bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 24
2 Chronicles 24
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 23
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 25 →
1
Yoasi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala. Alitawala kwa muda wa miaka makumi ine kule Yerusalema. Mama yake alikuwa Sibia kutoka Beri-Seba.
2
Wakati wote kuhani Yoyada alipokuwa muzima, Yoasi alitenda mema mbele ya Yawe.
3
Yoyada akamwoea wake wawili, nao wakamuzalia wana na wabinti.
4
Nyuma ya hayo Yoasi akaamua kujenga nyumba ya Yawe.
5
Basi, akawaita makuhani na Walawi na kuwaamuru: “Mwende katika miji ya Yuda, mukusanye feza kutoka kwa Waisraeli wote kwa kujenga upya nyumba ya Mungu wenu kila mwaka. Mufanye haraka.” Lakini Walawi hawakufanya haraka.
6
Basi mufalme akamwita kiongozi Yoyada, akamwuliza: “Mbona haujaamurisha Walawi kukusanya kutoka kwa watu wa Yuda na Yerusalema, kodi ambayo Musa mutumishi wa Yawe aliagiza watu walipe kwa ajili ya Hema Takatifu la Yawe?”
7
Kwa sababu wana wa Atalia, yule mwanamuke mwovu walivunja nyumba ya Mungu na kuingia ndani; vilevile vyombo vitakatifu vya nyumba ya Yawe walivitumia katika ibada za Mabali.
8
Basi mufalme akawaamuru, watengeneze sanduku la matoleo na kuliweka inje ya mulango wa nyumba ya Yawe.
9
Kisha tangazo likatolewa kote katika Yuda na Yerusalema, kwamba watu wote wamuletee Yawe kodi ambayo Musa mutumishi wa Mungu, aliwaamuru Waisraeli walipokuwa katika jangwa.
10
Wakubwa wote na watu wote wakafurahi wakaleta kodi yao wakaitumbukiza kwenye sanduku mpaka walipomaliza kufanya hivyo.
11
Walawi walipopeleka sanduku hilo kwa wakubwa wa mufalme, nao walipoona kwamba kuna kiasi kikubwa cha feza ndani, katibu wa mufalme pamoja na musimamizi wa Kuhani Mukubwa, wakazitoa ndani ya sanduku, kisha wakalirudisha kwa nafasi yake. Waliendelea kufanya vile kila siku, wakakusanya feza nyingi.
12
Mufalme na Yoyada walitoa feza zile na kuwapa wale waliosimamia kazi ya kujenga upya nyumba ya Yawe. Nao wakalipa wajengaji, waseremala kwa kutengeneza nyumba ya Yawe. Wakalipa vilevile wafuaji wa chuma na shaba kwa kujenga upya nyumba ya Yawe.
13
Hivyo wafundi hao walishugulika na kazi hiyo kwa bidii, wakairudisha nyumba ya Yawe katika hali yake ya zamani, na kuiimarisha.
14
Walipomaliza kutengeneza nyumba ya Yawe, wakamuletea mufalme na Yoyada zahabu na feza iliyobaki; halafu vyombo kwa ajili ya nyumba ya Yawe vilitengenezwa kwa feza hizo, vyombo hivyo vilikuwa vya kutumika katika kazi ya nyumba ya Yawe, matoleo ya sadaka za kuteketeza kwa moto na mabakuli ya kufukizia ubani, vilevile vyombo vya zahabu na vya feza. Watu waliendelea kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto katika nyumba ya Yawe wakati wote wa Yoyada.
15
Lakini Yoyada akazeeka na alipofikisha umri wa miaka mia moja na makumi tatu, akakufa.
16
Wakamuzika katika muji wa Daudi, kwenye makaburi ya wafalme kwa kuonyesha heshima yao kwake kwa sababu alifanya mema katika Israeli na mbele ya Mungu na nyumba yake.
17
Nyuma ya kifo cha Yoyada, wakubwa wa Yuda wakamwendea mufalme Yoasi wakainama uso mpaka chini mbele yake, wakamushawishi, naye akakubaliana nao.
18
Basi, watu wakaacha kuabudu katika nyumba ya Yawe, Mungu wa babu zao, wakaanza kuabudu Maashera na sanamu. Kasirani ya Mungu ikawaka juu ya Yuda na Yerusalema kwa sababu ya kosa lile.
19
Hata hivyo, akawatumia manabii kwa kuwaonya kusudi wamurudilie Yawe, lakini wao hawakuwasikiliza.
20
Halafu Roho wa Mungu akamujaza Zakaria mwana wa kuhani Yoyada, naye akasimama mbele ya watu kwa pahali palipokuwa juu kidogo, akawaambia: “Yawe anauliza: Kwa nini mumevunja sheria zake? Sasa hamuwezi kufanikiwa! Kwa vile mumemwacha, naye vilevile amewaacha!”
21
Lakini wakamufanyia shauri baya; na kwa amri ya mufalme, wakamupiga mawe kwenye kiwanja cha nyumba ya Yawe.
22
Mufalme Yoasi akasahau mema yote aliyotendewa na Yoyada, baba ya Zakaria, akamwua mwana wake. Alipokuwa karibu kufa, alisema: “Yawe uangalie mambo haya na kuyalipiza.”
23
Kwa mwisho wa mwaka, jeshi la Wasuria lilishambulia Yerusalema na Yuda. Wakawaua wakubwa wote, wakanyanganya vitu vingi na kuvituma kwa mufalme wa Damasiki.
24
Ingawa jeshi la Suria lilikuwa dogo, Yawe alilipatia ushindi mbele ya jeshi kubwa la watu wa Yuda kwa sababu hao watu wa Yuda walikuwa wamemwacha Yawe, Mungu wa babu zao. Hivi, Wasuria wakatimiza azabu ya Mungu juu ya mufalme Yoasi.
25
Waadui walipoondoka, wakamwacha akiwa ameumizwa vibaya sana, wakubwa wake wakamufanyia shauri baya, wakamwua juu ya kitanda chake, kwa kulipiza kisasi cha mauaji ya mwana wa kuhani Yoyada. Alizikwa katika muji wa Daudi, lakini si kwenye makaburi ya wafalme.
26
Watu waliomufanyia shauri baya walikuwa ni Zabadi mwana wa mwanamuke Mwamoni jina lake Simeati, na Yozabadi mwana wa mwanamuke Mumoabu jina lake Simuriti.
27
Habari za wana wake, za kujenga upya nyumba ya Yawe, na unabii wote juu yake, zimeandikwa katika maelezo ya kitabu cha Wafalme. Amazia mwana wake akatawala pahali pake.
← Chapter 23
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 25 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36