bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 22
2 Chronicles 22
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 21
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 23 →
1
Wakaaji wa Yerusalema wakamupa Ahazia mwana mudogo wa Yoramu ufalme, atawale pahali pa baba yake kwa sababu wakubwa wake wote waliuawa na kikundi fulani kilichokuja katika kambi pamoja na Waarabu. Hivyo, Ahazia mwana wa Yoramu, mufalme wa Yuda, akatawala.
2
Ahazia, alianza kutawala akiwa mwenye umri wa miaka makumi ine na miwili, akatawala kutoka Yerusalema kwa muda wa mwaka mumoja. Mama yake aliitwa Atalia, mujukuu wa Omuri.
3
Kwa sababu mama yake alikuwa mushauri wake katika kutenda maovu, naye vilevile alifuata mienendo ya jamaa ya Ahabu.
4
Alitenda maovu mbele ya Yawe kama vile jamaa ya Ahabu ilivyofanya maana hao ndio waliokuwa washauri wake nyuma ya kifo cha baba yake, mpaka kwa kuangamia kwake.
5
Hata akafuata shauri lao, akaenda pamoja na mufalme Yoramu mwana wa Ahabu mufalme wa Israeli kupigana vita na Hazaeli mufalme wa Suria kule Ramoti-Gileadi. Nao Wasuria wakamwumiza Yoramu.
6
Kisha akarudi Yezereheli kusudi apate kutunzwa vidonda alivyopata kule Rama, wakati alipopigana na Hazaeli mufalme wa Suria. Naye Ahazia mwana wa Yoramu mufalme wa Yuda akamutembelea Yoramu mwana wa Ahabu kule Yezereheli kwa sababu alikuwa mugonjwa.
7
Lakini ilikuwa imepangwa na Mungu kwamba maangamizi yatendeke kwa Ahazia kwa njia hiyo ya kumutembelea Yoramu; kwa sababu alipofika kule, alitoka pamoja na Yoramu kwenda kupigana na Yehu mwana wa Nimusi ambaye Yawe alimuchagua kwa kuangamiza uzao wa Ahabu.
8
Wakati Yehu alipokuwa akiwahukumu watu wa jamaa ya Ahabu alikutana na wakubwa wa Yuda pamoja na wana wa wandugu za Ahazia, waliomutumikia Ahazia, akawaua.
9
Akamutafuta Ahazia, naye akakamatwa akiwa amejificha kule Samaria. Wakamuleta mpaka kwa Yehu, akauawa. Wakauzika mwili wake maana walisema: “Yeye ni mujukuu wa Yosafati, ambaye alimutafuta Yawe kwa moyo wake wote.” Hapakubaki hata mutu mumoja wa jamaa ya Ahazia ambaye angeweza kushika ufalme.
10
Lakini wakati Atalia mama ya Ahazia alipoona kwamba mwana wake ameuawa, alitoka akaangamiza jamii yote ya kifalme ya Yuda.
11
Lakini Yoseba, binti ya mufalme Yoramu alimutwaa Yoasi, akamuchukua kwa siri kutoka kati ya wana wa mufalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamuficha yeye pamoja na yaya wake, katika chumba cha kulala. Hivyo Yoseba, binti ya mufalme Yoramu, muke wa kuhani Yoyada, kwa sababu alikuwa dada ya Ahazia, akamuficha Yoasi kusudi Atalia asimwone na kumwua.
12
Naye akakaa nao kwa muda wa miaka sita akiwa amefichwa ndani ya nyumba ya Mungu wakati Atalia alipokuwa akitawala inchi.
← Chapter 21
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 23 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36