bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Job 36
Job 36
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 35
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 37 →
1
Kisha Elihu akaendelea kusema:
2
Univumilie kidogo, nami nitakuonyesha kitu; maana ningali bado na cha kusema kwa ajili ya Mungu.
3
Nitaleta hekima yangu kutoka mbali sana, na kuonyesha kwamba Muumba wangu ni wa haki.
4
Kweli maneno yangu si ya uongo; mwenye elimu kamili yuko hapa nawe.
5
Sikia! Mungu ni mwenye nguvu wala hamuzarau mutu yeyote; uwezo wa akili yake ni mukubwa sana!
6
Hawaachilii waovu waendelee kuishi; lakini anawapatia wanaoteswa haki zao.
7
Haachi kuwalinda watu wa haki; nao anawaweka kuwa wafalme watawale na kutukuzwa.
8
Lakini kama watu wakifungwa minyororo, wakinaswa katika kamba za mateso,
9
Mungu anawaonyesha matendo yao maovu, na kwamba wao ni watu wenye kiburi.
10
Anafungua masikio wasikie mafundisho, na kuwaamuru warudi na kuacha uovu.
11
Wakimutii Mungu na kumutumikia, wanafanikiwa katika siku zao zote; miaka yao yote inakuwa ya furaha.
12
Lakini wasipomutii, wanaangamia kwa upanga, na kufa kwa kukosa akili.
13
Waovu wanapenda kukasirika; hawamwombi musaada anapowafunga.
14
Wanakufa wangali bado vijana, maisha yao yanaisha kama ya washerati.
15
Lakini Mungu anawaokoa wenye kuteswa kwa mateso yao, anatumia shida zao kwa kuwafumbua macho.
16
Mungu alikutoa katika taabu, akakuweka pahali pakubwa pasipo shida, na juu ya meza yako amekutayarishia vyakula vizuri.
17
Lakini sasa umehukumiwa kama mwovu, hukumu ya haki imekupata.
18
Angalia kasirani isikuvute kwa kuzarau, au usiache ukubwa wa mali za kukukomboa ukupotoshe.
19
Kilio chako kitafaa kukutoa katika taabu, au nguvu zako zote zitakusaidia?
20
Usitamani usiku ukuje, ambapo watu wanapotoweka.
21
Angalisho! Usielekee uovu maana umepewa mateso kwa kukuepusha na uovu.
22
Kumbuka ukubwa wa uwezo wa Mungu; nani anayeweza kufundisha kama yeye?
23
Nani basi aliyeweza kumupangia njia yake, au anayeweza kumwambia: “Umekosa”?
24
Usisahau kusifu matendo yake ambayo watu wameyashangilia.
25
Watu wote wameona mambo Mungu aliyofanya; mwanadamu anayaona kutoka mbali.
26
Mungu ni mukubwa sana hata hatuwezi kumujua; muda wa maisha yake hauchunguziki.
27
Yeye anayavuta kwake maji ya bahari, na kutoka ukungu anafanya matone ya mvua.
28
Anayafanya mawingu yanyeshe mvua, na kuwatiririshia wanadamu kwa wingi.
29
Nani anayejua jinsi mawingu yanavyotanda, au jinsi radi inavyonguruma kwake katika anga?
30
Yeye anatandaza umeme wake kumuzunguka, na kuvifunika vilindi vya bahari.
31
Kwa mvua anawakulisha watu na kuwapatia chakula kwa wingi.
32
Anaukamata umeme kwa mikono yake, kisha anapiga nao shabaha.
33
Radi inatangaza kuja kwa Mungu; hata nyama wanajua kwamba anakuja.
← Chapter 35
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 37
Chapter 38
Chapter 39
Chapter 40
Chapter 41
Chapter 42
Chapter 37 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36
37
38
39
40
41
42