bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 15
2 Chronicles 15
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 14
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 16 →
1
Roho wa Mungu alimujaza Azaria mwana wa Obedi,
2
naye akatoka kwenda kukutana na mufalme Asa, akamwambia: “Unisikilize, ee Asa na watu wote wa kabila la Yuda na la Benjamina! Yawe yuko pamoja nanyi, ikiwa mutakuwa pamoja naye. Mukimutafuta, mutamupata, lakini mukimwacha, naye atawaacha.
3
Kwa muda murefu sasa, Waisraeli wameishi bila Mungu wa kweli, wala makuhani wa kuwafundisha, na bila Sheria.
4
Lakini walipopatwa na shida, walimugeukia Yawe, Mungu wa Israeli, wakamutafuta, wakamupata.
5
Katika siku zile, hakuna mutu aliyeweza kuingia wala kutoka kwa usalama kwa sababu hapakukuwa amani; fujo nyingi sana ziliwasumbua wanainchi wa kila inchi.
6
Taifa moja lilipigana na taifa lingine na muji mumoja ulipigana na muji mwingine, kwa sababu Mungu aliwafazaisha kwa taabu za kila aina.
7
Lakini ninyi mujipe moyo, wala musiregee kwa maana mutapata malipo kwa kazi munayofanya.”
8
Asa aliposikia maneno haya, ni kusema unabii wa Azaria mwana wa Odedi, yakamutia moyo. Akaondoa sanamu zote za kuchukiza katika inchi yote ya Yuda na ya Benjamina, na kutoka katika miji yote aliyoteka katika inchi ya milima ya Efuraimu. Na kisha akatengeneza upya mazabahu ya Yawe iliyokuwa katika baraza la nyumba ya Yawe.
9
Asa akakusanya watu wote wa Yuda na Benjamina, na wengine wote waliokuwa wakikaa katika inchi yake kutoka kabila la Efuraimu, la Manase na la Simeoni. Hawa walikuja kwake walipoona kwamba Yawe, Mungu wake yuko pamoja naye.
10
Wote walikusanyika Yerusalema katika mwezi wa tatu wa mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
11
Siku ile, walimutolea Yawe sadaka za ngombe mia saba na kondoo elfu saba, kutoka katika vile vitu walivyoteka.
12
Nao wakafanya agano, kwamba watamutafuta Yawe, Mungu wa babu zao, kwa moyo wote na kwa roho yao yote;
13
na kwamba yeyote asiyemutafuta Yawe, Mungu wa Israeli, akuwe kijana au muzee, mwanaume au mwanamuke, sharti auawe.
14
Walimwapia Yawe kwa sauti kubwa, wakalalamika zaidi, wakapiga ngunga na baragumu.
15
Watu wote wa Yuda walikuwa na furaha tele kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wote. Walikuwa wamemutafuta kwa hamu, wakamupata. Naye Yawe akawapa amani pande zote.
16
Mufalme Asa alimwondoa hata mama yake Maka, cheo chake cha malkia, kwa sababu alitengeneza sanamu ya kuchukiza ya Ashera, mungu wa kike. Asa alikatakata sanamu hiyo, akaipondaponda na kuiteketeza kwa moto katika bonde la kijito Kidroni.
17
Lakini hata hivyo pahali pa kutambikia miungu mingine katika Israeli hapakuharibiwa; lakini yeye alikuwa na moyo mwaminifu maisha yake yote.
18
Alivirudisha katika nyumba ya Mungu vifaa vyote vilivyotakaswa na baba yake pamoja na vile alivyotakasa yeye mwenyewe; feza na zahabu na vyombo vingine.
19
Hapakukuwa vita tena katika inchi mpaka mwaka wa makumi tatu na tano wa utawala wa Asa.
← Chapter 14
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 16 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36