu ya bahari;
28
wakati alipoimarisha mawingu mbinguni, alipofanya imara chemichemi za bahari,
29
wakati alipowekea bahari mupaka wake kusudi maji yake yasipate kuvunja amri yake, wakati alipoweka misingi ya dunia.
30
Nilikuwa pamoja naye kama fundi wa kazi, nilikuwa furaha yake kila siku, nikishangilia mbele yake siku zote,
31
nikifurahia dunia na wakaaji wake, na kupendezwa kuwa pamoja na wanadamu.
32
“Sasa basi, wana wangu, munisikilize: heri wale wanaofuata njia zangu.
33
Musikilize mafundisho mupate hekima, wala musiyakatae.
34
Heri mutu anayenisikiliza, anayeikaa kila siku kwenye mulango wangu, anayekesha karibu na milango yangu.
35
Anayenipata mimi amepata uzima, na upendeleo kutoka kwa Yawe.
36
Asiyenipata anajizuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”
← Chapter 7
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 9 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31