bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 15
Deuteronomy 15
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 14
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 16 →
1
“Kila mwisho wa mwaka wa saba mutawasamehe wote wenye kuwa na madeni yenu.
2
Hivi ndivyo mutakavyofanya: kila mumoja aliyemukopesha mwenzake, afute lile deni, wala asijaribu kumudai kwa sababu Yawe mwenyewe ameamua deni hilo lifutwe.
3
Munaweza kuwadai wageni, lakini madeni yote ya wandugu zenu wenyewe mutayafuta.
4
“Yawe, Mungu wenu atawabariki katika inchi anayowapa ikuwe urizi wenu. Hakuna hata mumoja atakayekuwa masikini kati yenu,
5
ikiwa tu mutamutii Yawe, Mungu wenu, kwa kufuata kwa uangalifu amri ninazowapa hivi leo.
6
Yawe, Mungu wenu, atawabariki kama vile alivyowaahidi. Nanyi mutayakopesha mataifa mengi, lakini ninyi hamutakopa. Vilevile mutatawala mataifa mengi, lakini mataifa hayo hayatawatawala ninyi.
7
“Kukiwa masikini wa jamaa yenu katika miji ya inchi ambayo Yawe atawapa, musikuwe wachoyo na wagumu kwake.
8
Pahali pake, mufungue mikono yenu na kumukopesha kwa mapenzi kiasi cha kutosha mahitaji yake.
9
Muangalie wazo ovu lisiwaingie ndani ya mioyo yenu, mukisema: ‘Mwaka wa saba, mwaka wa kusamehe wadeni uko karibu’. Mukimwangalia ndugu yenu masikini na jicho baya na kukataa kumupa chochote, yeye anaweza kumulilia Yawe juu yenu na hiyo itakuwa zambi kwenu.
10
Mumupe ndugu masikini kwa moyo safi bila kunungunika, maana kwa ajili ya hayo, Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote na katika kila munalofanya.
11
Wamasikini hawatakosekana katika inchi; hivyo ninawaamuru, mukuwe wenye moyo safi kwa wandugu zenu wenye mahitaji na wamasikini katika inchi yenu.
12
“Kama ndugu Mwebrania, mwanaume au mwanamuke, akiuzishwa kwako, atakutumikia kwa miaka sita, lakini katika mwaka wa saba, utamwacha huru.
13
Nawe utakapomwacha huru, usimwache aende mikono mitupu.
14
Umupe kwa moyo safi kile ambacho Yawe amekubariki nacho: kondoo, ngano na divai.
15
Mukumbuke kwamba ninyi mulikuwa watumwa huko Misri na Yawe, Mungu wenu, aliwakomboa; ndiyo maana leo ninawaamuru hivyo.
16
Lakini akikuambia: ‘Sitaondoka kwako’, kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako na anaishi vizuri kwako,
17
basi, utatwaa chuma na kutoboa sikio lake mpaka chuma hicho kiingie ndani ya mulango naye atakuwa mutumwa wako milele. Utamutendea mujakazi wako namna hiyohiyo.
18
Wala usione ugumu utakapomwacha huru mutumwa wako, maana, amekutumikia kwa muda wa miaka sita kwa nusu ya mushahara wa mutumishi wa kulipwa. Fanya hivyo, naye Yawe, Mungu wako, atakubariki kwa kila utakalofanya.
19
“Umutolee Yawe, Mungu wako, wazaliwa wote wa kwanza dume wa kundi lako la ngombe na kondoo. Usiwafanyizishe ngombe hao kazi na kondoo hao usiwakate manyoya.
20
Kila mwaka, wewe na jamaa yako mutakula nyama hao mbele ya Yawe, Mungu wenu, pahali Yawe atakapochagua.
21
Lakini nyama huyo akiwa na kilema chochote, ni kusema kiwete au kipofu, au ana kilema chochote kikubwa, usimutoe kuwa sadaka kwa Yawe, Mungu wako.
22
Utakula nyama wa namna hiyo ukiwa katika muji wako; vilevile wote wanaokuwa safi na wasiokuwa safi wanaweza kumukula kama vile unavyokula paa au kulungu.
23
Lakini usikule damu yake; hiyo utaimwanga chini kama vile maji.
← Chapter 14
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 16 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34