bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Job 13
Job 13
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 12
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 14 →
1
Sikia! Hayo yote nimeyaona kwa macho yangu. Nimeyasikia kwa masikio yangu mwenyewe na kuelewa.
2
Yote munayoyajua, mimi vilevile ninayajua. Mimi si mutu wa akili ndogo kuliko ninyi.
3
Lakini ningependa kusema na Mungu Mwenye Uwezo, ninatamani kujitetea mbele ya Mungu.
4
Lakini ninyi munapakaa uongo chokaa, ninyi wote ni waganga wasiofaa kitu.
5
Heri mungekaa kimya kabisa, muonekane kwamba muna hekima!
6
Musikilize basi utetezi wangu, munisikilize ninapojitetea.
7
Munazani munamutumikia Mungu kwa kusema uongo na udanganyifu?
8
Munajaribu kumupendeza Mungu? Mutamutetea Mungu katika tribinali?
9
Akiwachunguza, ninyi mutapona? Au munazani munaweza kumudanganya Mungu kama watu?
10
Hakika yeye atawakaripia kama mukionyesha upendeleo kwa siri.
11
Utukufu wake hauwatishi? Hamupatwi na hofu juu yake?
12
Masemi yenu ni mezali za majivu, maneno yenu ni ukuta wa udongo.
13
Munyamaze, nami niseme. Kitu kitakachonipata, kinipate.
14
Niko tayari hata kuhatarisha maisha yangu.
15
Mungu aniue akitaka; sina la kupoteza. Hata hivyo nitautetea mwenendo wangu mbele yake.
16
Kama nikiweza kwa hiyo nitakuwa nimeshinda, maana mutu mwovu hawezi kwenda mbele yake.
17
Musikilize kwa uangalifu maneno yangu, maelezo yangu yatue katika masikio yenu.
18
Maneno yangu nimeyatarisha jinsi inavyofaa. Ninajua kwamba sina kosa.
19
Nani atakayebishana nami? Niko tayari kunyamaza na kufa.
20
Mungu wangu, unijalie tu mambo haya mawili, nami sitajificha mbali na wewe:
21
kwanza uniondolee mukono wako unaonipiga, na usiniogopeshe kwa kitisho chako.
22
Uanze kusema maneno yako nami nikujibu. Au mimi nianze, nawe unijibu.
23
Makosa na zambi zangu ni ngapi? Unijulishe kosa na zambi yangu.
24
Mbona unageuza uso wako mbali nami? Kwa nini unanitendea kama adui yako?
25
Utatikisatikisa jani linalopeperushwa, au kukimbiza nyasi iliyokauka?
26
Wewe umetoa mashitaki makali juu yangu, na kunibebesha zambi za ujana wangu.
27
Unanifunga minyororo kwenye miguu, unachunguza njia zangu zote, umeichapa miguu yangu.
28
Nami ninaisha kama muti uliooza, kama nguo iliyokuliwa na nondo.
← Chapter 12
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 14 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42