bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Proverbs 28
Proverbs 28
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 27
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 29 →
1
Waovu wanakimbia ijapokuwa hawafukuzwi na mutu, lakini wenye haki ni hodari kama simba.
2
Taifa lenye fujo lina viongozi wengi, lakini kwa kiongozi mumoja mwenye akili na maarifa kuna utengemano.
3
Mutu mwenye hitaji anayewatesa wamasikini, anafanana na mvua kubwa inayoharibu mimea.
4
Watu wanaovunja sheria wanasifu waovu, lakini wanaoshika sheria wanapingana nao.
5
Waovu hawaelewi haki ya sheria, lakini wanaomwogopa Yawe wanaielewa kabisa.
6
Afazali masikini mwenye mwenendo mukamilifu, kuliko tajiri anayeishi kwa upotovu.
7
Mutoto anayeshika sheria ni mwenye hekima, lakini rafiki wa walafi anafezehesha baba yake.
8
Anayeongeza mali yake kwa mazidio na kulipisha faida, anamukusanyia mwingine mwenye kuwahurumia wamasikini.
9
Anayekataa kuisikia sheria, yule, hata maombi yake, ni chukizo kwa Mungu.
10
Anayepotosha mutu wa usawa katika njia mbaya, ataanguka katika shimo lake mwenyewe. Wakamilifu watarizi mazuri.
11
Tajiri anajiona mwenyewe kuwa mwenye hekima, lakini masikini mwenye akili atamufichua.
12
Watu wa haki wakipata madaraka, kuna utukufu mukubwa. Lakini waovu wakitawala, watu wanajificha.
13
Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.
14
Heri mutu anayemwogopa Yawe siku zote, lakini mwenye moyo mugumu atapata hasara.
15
Mutawala mwovu anayetawala wamasikini ni kama simba anayenguruma au dubu anayeshambulia.
16
Mutawala asiyekuwa na akili anawagandamiza sana watu, lakini anayechukia mali ya udanganyifu atatawala kwa muda murefu.
17
Mutu anayelemewa na kosa ya kuua mutu, atakuwa mukimbizi mpaka katika kaburi. Mutu yeyote asijaribu kumusaidia.
18
Mwenye mwenendo mukamilifu ataponyeshwa, lakini munafiki wa njia mbili ataanguka mara moja.
19
Anayelima shamba lake atapata chakula kingi, lakini anayefuata mambo yasiyofaa atapata umasikini tele.
20
Mutu mwaminifu atapata baraka tele, lakini mwenye pupa ya kuwa tajiri hataepuka azabu.
21
Si vizuri kumubagua mutu. Watu wanafanya mabaya hata kwa ajili ya mukate.
22
Mutu muchoyo anakimbilia mali, wala hajui kwamba ukosefu utamufikia.
23
Anayemwonya mwenzake kwa mwisho atasifiwa naye, kuliko yule anayemubembeleza kwa maneno matamu.
24
Anayeiba mali ya baba yake au ya mama yake na kusema si kosa, anatumika pamoja na yule anayeangamia.
25
Muchoyo anachochea magomvi, lakini anayetegemea Yawe atafanikiwa.
26
Anayetegemea akili yake mwenyewe ni mupumbafu; lakini anayeishi kwa hekima atakuwa salama.
27
Anayesaidia wamasikini hatakosewa kitu, lakini anayekataa kuwaangalia atalaaniwa kwa wingi.
28
Waovu wakitawala, watu wanajificha. Lakini wakiangamia, wenye haki wanaongezeka.
← Chapter 27
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 29 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31