bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 11
2 Chronicles 11
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 10
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 12 →
1
Rehoboamu alipofika Yerusalema, alikusanya waaskari wafundi wa vita elfu mia moja na makumi nane wa makabila ya Yuda na Benjamina, apate kupigana na utawala wa Israeli, kusudi aurudishe utawala kwake yeye mwenyewe Rehoboamu.
2
Lakini neno la Yawe lilimufikia Semaya, yule mutu wa Mungu, kusema hivi:
3
“Umwambie Rehoboamu mwana wa Solomono, mufalme wa Yuda na Waisraeli wote katika Yuda na Benjamina kwamba
4
Bwana anasema hivi: ‘Musiende wala musipigane na wandugu zenu. Murudie kila mutu kwake, maana yale yaliyotokea ni kwa kufuata mupango wangu.’ ” Basi wakatii ujumbe wa Yawe, wakarudia kila mutu kwake, wala hawakwenda kupigana na Yeroboamu.
5
Rehoboamu alikaa Yerusalema na akajenga kuta kwa kuimarisha miji hii iliyokuwa katika inchi ya Yuda:
6
Betelehemu, Etamu, Tekoa,
7
Beti-Suri, Soko, Adulamu,
8
Gati, Maresa, Zifu,
9
Adoraimu, Lakisi, Azeka,
10
Zora, Ayaloni na Hebroni. Miji hiyo yenye kuzungukwa kuta iko Yuda na Benjamina.
11
Aliziimarisha kuta zile na mule ndani akaweka majemadari na magala ya vyakula, mafuta na divai.
12
Ndani ya kila muji, aliweka ngao na mikuki, na kuifanya miji hiyo kuwa imara sana. Yuda na Benjamina zikakuwa chini ya mamlaka yake.
13
Makuhani na Walawi wote waliokuwa wanaishi kote katika inchi ya Israeli, wote wakavuka mupaka wao na kumwendea.
14
Walawi wakaacha mashamba yao ya malisho ya nyama, na maeneo yao mengine kwa sababu Yeroboamu na wana wake waliwakataza kumutumikia Yawe kama vile makuhani wa Yawe.
15
Yeroboamu akajichagulia makuhani wake mwenyewe wa kutumika kwenye nafasi za ibada za miungu na wa kuabudu mizimu na sanamu za wana-ngombe alizojitengenezea.
16
Watu wote ambao walikuwa wamekusudia kwa moyo kumwabudu Yawe, Mungu wa Israeli, kutoka katika makabila yote ya Israeli, waliandamana na Walawi mpaka Yerusalema kusudi wapate kumutolea sadaka Yawe, Mungu wa babu zao.
17
Hivyo, wakaimarisha ufalme wa Yuda, na kwa muda wa miaka mitatu, wakauunga mukono utawala wa Rehoboamu mwana wa Solomono, ukakuwa imara na wakaishi katika hali ileile waliyoishi wakati walipokuwa chini ya utawala wa mufalme Daudi na mufalme Solomono.
18
Rehoboamu alioa muke, jina lake Mahalati binti ya Yeremoti mwana wa Daudi. Mama yake aliitwa Abihaili binti ya Eliabu, mwana wa Yese.
19
Naye akamuzalia wana watatu: Yeusi, Semaria na Zahamu.
20
Kisha, akamwoa Maka binti ya Abusaloma, naye akamuzalia Abiya, Atai, Siza na Selomiti.
21
Rehoboamu alioa wake kumi na wanane na wahabara makumi sita, akazaa wana makumi mbili na wane na wabinti makumi sita. Kati ya wake zake wote na wahabara wake, alimupenda zaidi Maka binti ya Abusaloma.
22
Hivyo akamuchagua Abiya, mwana wa Maka, kuwa mukubwa kati ya wandugu zake, maana alikusudia kumufanya kuwa mufalme.
23
Rehoboamu alifanya jambo la hekima, akawatawanya wamoja kati ya wana wake katika inchi yote ya Yuda na Benjamina akiwaweka katika miji yote yenye kuzungukwa na kuta. Wakiwa mule, akawapa vyakula vingi na vilevile akawaoea wake wengi.
← Chapter 10
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 12 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36