bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 21
2 Chronicles 21
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 20
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 22 →
1
Yosafati akakufa na kuzikwa pamoja na babu zake katika makaburi ya kifalme katika muji wa Daudi; naye Yoramu mwana wake akatawala pahali pake.
2
Yoramu alikuwa na wandugu, wana wa Yosafati; Azaria, Yehieli, Zakaria, Azaria, Mikaeli na Sefatia.
3
Baba yao aliwapa zawadi kubwakubwa za feza, zahabu na vitu vingine vya bei kali, na vilevile miji ya Yuda yenye kuta. Lakini kwa sababu Yoramu ndiye aliyekuwa muzaliwa wake wa kwanza, Yosafati akamupa ufalme atawale kwa pahali pake.
4
Yoramu alipoikalia kiti cha kifalme na utawala wake ulipokuwa umekwisha kuimarika, yeye akawaua wandugu zake wote kwa upanga, na vilevile wakubwa wamoja wa Israeli.
5
Yoramu alianza kutawala akiwa na umri wa miaka makumi tatu na miwili. Alitawala akiwa kule Yerusalema kwa muda wa miaka minane.
6
Alifuata njia mbaya za mufalme Ahabu na za wafalme wengine wa Israeli kama vile jamaa ya Ahabu ilivyofanya kwa sababu muke wake alikuwa binti ya Ahabu. Akatenda maovu mbele za Yawe,
7
lakini Yawe hakutaka kuangamiza ukoo wa Daudi kwa ajili ya agano alilokuwa amefanya na Daudi vilevile kwa sababu alikuwa ameahidi kwamba wazao wake wataendelea kutawala milele.
8
Wakati wa utawala wa Yoramu, Waedomu waliasi utawala wa Yuda, wakaweka mufalme wao wenyewe.
9
Kwa hiyo, Yoramu pamoja na wakubwa wake na magari yake yote akaondoka akawashambulia Waedomu waliokuwa wamemuzunguka yeye pamoja na wakubwa wake na magari.
10
Hivyo Waedomu wakaasi utawala wa Yuda mpaka sasa. Wakati uleule, vilevile wakaaji wa Libuna nao wakaasi utawala wake kwa sababu Yoramu alikuwa amemwacha Yawe, Mungu wa babu zake.
11
Tena alitengeneza pahali pa kuabudia miungu mingine katika milima ya Yuda na kusababisha wakaaji wa Yerusalema kukosa uaminifu na watu wa Yuda kupotoka.
12
Nabii Elia akamupelekea mufalme Yoramu barua hii: “Yawe, Mungu wa Daudi babu yako, anakulaani kwa sababu haukufuata mwenendo wa Yosafati baba yako, au wa Asa mufalme wa Yuda.
13
Lakini umeifuata mienendo ya wafalme wa Israeli na kuwaongoza watu wa Yuda na wa Yerusalema katika kukosa uaminifu kama vile Ahabu, na wafalme wa jamaa yake waliomufuata walivyoongoza Israeli kukosa uaminifu. Vilevile umewaua wandugu zako, wandugu za baba mumoja waliokuwa watu wema zaidi kuliko wewe.
14
Kwa sababu hiyo, Yawe atawaazibu vikali watu wako, wana wako, wake zako na kuharibu mali yako yote.
15
Wewe mwenyewe utapata ugonjwa mukali wa tumbo, ambao utaongezeka siku kwa siku, mpaka matumbotumbo yako yatoke inje.”
16
Kulikuwa Wafilistini na Waarabu wengine waliokuwa wakikaa karibu na Waetiopia. Hawa, Yawe aliwapandisha hasira kusudi wapigane vita na Yoramu.
17
Basi, wakashambulia inchi ya Yuda, wakanyanganya mali yote iliyokuwa katika nyumba yake na kutwaa wana wake wote na wake zake, isipokuwa Ahazia, mwana wake mudogo.
18
Nyuma ya hayo yote, Yawe akamuletea mufalme ugonjwa wa tumbo usioweza kupona.
19
Aliendelea kugonjwa, na ugonjwa wake ukakuwa unaongezeka siku kwa siku, hata kufikia mwisho wa mwaka wa pili, akakufa katika maumivu makali. Watu hawakuwasha moto kwa kuomboleza kifo chake kama vile walivyowafanyia babu zake.
20
Yoramu alianza kutawala akiwa na umri wa miaka makumi tatu na miwili; akatawala kule Yerusalema kwa muda wa miaka minane. Wakati alipokufa, hakuna mutu yeyote aliyemusikitikia. Alizikwa katika muji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
← Chapter 20
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 22 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36