bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 1
2 Chronicles 1
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 2 →
1
Solomono, mwana wa mufalme Daudi, alijiimarisha katika utawala wake, naye Yawe, Mungu wake akamubariki na kumufanya akuwe mukubwa sana.
2
Mufalme Solomono aliita majemadari wote wa vikundi vya maelfu na vya mamia, waamuzi, viongozi wote wa ukoo za Waisraeli.
3
Kisha akaandamana nao mpaka pahali pa ibada kule Gibeoni. Walikwenda kule kwa sababu pale ndipo pahali palipokuwa hema la mukutano la Mungu ambalo Musa mutumishi wa Yawe, alilotengeneza katika jangwa.
4
(Lakini, sanduku la Mungu lilikuwa Yerusalema katika hema ambalo mufalme Daudi alilipigia alipolileta kutoka Kiriati-Yearimu).
5
Tena, mazabahu ya shaba iliyotengenezwa na Bezaleli, mwana wa Uri na mujukuu wa Huri, ilikuwa kule Gibeoni mbele ya hema takatifu la Yawe. Hapo mufalme Solomono na watu wote wakamwomba Yawe.
6
Solomono akapanda mbele ya mazabahu ya shaba iliyokuwa kwenye hema la mukutano. Pale mbele ya Yawe, akatoa sadaka elfu moja za kuteketezwa juu ya mazabahu yale.
7
Usiku ule, Mungu akamutokea Solomono, akamwambia: “Omba kitu chochote unachotaka, nami nitakupa.”
8
Solomono akamwambia Mungu: “Ulimutendea baba yangu Daudi mema mengi, na umenijalia kuwa mufalme kwa pahali pake.
9
Sasa, ee Mungu, Yawe, utimize ahadi uliyomupa Daudi baba yangu. Umeniweka kuwa mufalme juu ya watu hawa wanaokuwa wengi kama mavumbi.
10
Kwa hiyo, ninakuomba unipe hekima na maarifa kusudi niweze kuwatawala watu wako vizuri. Kama sivyo, nitaweza namna gani kuwatawala hawa watu wako wanaokuwa wengi hivi?”
11
Mungu akamujibu Solomono: “Kwa sababu jambo hili uliloomba liko ndani ya moyo wako, na wala haukuomba mali, wala utajiri, wala heshima wala haukuomba wanaokuchukia waangamizwe, wala maisha marefu, lakini umeomba hekima na maarifa kusudi uwatawale vizuri watu wangu ambao nimekupa ukuwe mufalme wao,
12
ninakupa hekima na maarifa. Vilevile, nitakupa utajiri, mali na heshima zaidi ya mufalme mwingine yeyote aliyekuwa mbele yako na mufalme mwingine yeyote atakayetawala nyuma yako.”
13
Basi, Solomono akaondoka pahali pale pa kuabudia, kule Gibeoni, kulipokuwa hema la mukutano, akarudi Yerusalema. Akatawala inchi ya Israeli.
14
Solomono alikusanya magari ya vita na waaskari wapanda-farasi; alikuwa na magari ya vita elfu moja na mia ine, na waaskari wapanda-farasi elfu kumi na mbili. Aliwaweka katika miji yenye vituo vya magari ya vita na kwake katika Yerusalema.
15
Mufalme Solomono aliongeza feza na zahabu zikakuwa nyingi kama mawe katika Yerusalema, na mbao za mierezi zikapatikana kwa wingi kama mikuyu ya Sefela.
16
Farasi wa Solomono walitoka Misri na Kilikia; wachuuzi wake waliwanunua toka kule.
17
Walinunua gari moja la vita kutoka Misri kwa bei ya vikoroti mia sita za feza, na farasi mumoja kwa vikoroti mia moja na makumi tano za feza. Kisha waliwauzishia wafalme wa Wahiti na wa Wasuria farasi hao na magari.
18
Mufalme Solomono akakusudia kujenga nyumba ambamo Yawe ataabudiwa, na vilevile kujijengea yeye mwenyewe nyumba ya kifalme.
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 2 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36