bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Proverbs 11
Proverbs 11
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 10
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 12 →
1
Mizani danganyifu ni chukizo kwa Yawe, lakini matumizi ya vipimo vya haki ni furaha kwake.
2
Kiburi kinazaa haya, lakini kwa watu wanyenyekevu kuna hekima.
3
Ukamilifu wa watu wa usawa unawaongoza. Upotovu wa wadanganyifu unawaangamiza.
4
Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.
5
Haki ya watu wakamilifu inanyoosha njia yao, lakini waovu wanaanguka kwa uovu wao wenyewe.
6
Haki ya watu wa usawa inawaokoa na hatari, lakini wafitini wananaswa kwa tamaa zao wenyewe.
7
Mwovu akikufa, tumaini lake nalo linatoweka. Tumaini la asiyemwogopa Mungu ni la bure.
8
Mutu wa haki anaokolewa katika shida, na mwovu anaingia mule kwa pahali pake.
9
Asiyemwogopa Mungu anaangamiza wengine kwa kinywa chake, lakini mwenye haki anaokolewa kwa maarifa yake.
10
Watu wa haki wakipata fanaka, muji unashangilia. Waovu wakiangamia, watu wanapiga vigelegele.
11
Muji unafanikishwa kwa baraka za watu wa usawa, lakini unaangamizwa kwa kinywa cha waovu.
12
Anayemuzarau jirani yake hana akili; mutu mwenye ufahamu anakaa kimya.
13
Anayepitapita akichongea anatoa siri, lakini anayeaminiwa anaficha siri.
14
Pasipo uongozi taifa linaanguka; kwenye kuwa washauri wengi kuna usalama.
15
Anayejitoa kulipia mugeni deni yake atajuta, lakini anayechukia mapatano yale ana usalama.
16
Mwanamuke mwema anaheshimiwa; wanaume wenye nguvu wanatajirika.
17
Mutu mwema anafaidika yeye mwenyewe, lakini mutu mukali anajiumiza mwenyewe.
18
Faida mwovu anayopata ni ya uongo, lakini anayetenda mema, hakika atapata faida.
19
Mutu anayekusudia kuwa mwenye haki ataishi, lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.
20
Wenye nia mbaya ni chukizo kwa Yawe, lakini wenye mwenendo mukamilifu ni furaha yake.
21
Hakika mwovu hataepuka kuazibiwa, lakini wenye haki wataokolewa.
22
Mwanamuke muzuri asiyekuwa na akili ni kama pete ya zahabu kwenye pua la nguruwe.
23
Matazamio ya wenye haki yana matokeo mazuri; tamaa za waovu zinaleta kasirani.
24
Kuna watu wanaotoa mali yao kwa wingi na kuzidi; lakini wachoyo wanazilinda na kuendelea katika umasikini.
25
Mutu anayetoa kwa moyo safi atafanikishwa. Mutu anayekunywesha mwingine maji, naye atakunyweshwa.
26
Watu wanamulaani mutu anayeficha ngano, lakini wanamutakia baraka mwenye kuiuzisha.
27
Anayetafuta kutenda mazuri anapata upendeleo, lakini anayetafuta kutenda maovu atapatwa na maovu.
28
Anayetegemea mali zake ataanguka, lakini mwenye haki atastawi kama jani bichi.
29
Anayevunja nyumba yake, atavuna upepo. Mupumbafu atakuwa mutumwa wa wenye hekima.
30
Tunda la mwenye haki ni muti wa uzima, na mwenye hekima anavuta watu.
31
Ikiwa mwenye haki anapata malipo hapa katika dunia, hakika mwovu na mwenye zambi watalipwa!
← Chapter 10
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 12 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31