bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 10
2 Chronicles 10
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 9
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 11 →
1
Basi, Rehoboamu akaenda Sekemu, ambako Waisraeli wote walikuwa wamekusanyika kwa kumuweka kuwa mufalme.
2
Naye Yeroboamu mwana wa Nebati alipopata habari juu ya tendo hilo, wakati ule alikuwa angali anaishi Misri alikokwenda alipomukimbia Solomono, alirudi kutoka Misri.
3
Lakini Waisraeli walituma ujumbe na kumwita. Kisha, yeye pamoja na Waisraeli wote walimwendea Rehoboamu na kumwambia:
4
“Baba yako alitubebesha muzigo muzito. Basi, utupunguzie muzigo ule, nasi tutakutumikia.”
5
Rehoboamu akawajibu: “Mwende murudie kwangu nyuma ya siku tatu.” Basi wakaondoka.
6
Nyuma, Rehoboamu akataka kujua maoni ya wazee ambao walikuwa washauri wa baba yake Solomono alipokuwa angali muzima, akawauliza: “Munanishauria kwamba niwape jibu gani watu hawa?”
7
Wazee wale wakamujibu: “Ukiwahurumia watu hawa, ukiwafurahisha na kusema nao maneno mazuri, pale watakuwa watumishi wako siku zote.”
8
Lakini Rehoboamu alizarau shauri la wazee na kwa pahali pake akashauriana na vijana waliokomaa pamoja naye ambao walikuwa washauri wake.
9
Basi, akawauliza: “Ninyi munatoa shauri gani kusudi tuweze kuwajibu watu hawa walioniambia: ‘Punguza muzigo ambao baba yako alitubebesha?’ ”
10
Wale vijana wakamujibu: “Watu waliokuambia ‘Baba yako alitubebesha muzigo muzito, lakini wewe utupunguzie’, wewe uwaambie hivi: ‘Kidole changu kidogo cha mwisho ni kinene zaidi kuliko kiuno cha baba yangu.
11
Muzigo wa baba yangu ulikuwa muzito, lakini wangu utakuwa muzito zaidi. Baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa mijeledi yenye miiba.’ ”
12
Basi katika siku ya tatu Yeroboamu pamoja na watu wote wakarudi kwa Rehoboamu kama vile alivyokuwa amewaagiza.
13
Naye mufalme Rehoboamu akawajibu kwa ukali, akazarau shauri la wazee,
14
na kufuata shauri la vijana wenzake. Basi akasema: “Baba yangu aliwabebesha muzigo muzito, lakini mimi nitaufanya kuwa muzito zaidi. Baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa mijeledi yenye miiba”
15
Halafu mufalme hakuwajali watu kwa sababu jambo hili lilisababishwa na Mungu kusudi Yawe atimize neno lake alilomwambia Yeroboamu, mwana wa Nebati kwa njia ya Ahiya wa Shilo.
16
Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mufalme hakuwajali walimwambia: “Hatuna ushirika na Daudi! Hatuna urizi kutoka kwa mwana wa Yese. Kila mumoja arudie kwake, enyi watu wa Israeli! Utunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi!” Hivyo Waisraeli wote wakarudi kila mutu kwake.
17
Lakini Rehoboamu alitawala watu wa Israeli waliokaa katika miji ya Yuda.
18
Kisha mufalme Rehoboamu akamutuma Hadoramu aliyekuwa musimamizi wa kazi za kulazimishwa, nao watu wa Israeli walimupiga mawe, wakamwua. Halafu Rehoboamu akapanda ndani ya gari lake haraka akakimbilia Yerusalema.
19
Hivyo, watu wa Israeli wakakuwa katika hali ya uasi juu ya utawala wa ukoo wa Daudi mpaka leo.
← Chapter 9
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 11 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36