bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
2 Chronicles 35
2 Chronicles 35
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 34
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 36 →
1
Mufalme Yosia akafanyia Yawe sikukuu ya Pasaka katika Yerusalema, wakachinja wana-kondoo wa Pasaka siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza.
2
Akawaweka makuhani kwa kazi zao ambazo walihitajika kufanya katika nyumba ya Yawe na kuwatia moyo wazifanye kwa ukamilifu.
3
Pamoja na hayo, akawapa Walawi waliowafundisha watu wa Israeli na ambao walitakaswa kwa ajili ya Yawe, maagizo haya: “Muweke Sanduku takatifu ndani ya nyumba ambayo Solomono mwana wa Daudi, mufalme wa Israeli aliyojenga; hamuhitaji kulibebabeba tena juu ya mabega. Sasa mumutumikie Yawe, Mungu wenu, na watu wake Waisraeli.
4
Mushike kazi yenu kulingana na ukoo zenu, kufuatana na maagizo ya Daudi mufalme wa Israeli na ya Solomono mwana wake.
5
Musimame vilevile Pahali Patakatifu kama vile wasimamizi wa jamaa za ukoo zenu wasiofanya kazi za ukuhani, na kila mumoja asimamie jamaa moja ya Walawi.
6
Muchinje mwana-kondoo wa Pasaka, mujitakase, halafu mutayarishe Pasaka kwa ajili ya wandugu zenu, kusudi waweze kutimiza neno la Yawe lililosemwa na Musa.”
7
Kisha Yosia akawapa watu, wana-mbuzi yapata elfu makumi tatu, na ngombe dume elfu tatu, wote hawa toka katika makundi ya mufalme.
8
Nao wakubwa wake, kwa mapenzi yao, waliwapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zakaria na Yehieli, wasimamizi wa nyumba ya Mungu, waliwapa makuhani wana-kondoo na wana-mbuzi elfu mbili mia sita na ngombe dume mia tatu kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
9
Naye Konania na wandugu zake wawili, Semaya na Netaneli, pamoja na Hasabia, Yeieli na Yozabadi, waliokuwa viongozi wa Walawi, nao vilevile waliwapa wana-kondoo na wana-mbuzi elfu tano na ngombe dume mia tano, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
10
Basi utaratibu wa kazi ukapangwa, makuhani wakasimama pahali pao, na Walawi katika makundi yao; sawasawa na amri ya mufalme.
11
Wakachinja mwana-kondoo wa Pasaka, nao makuhani wakanyunyiza damu waliyopokea kwa mikono yao nao Walawi wakachuna nyama.
12
Halafu wakatenga sadaka za kuteketeza kwa moto kusudi wapate kuzigawanya kwa watu kulingana na jamaa zao kusudi wamutolee Yawe kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Musa. Nao wakafanya vile vile na wale ngombe dume.
13
Wakachoma mwana-kondoo wa Pasaka juu ya moto kufuatana na maagizo; vilevile wakatokotesha sadaka takatifu katika vyungu, masufuria na kwenye vikaango, na kuwagawanyia upesiupesi watu wasiofanya kazi ya ukuhani.
14
Kisha, Walawi wakafanya matayarisho kwa ajili yao wenyewe na kwa makuhani kwa maana makuhani wa uzao wa Haruni walikuwa wanashugulika na kutoa sadaka za kuteketeza kwa moto, na vipande vya mafuta, mpaka usiku; kwa hiyo Walawi walitayarisha kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Haruni.
15
Nao waimbaji wa uzao wa Asafu wakashika nafasi zao, kufuatana na maagizo ya mufalme Daudi, Asafu, Hemani na Yedutuni, nabii wa mufalme. Nao walinzi wa mulango walikuwa kwenye milango; hawakuhitajika kuacha nafasi zao za kazi kwa sababu wandugu zao Walawi waliwatayarishia Pasaka.
16
Hivyo basi, kazi yote ya Yawe ikatayarishwa siku hiyo, kwa kufanya Pasaka na kutoa sadaka za kuteketeza kwenye mazabahu ya Yawe; kama vile mufalme Yosia alivyoamuru.
17
Wakati ule watu wote wa Israeli waliokuwa pale walifanya sikukuu hiyo ya Pasaka na sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa muda wa siku saba.
18
Pasaka kama hiyo ilikuwa haikufanyika katika Israeli yote tangu siku za nabii Samweli. Hakujatokea mufalme hata mumoja wa Israeli aliyefanya Pasaka kama hii iliyofanyika na mufalme Yosia, makuhani, Walawi na watu wote wa inchi ya Yuda, wa Israeli vilevile na wakaaji wa Yerusalema.
19
Pasaka hiyo ilifanyika katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa mufalme Yosia.
20
Nyuma ya haya yote mufalme Yosia aliyofanya kwa ajili ya hekalu, Neko, mufalme wa Misri akapanda kwenda kushambulia Karkemisi kwenye muto Furati. Naye mufalme Yosia akatoka kwa kumushambulia,
21
lakini mufalme Neko akamutumia ujumbe akisema: “Vita hivi havikuelekei wewe hata kidogo, ewe mufalme wa Yuda. Sikukuja kupigana nawe lakini na waadui zangu, na Mungu ameniamuru niharakishe. Acha basi kumupinga Mungu, ambaye yuko upande wangu, kama sivyo atakuangamiza.”
22
Lakini Yosia hakukubali kumwachilia. Akakataa kusikiliza maneno Mungu aliyosema kwa njia ya Neko, kwa hiyo akajibadilisha kusudi asitambulikane, kisha akaingia katika vita katika bonde la Megido.
23
Nao wapiga upinde wakamuchoma mufalme Yosia mishale; basi mufalme akawaambia watumishi wake: “Muniondoshe! Nimeumia vibaya sana.”
24
Basi watumishi wake walipomutoa katika gari lake la vita, wakamubeba na gari lake la pili mpaka Yerusalema. Naye akakufa na kuzikwa katika makaburi ya kifalme. Watu wote wa inchi ya Yuda na Yerusalema wakaomboleza kifo cha Yosia.
25
Nabii Yeremia vilevile akatunga shairi la maombolezo kwa ajili ya kifo chake; nao waimbaji wote, wanaume na wanawake, wanamutaja Yosia katika maombolezo yao, mpaka leo. Wakakusudia kuwa wanafanya maombolezo haya katika Israeli; angalia nayo yameandikwa katika Maombolezo.
26
Matendo mengine ya Yosia na matendo yake mema kama vile yalivyoandikwa katika Sheria ya Yawe,
27
na matendo yake tangu mwanzo mpaka mwisho, angalia yameandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli na Yuda.
← Chapter 34
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 29
Chapter 30
Chapter 31
Chapter 32
Chapter 33
Chapter 34
Chapter 35
Chapter 36
Chapter 36 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
29
30
31
32
33
34
35
36