bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 34
2 Chronicles 34
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 33
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 35 →
1
Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala, alitawala miaka makumi tatu na mumoja akiwa kule Yerusalema.
2
Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe. Alifuata njia za Daudi babu yake, na kushika amri za Yawe kwa uangalifu.
3
Katika mwaka wa ine wa utawala wake, mufalme Yosia, akiwa bado kijana, alianza kumwabudu Mungu wa Daudi, babu yake. Kisha alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili alianza kusafisha inchi ya Yuda na Yerusalema kwa kuharibu pahali pa kutambikia miungu mingine, sanamu za Ashera, na sanamu zingine za kuchonga na za kuyeyusha.
4
Watu wake walibomoa mazabahu za ibada za Mabali mbele yake na alikatakata mazabahu za kufukizia ubani zilizoinuliwa juu ya mazabahu hizo; vilevile alipondaponda sanamu za Ashera na zingine za kuchonga na za kuyeyusha; akazifanya kuwa mavumbi, nayo mavumbi akayamwanga juu ya makaburi ya wale ambao walizitolea sadaka.
5
Akateketeza mifupa ya makuhani wa miungu hiyo kwenye mazabahu zao, hivyo akasafisha inchi ya Yuda na Yerusalema.
6
Alifanya vile vile katika miji ya Manase, ya Efuraimu, ya Simeoni mpaka ya Nafutali na kwenye mabomoko yaliyokuwa kandokando ya miji hiyo.
7
Alibomoa mazabahu na kupondaponda Maashera na sanamu za kuchongwa zikakuwa mavumbi. Vilevile akazikatakata mazabahu za kufukizia ubani katika inchi yote ya Israeli. Kisha akarudi Yerusalema.
8
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, wakati ambapo alikuwa amekwisha kuisafisha inchi na nyumba, alituma watu watatu: Safani mwana wa Azalia, Masea liwali wa muji na Yoa mwana wa Yoahazi, mwandishi kusudi waende kutengeneza nyumba ya Yawe, Mungu wake.
9
Wakamwendea Hilkia, Kuhani Mukubwa, wakamupa feza zilizokuwa zimeletwa katika nyumba ya Mungu ambazo zilikusanywa na Walawi walinzi wa mulango, kutoka kwa watu wa Manase, Efuraimu na kutoka pande zingine zote za Israeli, inchi ya Yuda yote na ya Benjamina, na vilevile kutoka kwa wenyeji wa Yerusalema.
10
Zikawekwa katika mikono ya wale wafundi waliosimamia kazi ya kutengeneza nyumba ya Yawe; na wafundi waliofanya kazi katika nyumba ya Yawe wakazitoa kwa kutengeneza na kufanya upya nyumba.
11
Wakawapatia waseremala na wajengaji kwa ajili ya kununua mawe yaliyochongwa, mbao za kuunganishia na nguzo za kutumia kwa kutengeneza yale majengo ambayo wafalme wa inchi ya Yuda waliyobomoa.
12
Watu wale walifanya kazi hiyo kwa uaminifu, wakiwa chini ya uongozi wa Walawi Yahati na Obadia, wa ukoo wa Merari na Zakaria na Mesulamu wa ukoo wa Kohati. Walawi wote waliokuwa na ujuzi sana wa kupiga vyombo vya muziki,
13
waliwasimamia wabebaji wa mizigo na kuwaongoza wote waliofanya kazi mbalimbali, na kati ya Walawi kulikuwa waandishi, wakubwa na hata walinzi wa mulango.
14
Wakati walipokuwa wakitoa inje feza zilizokuwa zimeletwa katika nyumba ya Yawe, kuhani Hilkia akapata kitabu cha Sheria ya Yawe iliyotolewa kwa mukono wa Musa.
15
Kisha Hilkia akamwambia Safani mwandishi: “Nimepata kitabu cha Sheria katika nyumba ya Yawe.” Halafu Hilkia akamupatia Safani kitabu kile.
16
Naye Safani akamupelekea mufalme kitabu kile na kumupasha habari, akisema: “Yote watumishi wako waliyopewa wanayafanya.
17
Wamekusanya feza zilizopatikana katika nyumba ya Yawe, halafu wakazitoa kwa wasimamizi na kwa wafundi.”
18
Kisha mwandishi Safani akamwambia mufalme: “Kuhani Hilkia amenipa kitabu.” Naye Safani akakisoma mbele ya mufalme.
19
Mufalme aliposikia maneno ya Sheria akapasua nguo yake.
20
Halafu mufalme akaamuru Hilkia, Ahikamu mwana wa Safani, Abidoni mwana wa Mika, mwandishi Safani na Asaya, mutumishi wa mufalme, akisema:
21
“Mwende mutafute shauri kutoka kwa Yawe kwa ajili yangu na kwa ajili ya watu ambao wamebaki katika Israeli na Yuda, juu ya maneno yanayokuwa katika kitabu kilichopatikana. Kwa sababu kasirani ya Yawe imetuangukia maana babu zetu hawakushika Neno la Yawe wala kufanya yaliyoandikwa humo.”
22
Kwa hiyo Hilkia pamoja na wale wengine mufalme aliowatuma wakamwendea nabii Hulda muke wa Salumu, mwana wa Tokati, mujukuu wa Hasira, mulinzi wa nguo zilizotumika katika hekalu; (alikuwa anaishi katika Yerusalema katika mukoa wa pili); nao walizungumuza naye juu ya yaliyotokea.
23
Basi akawaambia: “Hivi ndivyo Yawe, Mungu wa Israeli anavyosema: mumwambie yule aliyewatuma kwangu,
24
Yawe anasema hivi: ‘Angalia nitaleta uovu juu ya Yerusalema na juu ya wakaaji wake, laana zote zilizoandikwa katika kitabu kilichosomwa mbele ya mufalme wa Yuda.
25
Kwa sababu wameniacha mimi na kufukizia miungu mingine ubani kusudi wanikasirikishe sana kwa kazi zote za mikono yao, basi kasirani yangu itamwagika juu ya pahali hapa wala haitatulizwa.
26
Lakini juu ya mufalme wa Yuda, aliyewatuma kutafuta shauri la Yawe mumwambie kwamba, hivi ndivyo Yawe, Mungu wa Israeli, anavyosema juu ya maneno uliyoyasikia,
27
kwa sababu umetubu na kunyenyekea mbele yangu, hata umepasua nguo yako na kulia uliposikia maneno yangu juu ya pahali hapa, na juu ya wakaaji wake, na umejinyenyekeza mbele yangu, nami vilevile nimekusikia. –Ni ujumbe wa Yawe.–
28
Azabu ambayo nitailetea Yerusalema, sitaileta wakati ungali muzima. Utawala wako utakuwa wa amani.’ ” Basi wajumbe wakamupelekea mufalme Yosia habari hii.
29
Kisha mufalme Yosia akaita na kukusanya viongozi wote wa inchi ya Yuda na Yerusalema.
30
Naye mufalme akaenda katika nyumba ya Yawe pamoja na wanaume wote wa inchi ya Yuda, na wakaaji wa Yerusalema wakifuatana na makuhani, Walawi na watu wengine wote wakubwa kwa wadogo. Halafu akawasomea maneno ya kitabu cha agano kilichopatikana katika nyumba ya Yawe.
31
Kisha mufalme akasimama kwa pahali pake akafanya agano mbele ya Yawe, kumufuata Yawe, kushika amri, maamuzi na masharti yake kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kutenda maneno yote ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
32
Tena akawasukuma wote waliokuwa katika Yerusalema na inchi ya Benjamina kushika agano lile. Nao wakaaji wa Yerusalema walitenda kwa kufuata agano la Mungu, Mungu wa babu zao.
33
Kisha Yosia akaondoa sanamu zote za kuchukiza zilizokuwa katika eneo lote la watu wa Israeli, na kuwasukuma watu wote wa Israeli kumutumikia Yawe, Mungu wao. Katika maisha yake yote hawakumwacha Yawe, Mungu wa babu zao.
← Chapter 33
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 35 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36