bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 6
2 Chronicles 6
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 7 →
1
Halafu Solomono akasema: “Yawe alisema kwamba atakaa katika giza kubwa.
2
Hakika nimekujengea nyumba tukufu kuwa makao yako ya milele.”
3
Kisha Solomono akageukia mukutano wote wa watu wa Israeli wakiwa wanasimama akawabariki.
4
Akasema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, maana kwa nguvu zake ametimiza ahadi yake aliyoitoa kwa baba yangu Daudi akisema:
5
‘Tangu nilipowaondoa watu wangu kutoka inchi ya Misri, sikuchagua muji wowote katika makabila ya Waisraeli kusudi nijengewe nyumba nitakamoabudiwa; na sikumuchagua mutu yeyote akuwe mukubwa wa watu wangu Waisraeli.
6
Lakini kisha nilichagua muji wa Yerusalema ukuwe muji ambamo nitaabudiwa, na nilimuchagua Daudi awatawale watu wangu Waisraeli.’
7
“Kwa hiyo, baba yangu Daudi alikusudia kujenga nyumba ambamo Yawe, Mungu wa Israeli, atakamoabudiwa.
8
Lakini Yawe alimwambia baba yangu Daudi: ‘Ni vizuri kwamba ulikusudia ndani ya moyo wako kunijengea nyumba.
9
Hata hivyo, si wewe utakayejenga nyumba, lakini mwana wako utakayemuzaa ndiye atakayenijengea ile nyumba.’ ”
10
“Na sasa Yawe ametimiza ahadi yake, maana nimekuwa mufalme kwa pahali pa baba yangu Daudi, na kuikaa juu ya kiti cha kifalme cha Israeli kama vile Yawe alivyoahidi; tena nimejenga nyumba ya kumwabudia Yawe, Mungu wa Israeli.
11
Katika nyumba hiyo nimeweka Sanduku la Agano, ambalo ndani yake kuna agano la Yawe alilofanya na watu wa Israeli.”
12
Kisha, Solomono akasimama mbele ya mazabahu ya Yawe, halafu mbele ya mukutano wote wa watu wa Israeli, akainua mikono yake juu.
13
Solomono alikuwa ametengeneza mimbari ya shaba ambayo aliweka katikati ya kiwanja. Urefu na upana wake ulikuwa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano, na urefu kwenda juu metre moja na sentimetre makumi mbili na tano. Akapanda juu ya mimbari na kupiga magoti mbele ya watu wote wa Israeli, akainua mikono yake kuelekea mbinguni.
14
Aliomba akisema: “Ee, Yawe, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu mwingine kama wewe, mbinguni au katika dunia. Wewe ni mwaminifu, maana umetimiza agano lako na kutenda mema kwa watumishi wako wanaoishi wakikutii kwa moyo wao wote.
15
Umetimiza ahadi uliyotoa kwa mutumishi wako baba yangu Daudi, kweli, yale uliyosema umeyatimiza leo kwa uwezo wako mwenyewe.
16
“Kwa hiyo sasa, Ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba tena utimize ile ahadi uliyomwahidi mutumishi wako Daudi baba yangu, ukisema: ‘Siku zote utakuwa na mutu wa uzao wako wa kuikaa katika kiti cha kifalme cha Israeli, ikiwa wazao wako wataangalia mwenendo na kushika sheria zangu kama vile wewe ulivyofanya mbele yangu.’
17
Sasa, ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakusihi utimize yote uliyomwahidi mutumishi wako Daudi.
18
“Lakini, ee Mungu kweli utakaa humu katika dunia na wanadamu, ikiwa hata mbingu zenyewe, wala mbingu za mbingu za juu sana hazikutoshi? Namna gani nyumba hii ambayo nimejenga itakutoshelea?
19
Hata hivyo, ee Yawe, Mungu wangu, mimi mutumishi wako, ninakuomba unisikilize na kunitimizia ombi langu ninaloomba leo.
20
Uchunge nyumba hii muchana na usiku pahali ambapo umechagua watu wako waliabudie jina lako. Unisikilize mimi mutumishi wako ninapokuja pahali hapa kuomba.
21
Sikia maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watu wako Waisraeli wanapoomba wakielekea pahali hapa. Usikilize maombi kutokea kule mbinguni na ukisha kusikia, usamehe.
22
“Mutu akimukosea mwenzake, naye akiletwa apate kuapa mbele ya mazabahu yako katika nyumba hii, na akiapa tafazali
23
wewe usikilize kutokea kule mbinguni, utende na kuwahukumu watumishi wako. Anayekuwa na kosa umwazibu kadiri ya makosa yake; asiyekuwa na kosa umwachilie na kumupatia haki kadiri ya uhaki wake.
24
“Wakati watu wako Waisraeli watakaposhindwa na waadui zao, kwa sababu ya zambi walizotenda mbele yako, nao wakitubu kwako na kusifu jina lako, wakiomba musamaha wako kwa unyenyekevu, katika nyumba hii,
25
basi, usikilize kutokea kule mbinguni. Usamehe zambi zao na uwarudishe katika inchi uliyowapa wao na babu zao.
26
“Mvua isiponyesha kwa sababu wametenda zambi mbele yako, wakiomba wakielekea pahali hapa na kusifu jina lako, tena wakiacha zambi zao, tafazali
27
uwasikilize kutokea kule mbinguni, na usamehe zambi za watumishi wako watu wako Waisraeli, nawe ukiwafundisha kufuata njia nzuri, unyeshe mvua katika inchi yako hii ambayo uliwapa watu wako ikuwe urizi.
28
“Ikiwa kuna njaa katika inchi au ugonjwa mukali, ukosefu wa mvua, ugonjwa wa mimea, nzige au vidudu vingine, au ikiwa watu wako wakishambuliwa na waadui zao katika muji wao wowote, ikiwa kuna pigo lolote au ugonjwa wowote,
29
tafazali usikilize maombi yoyote yatakayoombwa na mutu yeyote au watu wako wote Waisraeli, kila mutu akijua taabu yake na huzuni yake akikuomba naye akinyoosha mikono yake kuelekea nyumba hii,
30
basi usikilize kutokea kule mbinguni, utoe musamaha, vilevile umutendee kila mutu kadiri anavyostahili, (maana ni wewe tu unayejua mawazo ya mioyo ya wanadamu wote),
31
kusudi wakutii na kwenda katika njia zako wakati wote wanapoishi katika inchi uliyowapa babu zetu.
32
“Na hata mugeni asiyekuwa Mwisraeli atakayekuja kutoka inchi ya mbali kwa ajili ya jina lako kubwa, na juu ya nguvu na ulinzi wako, akikuja kuomba katika nyumba hii,
33
ninakusihi umusikilize toka kule kwako mbinguni, na umujalie yule mugeni yote atakayokuomba kusudi watu wote katika ulimwengu wapate kujua jina lako na kukutii kama vile watu wako Waisraeli walivyofanya na wapate kufahamu kwamba nyumba hii ambayo nimejenga inajulikana kwa jina lako.
34
“Watu wako wakienda kwenye vita kupigana na waadui zao kokote kule utakakowapeleka, nao wakikuomba wakielekea muji huu uliochagua na nyumba ambayo nimejenga kwa ajili ya jina lako,
35
ninakusihi usikilize maombi yao na malalamiko yao ukiwa kule mbinguni na uwapatie ushindi katika vita.
36
“Ikiwa watatenda zambi mbele yako, maana hakuna mutu asiyetenda zambi, na ukiwakasirikia na kuwaacha washindwe na waadui, hata wapelekwe kuwa watumwa mpaka inchi ya mbali au ya karibu,
37
kama watakapokuwa kule katika uhamisho watajifikiri kwa roho yao yote na kwa moyo wao wote na kutubu na kukuomba musamaha, wakisema: ‘Tumetenda zambi; tumepotoka na kufanya maovu’,
38
tena kama watatubu kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote wakati watakapokuwa katika inchi ya uhamisho, na kama watakuomba wakielekea inchi yao ambayo uliwapatia babu zao, muji huu ambao uliuchagua na nyumba hii ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako,
39
basi, ninakusihi usikilize ukiwa kule mbinguni maombi yao na malalamiko yao na uwapatie haki zao tena uwasamehe watu wako ambao wametenda zambi mbele yako.
40
“Sasa ee Mungu wangu, utuangalie na upokee maombi tutakayoomba pahali hapa.
41
“Sasa, ee Yawe, Mungu, uingie pahali pako pa kupumzika, wewe pamoja na Sanduku la Agano la nguvu zako. “Ee Yawe, Mungu, makuhani wako wapate wokovu, na watakatifu wako wafurahie uzuri wako.
42
“Ee Yawe, Mungu, usimugeuzie masiya wako mugongo. Kumbuka wema wako kwa mutumishi wako Daudi.”
← Chapter 5
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 7 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36