bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Proverbs 13
Proverbs 13
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 12
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 14 →
1
Mutoto mwenye hekima anasikia maagizo ya baba yake, lakini mwenye kiburi hasikilizi maonyo.
2
Mutu muzuri anapata uzuri kutokana na maneno yake, lakini mudanganyifu anaishi kwa kutesa kwa ukali.
3
Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.
4
Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.
5
Mwenye haki anachukia uongo, lakini mwovu anatenda kwa kupatisha haya na mazarau.
6
Haki inalinda wenye mwenendo sawa, lakini zambi inaangusha waovu.
7
Kuna mutu anayejidai kuwa tajiri, kumbe hana kitu. Mwengine anajiona kuwa masikini wakati ana mali tele.
8
Ukombozi wa uzima wa mutu ni mali yake, lakini masikini hana njia ya kujikomboa.
9
Mwenye haki anaangaa kama vile taa inayowaka vizuri, lakini waovu ni kama taa inayozimika.
10
Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.
11
Mali ya harakaharaka inatoweka, lakini anayekusanya kidogokidogo ataiongeza.
12
Tumaini la kungojangoja linaumiza moyo, lakini tazamio linalotimia ni musingi wa uzima.
13
Anayezarau mashauri anajiletea maangamizi, lakini anayetii amri atapewa zawadi.
14
Mafundisho ya wenye hekima ni chemichemi ya uzima; inamwezesha mutu kuepuka mitego ya kifo.
15
Kuwa na akili kunaleta ukubali, lakini njia ya waovu ni ya taabu.
16
Mwenye akili anatenda kila kitu kwa kufikiri, lakini mupumbafu anatembeza upumbafu wake.
17
Mujumbe mubaya anawatumbukiza watu katika taabu, lakini mujumbe mwaminifu analeta amani.
18
Umasikini na mazarau vinamupata yule asiyejali mafundisho, lakini mwenye kusikia maonyo anaheshimiwa.
19
Ni jambo la kufurahisha unapopata kile unachotaka, kwa hiyo wapumbafu wanachukia kuepuka uovu.
20
Anayeandamana na wenye hekima anapata hekima, lakini anayejiunga na wapumbafu atapata hasara.
21
Wanaotenda zambi wanapatwa na hasara, lakini wenye haki wanafanikiwa.
22
Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.
23
Shamba la masikini linatoa mazao mengi, lakini linanyanganywa juu ya wale wanaopotosha haki.
24
Asiyemwazibu mutoto wake hamupendi; lakini anayemupenda mwana wake atamwazibu kwa wakati.
25
Mwenye haki yuko na chakula cha kumutoshelea, lakini tumbo la waovu linataabika kwa njaa.
← Chapter 12
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 14 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31