bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 32
Deuteronomy 32
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 31
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 33 →
1
Utege sikio, ee mbingu. Sikiliza, ee dunia, maneno ninayosema.
2
Mafundisho yangu yatone kama mvua, maneno yangu yadondoke kama umande, kama manyunyu kwenye mimea michanga, kama mvua nyepesi katika majani mabichi.
3
Maana nitatangaza jina la Yawe, nanyi museme: “Mungu wetu ni Mukubwa”.
4
Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.
5
Lakini ninyi mumekosa uaminifu kwake, ninyi sio watoto wake tena kwa sababu ya uovu, ninyi ni kizazi kiovu na kipotovu.
6
Munaweza namna gani kumulipa hivyo Yawe, enyi watu wapumbafu na wasiokuwa na akili? Yeye siye baba yenu aliyewaumba, aliyewafanya na kuwaimarisha?
7
Mukumbuke siku zilizopita, mufikiri miaka ya vizazi vingi. Muulize baba zenu nao watawajulisha, muulize wakubwa wenu nao watawaelezea.
8
Mungu Mukubwa alipogawanyia mataifa mali yao, alipowagawanyia wanadamu, kila taifa alilipatia mipaka yake, kulingana na hesabu ya wamalaika,
9
lakini alijiwekea watu wa Yakobo kuwa wake, hao alijichagulia kuwa mali yake.
10
Yawe alikuta Waisraeli katika inchi ya jangwa, jangwa tupu zenye upepo mukali. Aliwalinda na kuwatunza. Aliwakinga kama mboni ya jicho lake.
11
Alikuwa kama tai anayelinda chicha yake, anayeruka karibu ya vitoto vyake, akitandaza mabawa yake kwa kuwashikilia, na kuwabeba juu ya mabawa yake.
12
Yeye Yawe mwenyewe aliwaongoza na hakukuwa mungu mwingine wa kumusaidia.
13
Aliwapitisha katika inchi za juu za vilima, nao wakakula mazao ya mashamba. Akawapa asali kutoka katika mawe waonje na mafuta kutoka katika jiwe gumu.
14
Aliwapa siagi na maziwa ya mifugo, mafuta ya wana-kondoo na kondoo dume, makundi ya mifugo ya Basani na mbuzi. Aliwapa ngano nzuri kabisa na divai mupya wakakunywa.
15
Watu wa usawa walinona, wakapiga mateke. Walinenepa sana, kisha wakamwacha Mungu aliyewaumba, wakazarau Mulima wa wokovu wao.
16
Wakamufanya aone wivu mukali kwa miungu yao, wakamuchochea akasirike kwa matendo yao ya kuchukiza.
17
Wakatambikia pepo ambazo hazikukuwa miungu, wakaendea miungu ambayo hawakuijua hata kidogo, miungu mipya iliyotokea kwa siku za karibu, ambayo wazee wao hawakuiheshimu hata kidogo.
18
Hamukumujali Mulima wenu, yule aliyewapa uzima. Mulimusahau Mungu aliyewazaa ninyi.
19
Yawe aliona jambo hilo akawaacha; aliwakataa watoto wake, wanaume na wanawake.
20
Akasema hivi: Nitawaficha uso wangu nione mwisho wao utakuwa namna gani. Maana wao ni kizazi kipotovu, watoto wasiokuwa na uaminifu wowote.
21
Wamenichochea kuona wivu kwa kitu kisichokuwa mungu, wamenikasirikisha kwa sanamu zao. Hivyo nitawafanya waone wivu juu ya watu wa bure, nitawakasirikisha kwa kutumia taifa la wapumbafu.
22
Hasira yangu imewaka moto, inachoma mpaka chini kuzimu, itateketeza dunia na vinavyokuwa ndani yake, itaunguza misingi ya milima.
23
Nitalundika hasara nyingi juu yao, nitawamalizia mishale yangu.
24
Watakonda kwa njaa, wataangamizwa kwa homa kali. Nitaleta nyama wenye meno makali kuwashambulia, na nyoka wenye sumu wanaotambaa juu ya mavumbi.
25
Vita itasababisha vifo vingi inje, na ndani ya nyumba hofu itawatawala. Vijana wanaume na wanawake watauawa, hata wenye kunyonya na wazee wenye imvi.
26
Ningaliwaangamiza kabisa na kuwafanya wasikumbukwe tena na mutu yeyote,
27
isipokuwa tu kwa sababu ya majivuno ya waadui zao, kusudi waadui zao wasifikiri kwamba wamepata kuwaangamiza, nami Yawe sikufanya kitu katika mambo haya!
28
Israeli ni taifa lisilokuwa na akili, watu wake hawana ufahamu ndani yao.
29
Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa, wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwa namna gani.
30
Mutu mumoja anaweza namna gani kuwashinda watu elfu moja, au watu wawili wanaweza namna gani kuwashinda watu elfu kumi, isipokuwa kama mulinzi wao amewatupa, Yawe amewaacha?
31
Hata waadui zetu wenyewe wanajua wazi, mulinzi wao hana nguvu kama mulinzi wetu.
32
Maana mizabibu yao ni mizabibu ya Sodoma, zimetoka katika mashamba ya Gomora. Zabibu zake ni zabibu zenye sumu, vishada vyake ni vichungu.
33
Divai yao ni kama sumu ya nyoka, ina sumu kali ya nyoka kubwa.
34
Sina njia ya kuwaazibu? Silaha zangu ziko katika mukono wangu.
35
Ni kazi yangu kulipiza kisasi, mimi nitalipiza, wakati miguu yao itakapoteleza; maana siku yao ya hasara imefika mwisho wao uko karibu sana.
36
Yawe atawatetea watu wake, na kuwahurumia watumishi wake, wakati atakapoona nguvu zao zimeisha wala hakuna aliyebaki, mufungwa au mutu huru.
37
Ndipo Yawe atakapouliza watu wake: Iko wapi ile miungu yenu, mulinzi muliyekimbilia usalama?
38
Iko wapi hiyo miungu iliyokula matoleo yenu na kunywa divai na sadaka zenu za kinywaji? Basi isimame, iwasaidie; muache hiyo ikuwe ulinzi wenu sasa!
39
Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.
40
Ninanyoosha mukono wangu mbinguni na kuapa: Kama vile ninavyoishi milele,
41
nitanoa upanga wangu unaometemeta, nitanyoosha mukono kutoa hukumu, nitawalipiza kisasi waadui zangu, nitawaazibu wale wanaonichukia.
42
Mishale yangu nitailewesha kwa damu, upanga wangu utashiba nyama, utalowana na damu ya vidonda na wafungwa na waadui wenye nywele ndefu.
43
Enyi mataifa, mushangilie watu wake, maana yeye analipiza kisasi damu ya watumishi wake, anawalipiza kisasi wapinzani wake, na kuitakasa inchi ya watu wake.
44
Musa alikuja mbele ya Yoshua, mwana wa Nuni, wakarudilia maneno ya wimbo huu, kusudi Waisraeli wote wausikie.
45
Musa alipomaliza kuwaambia watu wa Israeli maneno haya yote,
46
akawaambia: “Muweke ndani ya mioyo yenu maneno yote ambayo ninawapa leo. Muwaamuru watoto wenu kusudi wafuate kwa uaminifu maneno yote ya sheria hii.
47
Maana sheria hii si maneno matupu lakini ni uzima wenu; kwa njia ya sheria hii, mutaishi maisha marefu katika inchi munayokwenda kurizi, ngambo ya muto Yordani.”
48
Siku hiyohiyo, Yawe akamwambia Musa:
49
“Panda juu ya mulima huu wa Abarimu, mulima Nebo katika inchi ya Moabu, kuelekea muji wa Yeriko, uiangalie inchi ya Kanana ninayowapa Waisraeli wairizi.
50
Kulekule juu ya mulima utakufa na kukutana na wazee wako kama vile kaka yako Haruni alivyokufa katika mulima Hori na kukutana nao,
51
kwa sababu ninyi wote wawili mulivunja uaminifu wenu kwangu mbele ya Waisraeli mulipokuwa kwenye maji ya Meriba, karibu na muji wa Kadesi, katika jangwa la Sini. Mukakosa kuhakikisha utakatifu wangu kati ya Waisraeli.
52
Utaona inchi inayokuwa mbele yako, lakini hautaingia katika inchi hiyo ninayowapa Waisraeli.”
← Chapter 31
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 33 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34