bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 36
2 Chronicles 36
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 35
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
1
Watu wa inchi ya Yuda wakatwaa Yoahazi, mwana wa Yosia, wakamuweka kuwa mufalme pahali pa baba yake.
2
Yoahazi alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitatu alipoanza kutawala; akatawala kwa muda wa miezi mitatu akiwa kule Yerusalema.
3
Kisha mufalme wa Misri akamwondoa kule Yerusalema na kulipisha inchi kodi ya kilo elfu tatu na mia ine za feza na kilo makumi tatu na ine za zahabu.
4
Kisha mufalme wa Misri akamweka Eliakimu, ndugu ya Yoahazi kuwa mufalme wa Yuda na Yerusalema, na akabadilisha jina lake kuwa Yoyakimu; lakini Neko akamupeleka ndugu yake Yoahazi mpaka Misri.
5
Yoyakimu alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mitano alipoanza kutawala, akatawala kwa muda wa miaka kumi na mumoja akiwa kule Yerusalema. Alitenda maovu mbele ya Yawe, Mungu wake.
6
Kisha Nebukadneza mufalme wa Babeli, akamushambulia, akamufunga kwa minyororo kwa kumupeleka Babeli.
7
Nebukadneza akatwaa vilevile vyombo vimoja vya nyumba ya Yawe akavipeleka Babeli na kuviweka katika nyumba ya kifalme kule Babeli.
8
Basi matendo mengine ya Yoyakimu, pamoja na machukizo aliyotenda na mambo mengine yaliyoonekana juu yake yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli na Yuda; naye Yoyakini mwana wake akatawala pahali pake.
9
Yoyakini alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala, alitawala kule Yerusalema kwa muda wa miezi mitatu na siku kumi. Alitenda maovu mbele ya Yawe.
10
Mwaka ulipokwisha, mufalme Nebukadneza alituma wajumbe, wakamuchukua Yoyakini na kumupeleka mpaka Babeli, pamoja na vyombo vya bei kali vya nyumba ya Yawe. Akamweka ndugu yake Sedekia kuwa mufalme wa Yuda na Yerusalema.
11
Sedekia alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mumoja alipoanza kutawala, akatawala kule Yerusalema kwa muda wa miaka kumi na mumoja.
12
Alitenda maovu mbele ya Yawe, Mungu wake, wala hakunyenyekea mbele ya nabii Yeremia ambaye alisema maneno yaliyotoka kwa Yawe.
13
Sedekia alimwasi vilevile mufalme Nebukadneza aliyekuwa amemufanya aape kwa jina la Mungu kwamba hatamwasi. Alikuwa mupotovu sana na kufanya moyo mugumu, akakataa kumugeukia Yawe, Mungu wa Israeli.
14
Hata makuhani, viongozi wa inchi ya Yuda pamoja na watu walikosa uaminifu kabisa wakiiga matendo yote ya kuchukiza ya watu wa mataifa mengine; waliichafua nyumba ya Yawe ambayo yeye mwenyewe alikuwa ameitakasa kule Yerusalema.
15
Yawe, Mungu wa babu zao, mara kwa mara alituma kwao wajumbe wake maana alikuwa na huruma kwa watu wake na makao yake.
16
Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.
17
Kwa hiyo, Yawe alimuleta mufalme wa Wakaldea ambaye aliwaangamiza vijana wao kwa upanga hata ndani ya Pahali Patakatifu; wala hakumuhurumia mutu yeyote akuwe kijana au binti, muzee au muzaifu. Wote Yawe aliwatia katika mikono yake.
18
Alitwaa vyombo vyote vya nyumba ya Mungu vikubwa na vidogo na hazina ya nyumba ya Yawe na ya mufalme na wakubwa wake. Alivipeleka vyote mpaka Babeli.
19
Aliichoma moto nyumba ya Mungu, akaubomoa ukuta wa Yerusalema, akazichoma moto nyumba zote za kifalme na kuharibu vyombo vyake vyote vya bei kali.
20
Watu waliookolewa kwenye vita aliwapeleka katika uhamisho Babeli. Kule wakakuwa watumwa wake na wa wazao wake mpaka ufalme wa Persia ulipoinuka kwa nguvu.
21
Na hivyo likatimia neno la Yawe alilosema kwa njia ya nabii Yeremia: “Mpaka inchi imetimiza Sabato zake, haitalimwa siku zote itakapokuwa ukiwa mpaka miaka makumi saba itakapotimia.”
22
Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Kiro mufalme wa Persia, kusudi litimie neno la Yawe alilolisema kwa njia ya nabii Yeremia, Yawe aliamusha nia ya Kiro naye akatoa amri hii katika ufalme wake wote, vilevile alituma habari hizo kwa njia ya maandiko:
23
“Hivi ndivyo anavyosema Kiro mufalme wa Persia: ‘Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote za ulimwengu, na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, katika inchi ya Yuda. Basi sasa kila mutu kati yenu, ninyi wote munaokuwa watu wa Yawe, Mungu wake akuwe pamoja naye, na aende.’ ”
← Chapter 35
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36