bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Deuteronomy 26
Deuteronomy 26
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 25
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 27 →
1
“Na kisha kufika na kurizi inchi ambayo Yawe, Mungu wenu anawapa ikuwe yenu na kuishi huko,
2
utatwaa malimbuko ya mazao utakayovuna katika inchi Yawe, Mungu wenu, anayokupa, na kuyaweka katika kikapu mpaka pale pahali ambapo Yawe, Mungu wenu, amechagua pawe makao yake.
3
Utamwendea kuhani anayetumika wakati huo, na kumwambia: ‘Leo ninashuhudia mbele ya Yawe, Mungu wangu, kwamba nimeingia katika inchi aliyowaapia wazee wetu kwamba atatupatia’.
4
“Naye kuhani atakapotwaa kikapu hicho toka mikono yako na kukiweka mbele ya mazabahu ya Yawe, Mungu wako,
5
utasema maneno haya mbele ya Yawe, Mungu wako: ‘Baba yangu alikuwa Musuria aliyetangatanga huko na huko, kisha akashuka kwenda Misri akaishi huko kama mugeni. Yeye na jamaa yake walikuwa watu wachache tu walipokuwa huko, lakini wakakuwa taifa kubwa lenye nguvu na watu wengi.
6
Wamisri walitutendea kwa ukali wakatutesa na kutulazimisha kufanya kazi ngumu ya watumwa.
7
Kisha tukamulilia Yawe, Mungu wa wazee wetu, akasikia kilio chetu, na kuona mateso yetu, kazi ngumu na mateso tulizozipata.
8
Basi, Yawe akatutoa huko Misri kwa mukono wake wa nguvu ulionyooshwa, kwa vitisho, vitambulisho na maajabu.
9
Akatuleta hapa na kutupatia inchi hii inayotiririka maziwa na asali.
10
Na sasa ninamuletea Yawe malimbuko ya mazao ya inchi ambayo amenipa’. “Kisha utaweka kikapu chini, mbele ya Yawe, Mungu wako, na kuabudu mbele yake.
11
Nawe utafurahia mema yote ambayo Yawe, Mungu wako, amekujalia wewe na jamaa yako. Nao watafurahi pamoja nawe.
12
Kila nyuma ya miaka mitatu, kila mumoja wenu atatoa sehemu ya kumi ya mazao yake yote kwa ajili ya Walawi na wageni, wayatima na wajane, kusudi wapate chakula chote wanachohitaji wanapokuwa katika miji yenu.
13
Kisha utasema mbele ya Yawe, Mungu wako, hivi: ‘Nimetoa katika nyumba yangu fungu takatifu, nikawapa Walawi, wageni, wayatima na wajane, kama vile ulivyoniamuru nifanye. Sijavunja amri zako wala sijasahau.
14
Sikukula sehemu ya kumi yoyote nilipokuwa ninaomboleza; sikuitoa inje ya nyumba yangu nilipokuwa muchafu na sikutoa sehemu ya kumi hiyo kwa wafu. Nimekutii ee Yawe, Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoamuru juu ya sehemu ya kumi.
15
Uangalie chini kutoka makao yako matakatifu mbinguni, uwabariki watu wako Israeli na inchi uliyotupatia kama vile ulivyowaapia wazee wetu; inchi inayotiririka maziwa na asali’.
16
“Leo hii, Yawe, Mungu wenu, anawaamuru kushika masharti na maagizo haya. Mukuwe waangalifu kuyatimiza kwa moyo wote na roho yote.
17
Leo Yawe ameahidi kwamba atakuwa Mungu wenu, kama mutafuata njia zake na kushika masharti, amri, na maagizo yake na kutii sauti yake.
18
Nanyi mumeahidi kwamba mutakuwa watu wake yeye mwenyewe na kwamba mutashika amri zake zote.
19
Atawafanya ninyi kuwa taifa kubwa kuliko mataifa yote aliyoumba. Nanyi mutatetea jina lake, sifa yake na heshima yake. Ninyi mutakuwa watakatifu wake kama vile alivyosema.”
← Chapter 25
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 27 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34