bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 31
2 Chronicles 31
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 30
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 32 →
1
Nyuma ya sherehe kumalizika, watu wote wa Israeli wakakwenda katika kila muji wa Yuda, wakavunjavunja nguzo za mawe na kukatakata sanamu za Ashera, mungu wa kike, na vilevile wakaharibu mazabahu na pahali pa kuabudia miungu mingine. Wakafanya vile katika inchi yote ya Yuda, Benjamina, Efuraimu na Manase, mpaka walipokwisha kuvimaliza vyote. Kisha Waisraeli wakarudi kwao, kila mutu kwenye urizi wake.
2
Mufalme Hezekia akawapanga tena makuhani na Walawi katika makundi, akamupa kila mumoja wao kazi kufuatana na utumishi wake katika sehemu mbalimbali za hekalu la Yawe. Kazi ile ni pamoja na utoaji wa sadaka za kuteketeza kwa moto na za amani, za shukrani na za kusifu.
3
Kutoka mali yake mwenyewe, mufalme akatoa sehemu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa asubui na magaribi, za siku ya Sabato na wakati wa sherehe za mwandamo wa mwezi na zile sikukuu zingine zilizoamuriwa kulingana na Sheria ya Yawe.
4
Zaidi ya hayo, mufalme akawaambia wakaaji wa Yerusalema watoe sehemu makuhani na Walawi waliyostahili kupewa, kusudi wao wajitolee kikamilifu katika shuguli za sheria za Yawe.
5
Mara tu amri hii ilipotolewa, watu wa Israeli wakatoa kwa wingi, malimbuko ya ngano, divai, mafuta, asali na mazao mengine mbalimbali ya shamba, na vilevile sehemu moja ya kumi ya kila kitu.
6
Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda, wakaleta vilevile sehemu moja ya kumi ya ngombe na kondoo na ya vitu vitakatifu vilivyotolewa kwa Yawe. Wakaviweka vitu hivyo katika mafungu.
7
Katika mwezi wa tatu wakaanza kuvipanga katika mafungu, wakamaliza katika mwezi wa saba.
8
Mufalme Hezekia na wakubwa wake walipokuja kuangalia mafungu yale, wakamushukuru Yawe na watu wake wa Israeli.
9
Mufalme Hezekia akawauliza makuhani na Walawi juu ya mafungu hayo.
10
Azaria, Kuhani Mukubwa aliyekuwa wa uzao wa Sadoki akamujibu: “Tangu wakati watu walipoanza kuleta matoleo yao katika hekalu, tumekuwa na vyakula vya kutosha na hata tuna akiba kubwa. Yawe amewabariki watu wake, ndiyo maana tumepata vitu hivi vyote.”
11
Kisha mufalme Hezekia akawaamuru watengeneze gala katika nyumba ya Yawe. Wakatengeneza;
12
na mule ndani wakaweka matoleo, sehemu moja za kumi na vyote vilivyotakaswa kwa uaminifu. Wakamuweka Konania, Mulawi, kuwa musimamizi mukubwa muchungaji wa vitu hivyo, na ndugu yake, Simea kuwa musaidizi wake.
13
Nao Yehieli, Azazia, Nahati, Asaeli, Yeremoti, Yozabadi, Elieli. Isimakia, Mahati na Benaya, wakawekwa kuwa wasimamizi chini ya uongozi wa Konania na ndugu yake Simei. Hawa wote walichaguliwa na mufalme Hezekia, na Azaria, kuhani mukubwa wa nyumba ya Mungu.
14
Kore mwana wa Imuna, Mulawi, aliyekuwa mulinzi wa Mulango wa Mashariki wa hekalu, akasimamia matoleo yote ya mapenzi kwa Mungu; na kugawanya matoleo kwa ajili ya Yawe na sadaka zinazokuwa takatifu kabisa.
15
Nao Edeni, Miniamini, Yesua, Semaya, Amaria na Sekania, walimusaidia kufanya kazi hiyo kwa uaminifu katika ile miji mingine makuhani walimoishi. Waliwagawanyia wandugu zao Walawi vyakula, kwa wakubwa kama vile kwa wadogo.
16
Tena, bila kujali ukoo walimoandikishwa, waliwapa sehemu wale watoto wa kiume waliokuwa wametimiza umri wa miaka mitatu na zaidi, na ambao waliingia katika nyumba ya Yawe kila siku kwa kutimiza kazi zao. Kila mumoja wao alipata sehemu yake kulingana na kazi aliyofanya kwa zamu yake.
17
Makuhani waliandikishwa kulingana na jamaa zao, na Walawi waliotimiza miaka makumi mbili na zaidi waliandikishwa kulingana na kazi zao na zamu zao.
18
Waliandikishwa wote pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, wana wao na wabinti zao kwa sababu, kwa kujitoa kwa kazi zao, walihitajika kujiweka katika hali ya utakaso kila mara.
19
Vilevile, kati ya wazao wa Haruni, makuhani waliokuwa wanakaa katika mashamba waliyorizi kwa pamoja inje ya miji yao, kulikuwa watu waliochaguliwa kwenye miji hiyo ambao waliwagawanyia sehemu zao za vyakula. Waliwapa sehemu kila mwanaume katika jamaa za makuhani, na kila mumoja aliyekuwa ameandikishwa kati ya Walawi.
20
Hivi ndivyo mufalme Hezekia alivyotenda mambo mema, ya haki na ya uaminifu mbele ya Yawe, Mungu wake, katika inchi yote ya Yuda.
21
Kila kazi aliyoifanya katika utumishi wa nyumba ya Mungu au katika kutii sheria na amri za Mungu kwa kufuata uongozi kutoka kwake, alizifanya kwa moyo wake wote, naye akafanikiwa.
← Chapter 30
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 32 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36