bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 16
2 Chronicles 16
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 15
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 17 →
1
Katika mwaka wa makumi tatu na sita wa utawala wa mufalme Asa, Basha, mufalme wa Israeli, alishambulia inchi ya Yuda na kuanza kujenga muji wa Rama kusudi apate kuzuia mutu yeyote asitoke wala asiingie kwa Asa, mufalme wa Yuda.
2
Kwa hiyo mufalme Asa akatwaa feza na zahabu kutoka katika hazina ya nyumba ya Yawe na ya nyumba ya kifalme, akazituma Damasiki kwa Beni-Hadadi, mufalme wa Suria, na ujumbe akasema:
3
“Tufanye mapatano ya ushirikiano kati yangu na wewe kama vile baba yangu na baba yako walivyofanya. Angalia ninakutumia zawadi ya feza na zahabu, kwenda uvunje mapatano ya ushirikiano unaokuwa kati yako na mufalme Basha wa Israeli kusudi aache mashambulizi juu yangu.”
4
Hapo mufalme Beni-Hadadi akakubali pendekezo la mufalme Asa. Akawatuma majemadari wake na majeshi yake kwenda kushambulia miji ya Israeli. Nao wakateka miji ya Iyoni, Dani, Abeli-Maimu, na miji yote ya Nafutali iliyokuwa na hazina.
5
Mufalme Basha alipopata habari za mashambulizi hayo, akaacha kujenga muji wa Rama, akasimamisha kazi yake.
6
Kisha mufalme Asa aliwapeleka watu wote wa inchi ya Yuda, wakahamisha mawe ya Rama na mbao, vifaa ambavyo Basha alitumia kwa kujenga. Kisha Asa akatumia vifaa hivyo kwa kujenga miji ya Geba na Misipa.
7
Kwa wakati ule, nabii Hanani akamwendea mufalme Asa wa Yuda, akamwambia: “Kwa sababu ulimutegemea mufalme wa Suria kuliko kumutegemea Yawe, Mungu wako, jeshi la mufalme wa Suria limekuponyoka.
8
Wale Waetiopia na Walibia hawakukuwa jeshi kubwa na magari na waaskari wapanda-farasi wengi? Lakini kwa vile ulimutegemea Yawe, yeye aliwatia katika mikono yako.
9
Yawe anachunga kwa uangalifu ulimwengu wote, kwa kuwapa nguvu wale wanaokuwa waaminifu kwake. Umetenda jambo la kipumbafu, kwa hiyo tangu sasa, utakuwa na vita kila mara.”
10
Kwa hiyo, Asa akamukasirikia sana nabii Hanani, hata akamuweka katika kifungo; maana amekuwa na hasira kubwa naye juu ya maneno yale. Wakati uleule, Asa akaanza kuwatesa vikali wamoja kati ya watu.
11
Matendo ya Asa, toka mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda na Israeli.
12
Katika mwaka wa makumi tatu na kenda wa utawala wake, Asa akashikwa na ugonjwa wa miguu. Ugonjwa ule ukazidi sana kuongezeka. Lakini hata wakati ule, Asa hakumugeukia Yawe amusaidie, lakini alijitafutia musaada kutoka kwa waganga.
13
Asa akakufa katika mwaka wa makumi ine na moja wa utawala wake.
14
Akazikwa katika kaburi alilokuwa amejichimbia yeye mwenyewe, katika muji wa Daudi. Walimulalisha juu ya kitanda kilichokuwa kimejazwa marasi ya kila aina yaliyotayarishwa na wafundi wa kutengeneza marasi, wakawasha moto mukubwa sana kwa heshima yake.
← Chapter 15
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 17 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36