bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Proverbs 24
Proverbs 24
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 23
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 25 →
1
Usiwaonee wivu watu waovu, wala usitamani kuwa pamoja nao,
2
maana mafikiri yao yote ni juu ya kutesa tu, nayo midomo yao inasema mabaya.
3
Nyumba inajengwa kwa hekima, na kuimarishwa kwa ufahamu.
4
Kwa maarifa vyumba vyake vinajazwa vitu vya bei kali na vya kupendeza.
5
Kuwa na hekima na maarifa ni bora kuliko kuwa na nguvu.
6
Maana kwa mipango mizuri unaweza kupigana vita, na kwa washauri wengi ushindi unapatikana.
7
Kwa mupumbafu hekima ni ngumu kuielewa; penye mukutano wa mashauri hafungui mudomo.
8
Anayefikiria kutenda maovu siku zote, ataitwa mutu mwenye fitina.
9
Mupango mupambafu anaofikiri ni zambi; mwenye kuzarau anachukiwa na kila mutu.
10
Ukiregea wakati wa shida, basi wewe ni muzaifu kweli.
11
Umwokoe mutu anayepelekwa kuuawa kwa bure; usisite kumwopoa anayeuawa bila kosa.
12
Usiseme kisha: “Hatukujua!” Maana Mungu anayepima mioyo ya watu anaona; yeye atakulipa kulingana na matendo yako!
13
Mwana wangu, ukule asali maana ni nzuri; sega la asali ni tamu katika kinywa chako.
14
Ndivyo hekima itakavyokuwa katika nafsi yako; ukiipata, siku nzuri zitakuja na tumaini lako halitakuwa la bure.
15
Usivizie kama mwovu kwa kushambulia makao ya mutu wa haki, wala usijaribu kuharibu nyumba yake,
16
maana mutu wa haki anaanguka mara nyingi naye anainuka tena, lakini mutu mwovu anaangamizwa na hasara.
17
Usishangilie kuanguka kwa adui yako; usifurahie ndani ya moyo wako kujikwaa kwake,
18
maana Yawe akiona yale hatapendezwa; ataacha kumuazibu.
19
Usihangaike kwa sababu ya watenda mabaya, wala usiwaonee wivu watu waovu,
20
maana siku mbaya zitamufikia mwovu; taa ya uzima wake itazimika.
21
Mwana wangu, uwaheshimu Yawe na mufalme, wala usishirikiane na waasi,
22
maana maangamizi yatawatokea kwa rafla. Hakuna anayejua magumu watakayoleta.
23
Hii ni misemo mingine ya wenye hekima. Kupendelea watu katika hukumu si vizuri.
24
Anayemwachilia mutu mwenye kosa analaaniwa na watu na kuchukiwa na mataifa.
25
Lakini wanaowaazibu waovu watapata furaha, na baraka nzuri zitawafikia.
26
Jibu linalokuwa la haki ni kama busu la rafiki.
27
Kwanza fanya kazi zako inje na kutayarisha kila kitu katika shamba. Kisha jenga nyumba yako.
28
Usishuhudie bure juu ya jirani yako, wala usiseme uongo juu yake.
29
Usiseme: “Nitamutendea kama vile alivyonitendea! Inapasa kulipiza kisasi!”
30
Nilipitia karibu na shamba la muvivu, ni kusema shamba la mizabibu la mutu mupumbafu,
31
niliona kwamba lilikuwa limeota miiba, majani yalikuwa yamefunika eneo lake lote, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
32
Niliangalia, nikawaza. Kwa mwisho nikapata fundisho:
33
Lala tu kidogo, sinzia tu kidogo, kunja mikono yako tu upumzike,
34
lakini kumbuka kwamba unapokuwa katika usingizi, umasikini utakufikia kama munyanganyi, ukosefu kama mutu mwenye silaha.
← Chapter 23
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 25 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31