bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 20
2 Chronicles 20
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 19
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 21 →
1
Nyuma ya mambo hayo, majeshi ya Wamoabu na Waamoni pamoja na sehemu ya Wameuni wakashambulia inchi ya Yuda.
2
Watu wamoja wakakuja kumwambia mufalme Yosafati: “Jeshi kubwa limekuja kukushambulia kutoka Edomu, ngambo ya bahari ya Chumvi. Tayari wamekwisha kufika Hazazoni-Tamari.” (Hili ni jina lingine la Engedi).
3
Yosafati akashikwa na woga, akamwomba Yawe amwongoze. Akatangaza kwamba watu wote katika inchi ya Yuda wafunge kula.
4
Watu wakakuja Yerusalema kutoka miji yote ya Yuda, wakakusanyika kwa kumwomba Yawe awasaidie.
5
Yosafati akasimama katikati ya kusanyiko la watu wa Yuda na Yerusalema mbele ya kiwanja kipya cha nyumba ya Yawe,
6
akaomba kwa sauti akisema: “Ee Yawe, Mungu wa babu zetu, wewe ndiwe Mungu unayekuwa mbinguni! Wewe unatawala falme zote katika dunia, una uwezo na nguvu, wala hakuna anayeweza kukupinga.
7
Si wewe, ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa inchi hii wakati watu wako Waisraeli walipoingia katika inchi hii, ukawapa wazao wa Abrahamu rafiki yako, ikuwe yao milele?
8
Nao wamekaa humu, na kukujengea hekalu kwa heshima ya jina lako, wakijua
9
kwamba wakipatwa na hasara yoyote, azabu, vita, ugonjwa mukali, au njaa, basi watakuja na kusimama mbele ya nyumba hii mbele yako, wakulilie katika shida zao, nawe utawasikiliza na kuwaokoa.
10
Sasa Waamoni, Wamoabu na watu wa mulima Seiri, ambao haukuwaruhusu babu zetu washambulie inchi zao walipotoka Misri, wakapitia kandokando wasiwaangamize,
11
angalia, jinsi wanavyotulipa. Wanakuja kutuondoa katika inchi yako uliyoturizisha ikuwe urizi wetu.
12
Wewe ndiwe Mungu wetu! Uwaazibu, maana sisi hatuna uwezo wowote mbele ya jeshi kubwa kama hili linalotufikia. Hatujui la kufanya lakini tunatazamia musaada kutoka kwako.”
13
Wanaume wote wa Yuda, pamoja na wake zao na watoto wao, walikuwa wakisimama pale mbele ya Yawe.
14
Halafu Roho wa Yawe akamujaza Mulawi mumoja aliyekuwa pale. Jina lake Yahazieli mwana wa Zakaria, aliyekuwa mwana wa Benaya, mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, wa ukoo wa Asafu.
15
Yahazieli akasema: “Musikilize ninyi watu wa Yuda na wakajii wa Yerusalema na mufalme Yosafati, Yawe anawaambia hivi: musiogope wala musihangaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Vita hivi si vyenu, lakini ni vya Mungu.
16
Kesho muwashambulie wakati watakapokuwa wakipanda Bonde la Sisi. Mutawakuta mwisho wa bonde, upande wa mashariki wa jangwa la Yerueli.
17
Hamutahitaji kupigana vita hivi. Ninyi mujipange tu halafu mungojee, na mutaona Yawe akiwashinda kwa jina lenu. Enyi watu wa Yuda na Yerusalema, musiogope wala musifazaike. Muende kwa vita, naye Yawe atakuwa pamoja nanyi!”
18
Kisha mufalme Yosafati akainama uso mpaka chini pamoja na watu wote wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema na kumwabudu Yawe.
19
Walawi na ukoo wa Kohati na Kora, wakasimama na kumusifu Yawe, Mungu wa Israeli, kwa sauti kubwa sana.
20
Kesho yake, wakaamuka asubui mapema, wakaenda mpaka katika jangwa la Tekoa. Walipokuwa wanaondoka, Yosafati akasimama, akawaambia: “Musikilize, enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema! Mumwamini Yawe, Mungu wenu, nanyi mutakuwa imara. Muwaaminie manabii wake, nanyi mutashinda.”
21
Nyuma ya kushauriana na watu, mufalme akachagua waimbaji kwa kumwimbia Yawe wavae nguo zao takatifu kisha watangulie mbele ya jeshi, wakiimba: “Mumushukuru Yawe, maana wema wake unadumu milele!”
22
Wakati walipoanza kuimba na kusifu, Yawe akawavuruga akili waaskari Waamoni, Wamoabu na watu wa mulima Seiri waliokuja kupigana na Yuda. Na waaskari wale wakashindwa.
23
Waamoni na Wamoabu wakawashambulia wenyeji wa mulima Seiri, na kuwaangamiza kabisa. Kisha kuwaangamiza wakaaji wa mulima Seiri wakaanza kushambuliana wao kwa wao, wakaangamizana.
24
Jeshi la Yuda lilipofika kwenye munara wa ulinzi kule katika jangwa, wakaangalia upande wa waadui, wakaona maiti zimesambaa kila pahali. Hakuna mutu yeyote aliyeponyoka.
25
Yosafati na waaskari wake wakaenda kukamata vitu. Wakakuta ngombe wengi, mali, nguo na vitu vingine vya bei kali. Iliwachukua muda wa siku tatu kusomba vitu hivyo, na hata hivyo, hawakuvimaliza maana vilikuwa vingi sana.
26
Siku ya ine wakakusanyika katika Bonde la Sifa, na kumusifu Yawe kwa yote aliyowafanyia. Hii ndiyo sababu bonde hilo linaitwa Bonde la Sifa mpaka hivi leo.
27
Kisha Yosafati akawaongoza waaskari wake mpaka Yerusalema kwa shangwe, kwa sababu Yawe aliwashinda waadui zao.
28
Walipofika Yerusalema, walikwenda moja kwa moja mpaka kwenye nyumba ya Yawe, wakipiga vinanda, vinubi na baragumu.
29
Falme zote zikaingiwa na hofu ziliposikia jinsi Yawe alivyowashinda waadui za Israeli.
30
Basi, Yosafati akatawala kwa amani, na Mungu akamupa amani pande zote.
31
Yosafati alikuwa na umri wa miaka makumi tatu na mitano alipoanza kutawala inchi ya Yuda. Alitawala kutoka Yerusalema kwa muda wa miaka makumi mbili na tano. Jina la mama yake ni Azuba binti ya Silihi.
32
Yosafati alitenda mema mbele ya Yawe kama vile Asa baba yake alivyofanya.
33
Lakini hakuharibu pahali pa kutambikia sadaka juu ya kilima. Watu walikuwa wangali hawajamugeukia na kumwabudu Mungu wa babu zao kwa mioyo yao.
34
Matendo mengine ya Yosafati, kutoka mwanzo wa utawala wake mpaka mwisho, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Yehu mwana wa Hanani, ambacho kiko katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli.
35
Nyuma ya hayo, Yosafati mufalme wa Yuda, akajiunga na Ahazia mufalme wa Israeli, aliyetenda mambo maovu.
36
Walishirikiana kutengeneza mashua za kusafiri mpaka Tarsisi, walizitengenezea kule Esioni-Geberi.
37
Lakini Eliezeri mwana wa Dodawa, kutoka muji wa Maresa, akatoa unabii juu ya Yosafati, akisema: “Kwa sababu umejiunga na Ahazia, Yawe atavunja mashua zote mulizotengeneza.” Na mashua zile zilivunjikavunjika; kwa hiyo hazikuweza kusafiri mpaka Tarsisi.
← Chapter 19
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 21 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36