bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 25
Acts 25
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 24
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 26 →
1
Siku tatu nyuma ya kufika kwake katika jimbo lile, Festo akaondoka Kaisaria na kwenda Yerusalema.
2
Kule wakubwa wa makuhani na wakubwa wa Wayuda wakamushitaki Paulo mbele yake.
3
Wakamusihi Festo awafanyie wema kwa kuwaletea Paulo Yerusalema, kwa maana walikuwa wakivizia kumwua katika njia.
4
Festo akajibu: “Paulo analindwa katika kifungo kule Kaisaria, na mimi mwenyewe nitaenda kule sasa hivi.
5
Basi wamoja kati ya wakubwa wenu waende pamoja nami Kaisaria nao wamushitaki kule ikiwa alifanya ubaya wowote.”
6
Kisha kukaa pamoja nao muda wa siku nane au kumi, Festo akarudi Kaisaria. Kesho yake akaikaa ndani ya tribinali na kuamuru wamulete Paulo.
7
Wakati Paulo alipofika, wale Wayuda waliotoka Yerusalema wakamuzunguka na kutoa mashitaki mengi mazito juu yake ambayo wao hawawezi kuhakikisha.
8
Halafu Paulo akajitetea, akisema: “Mimi sikufanya kosa lolote juu ya Sheria ya Musa, juu ya hekalu, wala juu ya Mufalme wa Roma.”
9
Festo aliyetaka kujipendekeza kwa Wayuda, akamwuliza Paulo: “Unataka niende kukusambishia maneno haya kule Yerusalema?”
10
Paulo akajibu: “Mimi ninasimama mbele ya tribinali ya Mufalme wa Roma, na ni hapa ninapopaswa kusambishwa. Sikuwakosea Wayuda kosa lolote, kama vile wewe mwenyewe unavyojua vizuri.
11
Kama mimi ni mukosaji au nimefanya kitendo kinachonipasa kuuawa, mimi sikatai kufa. Lakini kama hakuna ukweli wowote katika mashitaki yao juu yangu, hakuna mutu anayeweza kunitoa kwao. Ninaomba kusambishwa na Mufalme wa Roma.”
12
Basi Festo alipokwisha kukata shauri pamoja na washauri wake, akajibu: “Unaomba kusambishwa na Mufalme wa Roma, basi utakwenda kwa Mufalme wa Roma.”
13
Kulipopita siku chache, mufalme Agripa na dada yake Berenike wakafika Kaisaria kumusalimia Festo.
14
Kufuatana na vile walikaa kule siku nyingi, Festo akamwelezea mufalme maneno ya Paulo. Akamwambia: “Hapa kuna mutu mumoja aliyeachwa na Feliki katika kifungo.
15
Wakati nilipokwenda Yerusalema, wakubwa wa makuhani na wazee wa Wayuda walimushitaki na kuniomba nimuhukumu.
16
Nami nikawajibu kwamba si desturi ya Waroma kumutoa mutu yeyote aliyeshitakiwa mbele ya kusamba uso kwa uso na washitaki wake na kupata nafasi ya kujitetea juu ya jambo walilomushitakia.
17
Basi walipofika hapa pamoja nami, sikupoteza wakati lakini kesho yake nikaikaa ndani ya tribinali na kuamuru wamulete mutu yule.
18
Nao washitaki wake waliposimama, hawakumushitaki juu ya neno baya kama nilivyokuwa ninawazia.
19
Walikuwa tu wakibishana naye juu ya dini yao wenyewe na juu ya mutu mumoja aliyeitwa Yesu; lakini Paulo alidai kwamba yuko muzima.
20
Kwa ngambo yangu sikujua nifanye nini kwa kuchunguza ukweli wa mabishano hayo. Nikamwuliza Paulo kama anataka kwenda Yerusalema kusambishwa kule juu ya maneno yale.
21
Lakini wakati Paulo alipoomba maneno yake yakatwe na Mufalme wa Roma, nikaamuru alindwe katika kifungo mpaka nitakapomutuma kwa Mufalme wa Roma.”
22
Halafu Agripa akamwambia Festo: “Na mimi vilevile ningependa kumusikiliza mutu huyu peke yangu.” Festo akajibu: “Utamusikiliza kesho.”
23
Basi kesho yake Agripa pamoja na Berenike walifika katika shangwe kubwa na kuingia katika chumba cha mukutano, pamoja na wakubwa wa jeshi, na wakubwa wa muji. Festo akaamuru wamulete Paulo.
24
Halafu Festo akasema: “Mufalme Agripa, na ninyi wote munaokuwa hapa pamoja nasi, munamwona mutu huyu Wayuda wote waliyemushitaki kwangu kule Yerusalema na hapa vilevile wakilalamika kwamba hastahili kuishi tena.
25
Mimi niliona kwamba hakufanya kitendo chochote cha kustahili kufa. Lakini kwa sababu yeye mwenyewe aliomba maneno yake yakatwe na Mufalme wa Roma, nilikusudia kumutuma kwake.
26
Mimi sina maneno kamili ya kumwandikia Mufalme wa Roma juu yake. Ndiyo maana nimemuleta mbele yenu na zaidi mbele yako, wewe mufalme Agripa, kusudi kisha kumwuliza, nipate maneno ya kuandika.
27
Kwa sababu ninaona kwamba haina maana kumutuma mufungwa pasipo kueleza wazi mashitaki juu yake.”
← Chapter 24
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 26 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28