bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 11
Acts 11
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 10
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 12 →
1
Mitume na wandugu waamini waliokuwa Yudea wakasikia kwamba watu wamoja wa mataifa mengine wameamini Neno la Mungu vilevile.
2
Na Petro aliporudi Yerusalema, wale wanafunzi Wayuda wakabishana naye,
3
wakisema: “Uliingia ndani ya nyumba ya watu wasiokuwa wa taifa letu na kula chakula pamoja nao!”
4
Halafu Petro akaanza kuwaelezea mambo yote yaliyotokea kwa utaratibu. Akawaambia:
5
“Mimi nilikuwa katika muji Yopa nikiomba. Kisha nikakuwa sawa nimezimia, nami nikapata maono. Nikaona kitu kinachokuwa kama nguo kubwa kikishuka toka mbingu, kikitelemushwa, kikishikwa kwenye pembe zake ine. Nacho kikafika karibu nami.
6
Nilipochungulia ndani yake kwa uangalifu, nikaona nyama wa ufugo wenye miguu mine, nyama wa pori, nao nyama wenye kutambaa pamoja na ndege.
7
Na nikasikia sauti ikiniambia: ‘Petro, simama. Chinja na ukule!’
8
Lakini nikajibu: ‘Hapana, hata kidogo, ee Bwana! Ndani ya kinywa changu hamujaingia bado kitu chochote kisichoruhusiwa kukuliwa wala chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu.’
9
Lakini sauti ikanirudilia kutoka mbingu ikisema: ‘Vitu vilivyotakaswa na Mungu, usivihesabu kuwa vichafu.’
10
Nayo maneno haya yakasikilika tena mara tatu, kisha vile vitu vyote vikanyanyuliwa mbinguni.
11
Na saa ile ile watu watatu waliotumwa kwangu kutoka muji Kaisaria wakafika kwa mulango wa nyumba niliyokaa ndani yake.
12
Naye Roho Mutakatifu akaniambia kwamba niende pamoja nao bila kusita. Na hawa wandugu sita munaowaona wakanisindikiza, nasi tukafika na kuingia sisi wote ndani ya nyumba ya Kornelio.
13
Naye akatuelezea namna malaika alivyomutokea ndani ya nyumba yake na kumwambia: ‘Tuma wajumbe, kwenda Yopa kwa kumwita Simoni, anayeitwa vilevile Petro.
14
Ni yeye atakayekuambia mambo yanayokupasa wewe pamoja na watu wote wa nyumba yako kusudi mupate kuokolewa.’
15
Nami nilipoanza kusema, Roho Mutakatifu akashuka juu yao sawa vile alivyoshuka juu yetu kwanza.
16
Halafu nikakumbuka maneno haya Bwana aliyosema: ‘Yoane amebatiza kwa maji, lakini ninyi mutabatizwa kwa Roho Mutakatifu.’
17
Basi ikiwa Mungu aliwapa wale watu zawadi ile ile Roho Mutakatifu aliyotupatia sisi wakati tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani hata nisubutu kupingana na Mungu?”
18
Wandugu waamini waliposikia maneno hayo, wakatulia na kumusifu Mungu, wakisema: “Kumbe Mungu amewajalia hata watu wa mataifa mengine vilevile kusudi waweze kugeuka toka zambi na kupata uzima kamili.”
19
Nyuma ya kuuawa kwa Stefano, wanafunzi walisambaa kwa ajili ya mateso. Nao wakasafiri mpaka katika inchi ya Foinikia na ya Kipuro na kufika katika muji Antiokia. Na kule walihubiri Neno la Mungu, lakini kwa Wayuda peke yao tu.
20
Lakini kulitokea wanafunzi wengine, waliokuwa watu wa Kipuro na wa inchi ya Kurene, waliofika Antiokia. Nao wakaanza kusemezana na Wagriki vilevile, wakiwahubiri Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21
Na Bwana akawaongoza kwa uwezo wake, hata watu wengi sana wakaamini neno la Bwana na kumugeukia.
22
Watu wa kanisa la Yerusalema waliposikia habari hii, wakamutuma Barnaba kwenda kule Antiokia.
23
Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.
24
Barnaba alikuwa mutu mwema, mwenye kujazwa na Roho Mutakatifu na mwenye imani sana. Na watu wengi wakaongezeka kwa Bwana.
25
Kisha Barnaba akatoka kule na kwenda Tarso kwa kumutafuta Saulo.
26
Naye alipomwona, akamuleta Antiokia. Na kwa muda wa mwaka muzima Barnaba na Saulo walikusanyika katika kanisa la kule na wakawafundisha watu wengi. Ni kule Antiokia ndiko wanafunzi waliitwa kwa mara ya kwanza jina la Wakristo.
27
Katika siku zile, manabii wamoja walifika Antiokia wakitoka Yerusalema.
28
Na mumoja wao, aliyeitwa Agabo, akasimama, akatabiri kwa njia ya Roho Mutakatifu kwamba kutakuwa njaa kubwa katika dunia nzima. (Nayo ikatokea katika nyakati za utawala wa mufalme Klaudio wa Roma.)
29
Wanafunzi wakakusudia kutuma musaada kwa wandugu waamini waliokaa katika jimbo la Yudea, kila mumoja kwa kadiri alivyoweza kutoa.
30
Nao wakafanya vile, wakatuma misaada waliyokusanya kwa wazee wa kanisa kwa mukono wa Barnaba na Saulo.
← Chapter 10
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 12 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28