bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 23
2 Chronicles 23
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 22
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 24 →
1
Katika mwaka wa saba kuhani Yoyada akajipa moyo akafanya mapatano na majemadari: Azaria mwana wa Yoramu, Isimaeli mwana wa Yohanani, Azaria mwana wa Obedi, Maseya mwana wa Adaya, na Elisafati mwana wa Zikiri.
2
Wakazunguka katika miji yote ya Yuda wakiwakusanya Walawi na viongozi wa makabila ya Israeli, wakaenda mpaka Yerusalema.
3
Mukutano wote ukafanya agano na mufalme katika nyumba ya Mungu. Yoyada akawaambia: “Muangalie huyu mwana wa mufalme! Mumwache atawale kulingana na ahadi Yawe aliyotoa juu ya uzao wa Daudi.
4
Hivi ndivyo mutakavyofanya: sehemu moja ya tatu ya kundi lenu ninyi makuhani na Walawi mutakaoshika zamu siku ya Sabato, mutalinda milango,
5
sehemu moja ya tatu ingine italinda nyumba ya kifalme na sehemu iliyobakia mutalinda Mulango wa Musingi. Watu wote watakuwa katika viwanja vya nyumba ya Yawe.
6
Asikubaliwe mutu mwingine yeyote kuingia ndani ya nyumba ya Yawe isipokuwa makuhani tu pekee na wale Walawi watakaokuwa wanatumika. Hao wanaweza kuingia kwa sababu wao ni watakatifu, lakini wale watu wengine wote, watatii amri ya Yawe.
7
Walawi watamuzunguka mufalme, kila mutu na silaha yake katika mukono; na mutu yeyote atakayejaribu kuingia katika nyumba ya Yawe, atauawa. Mukae na mufalme anapoingia ndani na anapotoka inje.”
8
Walawi na watu wa Yuda walitii amri zote kuhani Yoyada alizotoa. Kila mukubwa akawatwaa watu wake wote, wale waliokuwa wamemaliza zamu na wale waliokuwa wanaingia kushika zamu siku ya Sabato; kwa sababu Yoyada hakuwaruhusu waondoke.
9
Kisha kuhani Yoyada akawapa majemadari mikuki na ngao kubwa na ndogo zilizokuwa mali ya mufalme Daudi, na ambazo zilikuwa zimewekwa katika nyumba ya Yawe.
10
Kisha, akawapanga watu wote kuanzia upande wa kusini mpaka upande wa kaskazini wa nyumba na kuzunguka mazabahu na nyumba, kila mumoja silaha yake katika mikono, kwa kumulinda mufalme.
11
Halafu wakamutoa mwana wa mufalme inje wakamuvalisha taji juu ya kichwa, na kumupa ule ushuhuda; wakamuweka kuwa mufalme nao Yoyada na wana wake wakamupakaa mafuta kisha watu wakashangilia wakisema: “Mufalme aishi milele!”
12
Naye Malkia Atalia aliposikia sauti za watu wakikimbia na kumushangilia mufalme akawaendea hao watu waliokuwa katika nyumba ya Yawe.
13
Alipochungulia akamwona mufalme mupya akisimama karibu na nguzo kwenye mulango, wakati majemadari na wapiga baragumu wakiwa kando ya mufalme na wakaaji wote wakishangilia na kupiga baragumu; nao waimbaji wakiwa na ala zao za muziki wakiongoza watu katika sherehe; halafu akapasua nguo yake na kusema kwa sauti kubwa: “Uasi! Uasi!”
14
Kisha kuhani Yoyada akawatoa inje majemadari wa jeshi akisema: “Mumutoe Atalia inje katikati ya waaskari; yeyote atakayemufuata auawe kwa upanga,” kwa sababu hakutaka wamwue katika nyumba ya Yawe.
15
Basi, wakamukamata, na akaingia katika njia ya mulango wa Farasi wa nyumba ya kifalme, wakamwua huko.
16
Yoyada akafanya agano kati yake mwenyewe, watu wote, na mufalme kwamba watakuwa watu wa Yawe.
17
Halafu watu wote wakaenda kwenye nyumba ya Bali na kuibomoa wakavunja mazabahu pamoja na sanamu zake, hata wakamwua Matani, kuhani wa Bali, mbele ya mazabahu.
18
Kuhani Yoyada akaweka walinzi kwa kulinda nyumba ya Yawe. Hao walinzi wakasimamiwa na makuhani na Walawi ambao Daudi aliwaweka katika kazi ya kutunza nyumba ya Yawe kutoa sadaka za kutetezwa kwa moto kwa Yawe kama vile ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, wakishangilia na kuimba kwa kufuata amri ya Daudi. Vilevile wakasimamia mambo ya uimbaji na sherehe.
19
Akaweka walinzi kwenye milango ya nyumba ya Yawe kusudi mutu yeyote anayehesabiwa kuwa muchafu kwa njia moja au nyingine asiingie.
20
Alitwaa majemadari wa jeshi, waheshimiwa, watawala wa watu, na wakaaji wote; nao wakamusindikiza mufalme kutoka nyumba ya Yawe, wakapitia katika mulango wa juu mpaka kwenye nyumba ya kifalme. Kisha wakamuikalisha mufalme kwenye kiti cha kifalme.
21
Kwa hiyo wakaaji wote wakajaa na furaha; na muji wote ukakuwa mutulivu nyuma ya Atalia kuuawa kwa upanga.
← Chapter 22
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 24 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36