bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 13
2 Chronicles 13
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 12
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 14 →
1
Abiya akaanza kutawala inchi ya Yuda katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa mufalme Yeroboamu.
2
Alitawala kwa muda wa miaka mitatu akiwa Yerusalema. Mama yake aliitwa Mikaya binti ya Urieli wa Gibea. Kukatokea vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
3
Abiya alijitayarisha kupigana vita akiwa na jeshi la waaskari hodari elfu mia ine, naye Yeroboamu akajitayarisha na jeshi lake la waaskari hodari elfu mia nane.
4
Mufalme Abiya akasimama juu ya mulima Zemaraimu, unaokuwa kati ya milima ya Efuraimu akamwambia Yeroboamu na Waisraeli: “Unisikilize, ewe Yeroboamu na Waisraeli wote!
5
Hamujui kwamba Yawe, Mungu wa Israeli, amemupa Daudi na wazao wake ufalme kwa milele kwa kufanya naye agano lisilovunjika?
6
Lakini Yeroboamu mwana wa Nebati mutumishi wa Solomono mwana wa Daudi alimwasi bwana wake.
7
Na watu wa ovyoovyo wakajiunga naye, watu wapumbafu wasiofaa kitu, nao wakamushawishi Rehoboamu mwana wa Solomono kutenda yale waliyotaka wao, naye hangeweza kuwazuia maana wakati ule alikuwa angali kijana bila mazoezi mengi.
8
“Sasa ninyi munazani munaweza kupinga ufalme wa Yawe ambao Daudi na wazao wake walipewa kwa sababu muko na jeshi kubwa na sanamu za zahabu za wana-ngombe, Yeroboamu alizowatengenezea kuwa miungu yenu!
9
Hamukuwafukuza makuhani wa Yawe, wana wa Haruni, vilevile na Walawi, na kujifanyia makuhani wenu wenyewe kama vile watu wa mataifa mengine wanavyofanya? Yeyote anayekuja kwenu kujitakasa na mwana-ngombe dume au kondoo dume anakuwa kuhani wa vitu ambavyo si miungu.
10
“Lakini kwa ngambo yetu, Yawe ni Mungu wetu, wala hatujamwacha. Tena tuko na makuhani wa uzao wa Haruni ambao wanamutumikia Yawe, nao wanasaidiwa na Walawi.
11
Kila siku asubui na magaribi, makuhani wanamutolea sadaka za kuteketezwa na kumufukizia ubani wenye harufu nzuri, tena wanapanga mikate inayotolewa na Mungu juu ya meza ya zahabu safi, na kutunza kinara cha zahabu na kuwasha taa kila siku magaribi. Sisi tunayafuata maagizo ya Yawe, Mungu wetu, lakini ninyi mumemwacha.
12
Na muangalie, Mungu mwenyewe ndiye kiongozi wetu na makuhani wake wako na baragumu zao tayari kuzipiga kwa kupana kitambulisho cha kuanza vita juu yenu. Enyi watu wa Israeli, muache kupigana vita na Yawe, Mungu wa babu zenu. Hamuwezi kushinda!”
13
Lakini wakati ule, Yeroboamu alikuwa amekwisha kutuma waaskari wake wamoja kushambulia jeshi la Yuda kutoka upande wa nyuma, wakati wale wengine wamewashambulia kutoka upande wa mbele.
14
Watu wa Yuda walipoangalia nyuma, walishituka kuona wamezungukwa; basi wakamulilia Yawe, nao makuhani wakapiga baragumu zao.
15
Halafu waaskari wa Yuda wakapiga kelele la vita, na walipofanya hivyo, Mungu akamushinda Yeroboamu na jeshi lake la Waisraeli mbele ya Abiya na watu wa Yuda.
16
Watu wa Israeli wakawakimbia Wayuda naye Mungu akawatia katika mikono yao.
17
Abiya na jeshi lake akawapiga Waisraeli sana, akawashinda; akaua waaskari wa Israeli, elfu mia tano waliokuwa kati ya waaskari hodari sana katika Israeli.
18
Kwa hiyo, watu wa Yuda walipata ushindi mbele ya Waisraeli kwa sababu walimutegemea Yawe, Mungu wa babu zao.
19
Abiya akamufukuza Yeroboamu, akamunyanganya miji yake: Beteli, Yesana, Efuroni pamoja na vijiji vilivyokuwa kandokando ya miji hiyo.
20
Yeroboamu hakuweza kupata nguvu tena wakati wa Abiya. Kwa mwisho Yawe akamupiga, naye akakufa.
21
Lakini Abiya aliendelea kupata nguvu zaidi. Akaoa wanawake kumi na wane, akazaa wana makumi mbili na wawili na wabinti kumi na sita.
22
Matendo mengine ya Abiya, njia zake na maneno yake, yameandikwa katika kitabu cha “Historia ya Nabii Ido.”
23
Kwa mwisho, Abiya alikufa na kuzikwa katika muji wa Daudi na mwana wake Asa akatawala kwa pahali pake. Wakati wa Asa, kulikuwa amani katika inchi kwa muda wa miaka kumi.
← Chapter 12
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 14 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36