bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 1
Acts 1
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 2 →
1
Katika kitabu changu cha kwanza nilikuelezea mambo yote Yesu aliyofanya na kufundisha tangu alipoanza kazi yake
2
mpaka siku ile aliponyanyuliwa mbinguni. Mbele ya kunyanyuliwa kule, alitoa maagizo kwa njia ya Roho Mutakatifu kwa watu aliokuwa amewachagua kuwa mitume wake.
3
Nyuma ya kufa kwake, alijionyesha kwao kwa namna nyingi kwa kuhakikisha kwamba amefufuka. Kwa muda wa siku makumi ine, alionekana kwao na kusema nao juu ya maneno yanayoelekea Ufalme wa Mungu.
4
Siku moja alipokuwa akikusanyika pamoja nao, akawaagiza: “Musitoke Yerusalema, lakini mubaki kule mukingojea zawadi ambayo Baba yangu aliahidi, ile niliyowaambia ninyi.
5
Kwa maana Yoane alibatiza kwa maji, lakini kisha siku chache, ninyi mutabatizwa kwa Roho Mutakatifu.”
6
Basi mitume walipokusanyika pamoja na Yesu, wakamwuliza: “Bwana, wakati huu ndio utakapowarudishia Waisraeli ufalme wao?”
7
Yesu akawajibu: “Si kazi yenu kutambua siku wala nyakati Baba yangu alizopanga kwa mamlaka yake mwenyewe.
8
Lakini mutapokea uwezo wakati Roho Mutakatifu atakaposhuka juu yenu. Nanyi mutakuwa washuhuda wangu katika Yerusalema, katika Yudea yote na Samaria na hata katika inchi zote za dunia.”
9
Kisha kusema maneno haya, Yesu akanyanyuliwa mbinguni, nao walikuwa wakimwangalia. Na wingu likamuficha hata hawakumwona tena.
10
Walipokuwa wangali wakiangalia mbinguni wakati Yesu alipopanda, kwa rafla kukaonekana watu wawili wanaovaa nguo nyeupe, wakasimama karibu nao.
11
Watu hao wakawaambia: “Ninyi Wagalilaya, sababu gani munasimama pale mukiangalia mbinguni? Huyu Yesu aliyenyanyuliwa toka katikati yenu kwenda mbinguni, atarudi sawa vile mulivyomwona akienda.”
12
Kisha mitume wakarudi Yerusalema tokea kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa karibu na muji huo kwenye umbali wa yapata kilometre moja.
13
Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.
14
Hawa wote walikuwa wakikusanyika kwa nia moja kwa kuomba, pamoja na wanawake wamoja, Maria mama wa Yesu, na wandugu za Yesu.
15
Katika siku zile, kulikuwa mukutano wa wandugu waamini yapata watu mia moja makumi mbili. Basi Petro akasimama katikati yao, akasema:
16
“Wandugu zangu, ilikuwa lazima yale Maandiko Matakatifu yatimie ambayo Roho Mutakatifu alitabiri kwa kinywa cha mufalme Daudi juu ya Yuda, yule aliyewaongoza wale waliomukamata Yesu.
17
Yuda alikuwa mumoja wa kundi letu, naye alikuwa ameshiriki pamoja nasi katika kazi hii.”
18
(Yuda alinunua shamba kwa njia ya feza alizopata kwa ajili ya kitendo chake cha uovu. Pale akaangukia kichwa chini, maiti yakapasuka na matumbotumbo yake yote yakatoka inje.
19
Jambo hilo likajulikana na wakaaji wote wa Yerusalema, hata wakaita shamba lile katika luga yao “Akeldama,” maana yake, “Shamba la Damu.”)
20
“Kwa sababu imeandikwa hivi katika kitabu cha Zaburi: ‘Makao yake yabakie ukiwa na mutu asiishi ndani yake.’ Na imeandikwa tena: ‘Mutu mwingine atwae kazi yake.’
21
“Basi kwa hiyo, ni lazima mutu mumoja ajiunge pamoja nasi kuwa mushuhuda wa ufufuko wa Bwana Yesu. Mutu yule anapaswa kuwa mumoja kati ya wale waliokuwa wakitusindikiza kwa wakati wote Bwana Yesu alipokuwa pamoja nasi; tangia wakati Yoane alipomubatiza mpaka siku ile Yesu aliponyanyuliwa toka katikati yetu kwenda mbinguni.”
23
Basi wakataja watu wawili: mumoja alikuwa Yosefu, aliyeitwa vilevile Barisaba na aliyejulikana vilevile kwa jina la Yusto, na mwingine Matia.
24
Kisha wakaomba wakisema: “Bwana, wewe unayejua yanayokuwa ndani ya mioyo ya watu wote, utuonyeshe ni nani uliyemuchagua kati ya hawa wawili
25
kusudi atiwe katika kazi hii ya kuwa mutume kwenye nafasi Yuda aliyoacha na kwenda pahali pake mwenyewe.”
26
Halafu wakapiga kura, na kura ikamwangukia Matia. Naye akaongezwa katika kundi la wale mitume kumi na mumoja.
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 2 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28