bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 32
2 Chronicles 32
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 31
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 33 →
1
Nyuma ya matendo hayo ya uaminifu ya mufalme Hezekia, mufalme Saniharibu wa Asuria akashambulia inchi ya Yuda. Akakuja kupiga makambi kwenye miji yenye kuta akitumaini kwamba ataishinda ikuwe mali yake.
2
Mufalme Hezekia alipoona kwamba mufalme Saniharibu amekuja kwa kusudi la kuishambulia Yerusalema,
3
akaamua, yeye pamoja na wakubwa wake na wakubwa wa majeshi kufunga maji ya chemichemi zilizokuwa inje ya miji; nao wakamuunga mukono, wakamusaidia.
4
Wakawakusanya watu wengi pamoja, wakazifunga chemichemi zote pamoja na kijito kilichopitia kati ya sehemu hiyo wakisema: “Kwa nini kuwaachia wafalme wa Asuria, wakikuja wakute maji tele?”
5
Hezekia akajitia moyo, akajenga upya ukuta wote uliokuwa umebomoka, na juu yake akajenga minara. Upande wa inje, akajenga ukuta mwingine wa pili, na akaiimarisha uwanja wa Milo katika muji wa Daudi. Zaidi ya hayo akatengeneza silaha na ngao kwa wingi.
6
Akaweka watu wote wa muji chini ya uongozi wa majemadari, kisha akawaamuru wakusanyike katika uwanja penye Mulango wa Muji. Hapo akawatia moyo akisema:
7
“Muwe imara na hodari. Musiogope wala musifazaike mbele ya mufalme wa Asuria au majeshi yake maana tunayekuwa naye ni mukubwa kuliko anayekuwa na Saniharibu.
8
Yeye ana nguvu za kibinadamu tu, lakini sisi tuna Yawe, Mungu wetu, kwa kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Maneno haya ya mufalme Hezekia yakawatia moyo sana watu wale.
9
Nyuma ya hayo, Saniharibu mufalme wa Asuria, ambaye alikuwa angali anauzunguka muji wa Lakisi akiwa na majeshi yake yote, akawatuma watumishi wake Yerusalema kwa Hezekia mufalme wa Yuda na kwa watu wote wa inchi ya Yuda waliokuwa Yerusalema, akisema:
10
“Hivi ndivyo Saniharibu mufalme wa Asuria anavyosema: Munategemea nini hata munakaa Yerusalema, muji ambao umezungukwa?
11
Si Hezekia ndiye anayewadanganya mukufe kwa njaa au kiu anapowaambia: ‘Yawe, Mungu wenu atawaokoa toka mikono ya mufalme wa Asuria?’
12
Si ni huyu Hezekia ndiye aliyeharibu pahali pake pa kuabudia na mazabahu zake na kuwaamuru watu wote wa inchi ya Yuda na Yerusalema akisema: ‘Mutaabudu mbele ya mazabahu moja, na juu yake mutateketeza sadaka zenu?’
13
Hamujui yale yote ambayo mimi na babu zangu tumewatendea watu wote wa inchi zingine? Miungu ya watu wa inchi hizo iliweza kukomboa inchi zao toka mikono yangu?
14
Ni mungu gani kati ya miungu ya mataifa yale yaliyoharibiwa kabisa na babu zangu aliyeweza kuwakomboa watu wake kutoka katika mikono yangu ndiyo nanyi mukuwe na tumaini kwamba Mungu wenu atawaokoa toka mikono yangu?
15
Musidanganywe na Hezekia wala musishawishiwe kwa hayo. Musimwamini mutu huyu, kwa maana hakujatokea mungu wa taifa au mufalme yeyote aliyeweza kuwakomboa watu wake kutoka mikono ya mufalme wa Asuria. Vile vile mungu wenu hataweza!”
16
Watumishi wa mufalme wa Asuria walisema maneno mengine mengi mabaya juu ya Mungu wetu Yawe na juu ya Hezekia mutumishi wake.
17
Mufalme mwenyewe aliandika barua akamutukana na kumuzarau Yawe, Mungu wa Israeli, akisema: “Kama vile ambavyo miungu ya inchi zingine haikuweza kuwaokoa watu wao kutoka mikono yangu, vile vile mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake.”
18
Wakubwa wale wakawaambia kwa sauti kubwa kwa luga ya Kiebrania, watu wa Yerusalema waliokuwa juu ya ukuta, wakikusudia kuwatia hofu na woga kusudi wakamate muji.
19
Wakasema juu ya Mungu wa Yerusalema kama vile wangesema juu ya miungu ya mataifa mengine ambayo ni sanamu tu zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
20
Halafu mufalme Hezekia na nabii Isaya, mwana wa Amozi, wakamwomba Mungu na kumulilia awasaidie kwa ajili ya mambo haya.
21
Naye Yawe akatuma malaika aliyewaua waaskari shujaa, majemadari na wakubwa katika kambi ya mufalme wa Asuria. Basi, mufalme wa Asuria akarudia katika inchi yake akijaa haya. Mara tu alipoingia ndani ya nyumba ya mungu wake, wana wake mwenyewe wakamwua palepale kwa upanga.
22
Kwa njia hii basi, Yawe akamwokoa mufalme Hezekia na wakaaji wa Yerusalema kutoka mukono wa Saniharibu mufalme wa Asuria, na kutoka mukono wa waadui zake wote. Akawapa maisha ya amani na wajirani zao wote.
23
Watu wengi sana walikuja wakamuletea Yawe sadaka kule Yerusalema, vilevile wakamuletea Hezekia, mufalme wa Yuda zawadi za bei kali. Hivyo kutoka wakati ule, akasifiwa sana na mataifa mengine yote.
24
Wakati ule, Hezekia akagonjwa sana, karibu kufa. Akamwomba Yawe, naye akamujibu na kumwonyesha kitambulisho.
25
Lakini Hezekia hakumutolea Yawe shukrani kwa yale yote aliyomutendea kwa sababu moyo wake ulikuwa umejaa majivuno. Hii ikasababisha kutaabika kwa inchi ya Yuda na Yerusalema.
26
Kwa hiyo kasirani ikakuwa juu yake, juu ya inchi ya Yuda na juu ya Yerusalema. Kisha Hezekia akanyenyekea akaacha kuwa na moyo uliojaa majivuno, yeye na wakaaji wa Yerusalema wakajinyenyekeza; kwa hiyo kasirani ya Yawe haikuwafikia wakati wa utawala wa Hezekia.
27
Mufalme Hezekia akatajirika sana na kuheshimiwa. Alijitengenezea hazina za feza, za zahabu, za mawe ya bei kali za viungo, ngao na za aina zote za vyombo vya bei kubwa.
28
Vilevile alijijengea nyumba za kuwekea mazao ya ngano, divai na mafuta, na mazizi kwa ajili ya ngombe na mengine kwa ajili ya kondoo.
29
Vile vile alijiongezea miji kwa ajili yake mwenyewe, makundi mengi ya ngombe na kondoo kwa sababu Yawe alimupa mali nyingi.
30
Mufalme Hezekia ndiye aliyefunga maji ya chemichemi ya Gihoni, akayachimbia mufereji na kuyapitisha chini moja kwa moja mpaka upande wa magaribi wa muji wa Daudi. Hezekia alijaliwa katika kila jambo alilofanya,
31
na hata wakati ambapo wajumbe wa wakubwa wa Babeli waliotumwa kwake kuuliza juu ya mambo ya ajabu yaliyotokea mule, Mungu, alimwacha ajiamulie mwenyewe, kusudi amupime na kujua yote yaliyokuwa ndani ya moyo wake.
32
Matendo mengine ya mufalme Hezekia na wema wake, yameandikwa katika “Maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi,” katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda na Israeli.
33
Hezekia akakufa na kuzikwa kwenye sehemu ya juu ya makaburi ya wafalme. Watu wote wa inchi ya Yuda na wakaaji wa Yerusalema wakamutolea heshima kubwa wakati wa kifo chake, naye Manase, mwana wake, akatawala pahali pake.
← Chapter 31
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 33 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36