bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 26
2 Chronicles 26
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 25
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 27 →
1
Kisha watu wote wa Yuda wakamukamata Uzia mwana wa Amazia akiwa mwenye umri wa miaka kumi na sita, wakamufanya kuwa mufalme pahali pa Amazia baba yake.
2
Halafu nyuma ya kifo cha baba yake akajenga upya muji wa Eloti na kuurudisha kwa inchi ya Yuda.
3
Uzia alianza kutawala akiwa na umri wa miaka kumi na sita; akatawala kwa muda wa miaka makumi tano na miwili kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalema.
4
Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kama vile baba yake alivyotenda.
5
Akamutumikia Yawe kwa uaminifu wakati wa kuishi kwa Zakaria, aliyemufundisha kumutii Mungu. Kwa jinsi alivyomutafuta Mungu, Mungu alimufanikisha.
6
Uzia akaondoka kwa kupigana vita na Wafilistini, akabomoa kuta za miji ya Gati, Yabune na Asidodi. Akajenga miji katika eneo la Asidodi na fasi ingine katika inchi ya Filistia.
7
Mungu akamusaidia kuwashinda Wafilistini, Waarabu waliokaa Guribali na Wameuni.
8
Waamoni walimulipa kodi, na sifa zake zikaenea mpaka Misri, kwa sababu alipata nguvu.
9
Tena Uzia akajenga minara ya kukinga muji kwenye milango tatu ya Yerusalema na kuiimarisha.
10
Hata katika jangwa vilevile alijenga minara, akachimba visima vingi, maana alikuwa na makundi mengi ya nyama kwenye sehemu za miinuko na mabonde. Alikuwa na walimaji na watunza mizabibu kwenye milima, na katika inchi yenye mboleo maana alipenda mulimo.
11
Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililokuwa tayari kwa vita. Lilikuwa limegawanywa katika vikundi mbalimbali, na jumla ya hesabu yao iliwekwa na katibu Yeieli, na Masea, mukubwa, nao wote walikuwa chini ya uongozi wa Hanania, mumoja wa majemadari wa mufalme.
12
Kwa jumla, viongozi wote wa majeshi walikuwa elfu mbili na mia sita.
13
Chini yao, kulikuwa jeshi la waaskari elfu mia tatu na saba na mia tano, wenye uwezo mukubwa wa kupigana na waadui wa mufalme.
14
Uzia aliwapa waaskari wale ngao, mikuki, kofia za chuma, nguo za chuma, pinde na mawe kwa ajili ya kupiga mujeledi.
15
Kule Yerusalema wafundi wake wakamutengenezea mitambo ya kurushia mishale na mawe makubwamakubwa. Sifa zake zikaenea kila pahali, nguvu zake zikaongezeka zaidi kwa sababu ya usaidizi mwingi alioupata kutoka kwa Mungu.
16
Lakini wakati mufalme Uzia alipokuwa na nguvu, moyo wake akajaa kiburi ambacho kilisababisha maangamizi yake. Akamwasi Yawe wake kwa kuingia ndani ya hekalu akikusudia kufukiza ubani juu ya mazabahu.
17
Lakini kuhani Azaria, pamoja na makuhani wengine mashujaa makumi nane, wakamufuata mufalme
18
na kumuzuia. Wakamwambia: “Si kazi yako hata kidogo Uzia, kumufukizia Yawe ubani. Ni makuhani tu wa uzao wa Haruni ambao wametakaswa kwa kufukiza ubani. Ondoka pahali hapa patakatifu. Umemukosea Yawe na hautapata heshima yoyote kutoka kwake.”
19
Wakati ule, Uzia alikuwa amesimama ndani ya hekalu karibu na mazabahu, akishika chetezo cha kufukizia ubani katika mukono. Akawakasirikia makuhani; na mara tu alipofanya hivyo, akashikwa na ukoma katika paji la uso wake mbele ya makuhani hao.
20
Azaria, Kuhani Mukubwa, na wale makuhani wengine, wakamwangalia, kisha wakaharakisha kumutoa inje; hata yeye mwenyewe akafanya haraka kutoka, kwa maana Yawe alikuwa amemwazibu.
21
Basi mufalme Uzia akakuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Alikaa katika nyumba yake ya pekee maana hakukubaliwa tena kuingia katika nyumba ya Yawe. Na Yotamu mutoto wake, akatunza jamaa yake akitawala wakaaji wa inchi.
22
Matendo mengine yote ya mufalme Uzia kutoka mwanzo mpaka mwisho, yaliandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi.
23
Uzia akakufa na kuzikwa katika eneo la kuzikia wafalme, kwa sababu walisema: “Yeye ana ukoma”. Naye Yotamu mwana wake, akatawala pahali pake.
← Chapter 25
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 27 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36