bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 25
2 Chronicles 25
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 24
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 26 →
1
Amazia alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitano alipoanza kutawala, akatawala kwa muda wa miaka makumi mbili na mitano katika Yerusalema. Mama yake aliitwa Yoadani wa Yerusalema.
2
Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe ingawa hakutenda kwa moyo mukamilifu.
3
Mara tu Amazia alipojiimarisha katika mamlaka akawaua watumishi waliomwua mufalme baba yake.
4
Lakini hakuwaua watoto wao, kama vile ilivyoandikwa katika sheria zinazokuwa katika kitabu cha Musa, ambamo Yawe anatoa amri akisema: “Wazazi hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya wazazi wao; lakini kila mutu atauawa kwa ajili ya zambi zake mwenyewe.”
5
Mufalme Amazia akawakusanya wanaume wa Yuda, akawapanga katika vikundi mbalimbali kulingana na ukoo zao, akawaweka chini ya majemadari wa maelfu na wa mamia kwa ajili ya Yuda na Benjamina. Alipowakagua wale wenye miaka makumi mbili na zaidi, akapata watu elfu mia tatu kwa jumla. Wote walikuwa watu waliochaguliwa wanaofaa kwa vita, wanaoweza kutumia mikuki na ngao.
6
Tena, alilipa waaskari wengine mashujaa elfu moja kutoka Israeli, kwa bei ya kilo elfu tatu za feza.
7
Lakini mutu wa Mungu akamwendea na kumwambia: “Ee mufalme, usiende kwenye vita pamoja na hawa waaskari wa Israeli, maana Yawe hayuko pamoja na watu wa Israeli. Hayuko pamoja na hawa Waefuraimu wote.
8
Lakini ukitaka kwenda, basi ufanye vile, ukuwe hodari katika vita, lakini Mungu atakufanya ushindwe na waadui, kwa maana Mungu ana nguvu kwa kusaidia au kumufanya mutu ashindwe.”
9
Amazia akamwuliza yule mutu wa Mungu: “Tutafanya nini na feza yote ambayo nimekwisha wapa waaskari wa Israeli?” Naye akamujibu: “Yawe anaweza kukupa zaidi ya hiyo.”
10
Kwa hiyo Amazia akawaacha waaskari waliotoka Efuraimu warudi kwao. Basi wakarudi kwao wakiwa wamewakasirikia sana watu wa Yuda.
11
Amazia akajipa moyo akaongoza jeshi lake mpaka kwenye Bonde la Chumvi. Hapo akapigana na kuwaua watu elfu kumi wa Seiri.
12
Na wengine watu elfu kumi, wakakamatwa na kuwapandisha juu ya jiwe kubwa na kuwatupa chini toka juu ya jiwe, wakavunjika vipandevipande.
13
Wakati uleule, wale waaskari Waisraeli ambao Amazia aliwaacha warudi kwao akiwakataza wasijiunge naye katika vita, wakakwenda na kuishambulia miji ya Yuda, toka Samaria mpaka Beti-Horoni, wakaua watu elfu tatu na kunyanganya vitu vingi.
14
Amazia aliporudi kisha kuwashinda Waedomu, akaleta miungu ya Waedomu akaifanya kuwa miungu yake, akainama uso mpaka chini mbele yao na kuifukizia ubani.
15
Hayo yakamukasirisha sana Yawe, akatuma nabii kwa Amazia. Nabii huyo akamwuliza Amazia: “Kwa nini unategemea miungu ya watu wengine ambayo hata haikuweza kuwaokoa watu wake wenyewe kutoka katika mikono yako?”
16
Na alipokuwa angali akisema naye, Amazia akamwambia: “Nyamaza! Tulikufanya wewe kuwa mushauri wa mufalme? Kwa nini uawe?” Nabii akanyamaza, lakini akasema: “Ninafahamu kwamba Mungu ameamua kukuangamiza kwa maana umetenda haya yote, kisha unazarau shauri langu.”
17
Basi Amazia mufalme wa Yuda alifanya shauri, akatuma ujumbe kwa Yoasi, mwana wa Yoahazi, mwana wa Yehu mufalme wa Israeli, akamwambia: “Kuja tuonane uso kwa uso.”
18
Lakini Yoasi mufalme wa Israeli akamupelekea Amazia ujumbe akisema: “Siku moja, muti wa mubaruti wa Lebanoni ukauambia mwerezi nao ni wa kule hivi: ‘Umwoeshe binti yako kwa mwana wangu!’ Lakini nyama mumoja wa pori akapita pale na kukanyagakanyaga mubaruti ule.
19
Sasa wewe Amazia unasema: ‘Nimewaua Waedomu’ na moyo unakufanya ujivune. Basi, ikaa ndani ya nyumba yako; kwa nini kujitafutia taabu zitakazokuangamiza wewe mwenyewe pamoja na watu wako wa Yuda?”
20
Lakini Amazia hakujali kwa maana lilikuwa kusudi la Mungu apate kuwekwa katika mukono wa waadui zao kwa sababu alitegemea miungu ya Edomu.
21
Kwa hiyo, Yoasi, mufalme wa Israeli akatoka akapambana uso kwa uso na Amazia, mufalme wa Yuda katika vita kule Beti-Semesi, katika inchi ya Yuda.
22
Watu wa Yuda wakashindwa na watu wa Israeli na kila mumoja akarudia kwake.
23
Halafu Yoasi mufalme wa Israeli alimukamata Amazia mufalme wa Yuda, mwana wa Yoasi, mwana wa Ahazia kule Beti-Semesi akamupeleka mpaka Yerusalema. Kule, akabomoa ukuta wa muji ule, kuanzia kwenye mulango wa Efuraimu mpaka kwenye mulango wa Pembeni, umbali wa karibu metre mia mbili.
24
Akatwaa zahabu yote na feza hata na vifaa vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Yawe chini ya ulinzi wa Obedi-Edomu; vilevile akatwaa hazina ya nyumba ya kifalme mateka, kisha akarudi Samaria.
25
Amazia mufalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano nyuma ya kifo cha mufalme Yoasi mwana wa Yoahazi mufalme wa Israeli.
26
Matendo mengine yote ya Amazia kutoka mwanzo mpaka mwisho yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda na Israeli.
27
Mashauri mabaya ya kumwua Amazia yalifanywa Yerusalema tangu alipomwacha Yawe, kwa hiyo akakimbilia Lakisi. Lakini waadui wakatuma watu Lakisi wakamwua kule.
28
Maiti yake ikaletwa juu ya farasi, na kuzikwa kwenye makaburi ya kifalme katika muji wa Daudi.
← Chapter 24
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 26 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36