bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Proverbs 22
Proverbs 22
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 21
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 23 →
1
Afazali kuwa na sifa nzuri kuliko mali mengi. Kupata kukubaliwa ni bora kuliko feza au zahabu.
2
Watajiri na wamasikini wana hali hii moja: Yawe ni Muumba wao wote.
3
Mwenye akili anaona hatari na kujificha, lakini wajinga wanajitokeza mbele na kuumia.
4
Ukinyenyekea na kumwogopa Yawe, utapata zawadi ya fanaka, heshima, na uzima.
5
Njia ya waovu imejaa miiba na mitego; anayetaka kulinda maisha yake ataiepuka.
6
Umufundishe mutoto njia anayopaswa kufuata, naye hataiacha hata katika uzee.
7
Tajiri anamutawala masikini. Mwenye kukopesha ni mutumwa wa mwenye kukopeshwa.
8
Anayepanda ubaya atavuna hasara. Uwezo wake wa kutenda mabaya utavunjwa.
9
Mutu mwenye kuwa tayari kusaidia atabarikiwa, maana anagawanya chakula chake na masikini.
10
Umufukuze mwenye kiburi na fujo itatoweka, na ugomvi na matusi vitakoma.
11
Mwenye nia safi na maneno mazuri atakuwa rafiki wa mufalme.
12
Yawe analinda maarifa lakini anayavuruga maneno ya waovu.
13
Muvivu anasema: “Kuna simba inje. Nitauawa katika njia.”
14
Kinywa cha mwasherati ni shimo refu; anayechukiwa na Yawe atatumbukia ndani yake.
15
Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mutoto, lakini fimbo ya kufundisha itaufukuza mbali.
16
Anayemutesa masikini kwa kujitajirisha na anayewapa watajiri zawadi, wote wawili wataishia kuwa wamasikini.
17
Tega sikio usikie maneno ya wenye hekima; elekeza moyo wako kwa maarifa yangu.
18
Wewe utafurahi kama utayaweka ndani ya moyo, na kuyarudiliarudilia kila wakati.
19
Ninayependa kumufundisha leo ni wewe, kusudi tumaini lako likuwe kwa Yawe.
20
Nimekuandikia misemo makumi tatu, misemo ya maonyo na maarifa,
21
kwa kukufundisha mambo yanayokuwa sawa na kweli; na mutu akikuuliza upate kumupa jibu la kweli.
22
Usinyanganye masikini mali yake kwa sababu ni masikini, wala usimunyime mukosefu haki yake katika tribinali.
23
Maana Yawe atawatetea; atagandamiza maisha ya wale wanaowagandamiza.
24
Usifanye urafiki na mutu wa hasira, wala usiandamane na mwenye kukasirika upesi.
25
Usijifunze mwenendo wake, na kujinasa kabisa katika mutego.
26
Usikuwe mumoja wa wale ambao wanajitoa rehani kwa madeni ya wengine.
27
Ikiwa hauna chochote cha kulipa, hata kitanda unacholalia kitanyanganywa!
28
Usiondoe kitambulisho cha mupaka wa zamani, ambacho kiliwekwa na babu zako.
29
Kuna mutu mwenye akili na maarifa ndani ya kazi? Yule atawatumikia wafalme; hatawatumikia watu wasiofaa.
← Chapter 21
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 23 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31