bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 12
2 Chronicles 12
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 13 →
1
Wakati Rehoboamu alipoimarisha utawala wake, yeye pamoja na watu wake wote waliacha kutii Sheria ya Yawe.
2
Katika mwaka wa tano wa utawala wake, kwa sababu hawakumutii Yawe, Sisaki, mufalme wa Misri akashambulia muji wa Yerusalema,
3
akiwa na magari elfu moja na mia mbili, waaskari wapanda-farasi elfu makumi sita. Alikuwa vilevile na waaskari wengi sana wasioweza kuhesabiwa toka Misri; Walibia, Wasuki na Waetiopia.
4
Aliteka miji yenye kuzungukwa na kuta katika Yuda, akafika mpaka Yerusalema.
5
Kisha Nabii Semaya akamwendea mufalme Rehoboamu na wakubwa wa Yuda, waliokusanyika Yerusalema ambapo walikimbilia kwa kumwepuka Sisaki, akamwambia: “Yawe anasema hivi: ‘Ninyi mumeniacha mimi, kwa hiyo basi, nami nimewaacha ninyi na kuwatia katika mikono ya Sisaki.’ ”
6
Halafu wakubwa wa Israeli na mufalme wakajinyenyekeza, wakasema: “Yawe ni mwenye haki.”
7
Yawe alipoona kwamba wamejinyenyekeza, akazungumuza tena na nabii Semaya, akamwambia: “Wamejinyenyekeza, sitawaangamiza, lakini nitawaokoa nyuma ya muda mufupi. Sitashushia muji Yerusalema kasirani yangu na kuuharibu kwa mukono wa Sisaki,
8
lakini watamutumikia kusudi wapate kujua tofauti inayokuwa kati ya kunitumikia mimi na kuwatumikia wafalme wa dunia.”
9
Basi, mufalme Sisaki wa Misri akashambulia muji Yerusalema, akaichukua hazina yote ya nyumba ya Yawe na ya nyumba ya kifalme, pamoja na ngao za zahabu ambazo mufalme Solomono alizozitengeneza.
10
Kwa pahali pa ngao hizo, mufalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba na kuziweka chini ya ulinzi wa walinzi wa mulango wa nyumba ya kifalme.
11
Kila wakati mufalme alipokwenda katika nyumba ya Yawe, walinzi waliingia walibeba ngao zile na kisha walizirudisha katika chumba cha ulinzi.
12
Alipojinyenyekeza, Yawe akaacha kumukasirikia na hakumwangamiza kabisa. Zaidi ya hayo, hali ya inchi ya Yuda ilikuwa nzuri.
13
Basi mufalme Rehoboamu akajiimarisha zaidi katika Yerusalema, na kutawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka makumi ine na mumoja alipoanza kutawala. Naye alitawala kwa muda wa miaka kumi na saba katika Yerusalema, muji ambao Yawe aliuchagua kati ya makabila yote ya Israeli kusudi aabudiwe ndani yake. Mama ya Rehoboamu aliitwa Nama, kutoka Amoni.
14
Rehoboamu alitenda maovu, kwa maana hakutayarisha moyo wake kwa kumutafuta Yawe.
15
Matendo ya mufalme Rehoboamu tangu mwanzo mpaka ya mwisho yameandikwa katika kitabu cha “Mambo ya Siku ya nabii Semaya”, na “Mambo ya Siku ya nabii Ido.” Wakati huu wote, kulikuwa vita ya mufululizo kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
16
Kisha Rehoboamu alikufa na kuzikwa katika muji wa Daudi, na Abiya mwana wake akatawala kwa pahali pake.
← Chapter 11
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 13 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36