bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 5
Acts 5
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 6 →
1
Vilevile kulikuwa mutu mwingine mumoja aliyeitwa Anania. Yeye alipokwisha kupatana na muke wake Safira, akauzisha shamba lake.
2
Lakini akaficha sehemu ya feza alizopata na kuleta sehemu iliyobaki kwa mikono ya mitume. Muke wake alijua maneno hayo yote.
3
Basi Petro akamwuliza: “Anania, namna gani Shetani amekuingia hata akakusemesha uongo mbele ya Roho Mutakatifu na kuficha sehemu ya feza ulizopata ulipouzisha lile shamba?
4
Mbele haujauzisha lile shamba, si lilikuwa mali yako? Na nyuma ya kuliuzisha, feza ulizopata haungezitumia sawa unavyotaka? Basi namna gani ulikusudia kufanya jambo kama hili? Haukusema uongo mbele ya watu, lakini mbele ya Mungu!”
5
Anania aliposikia maneno hayo, mara moja akaanguka chini na kufa. Na wote waliosikia habari ile wakashikwa sana na woga.
6
Kisha vijana wakakuja, wakafunika maiti yake wakamubeba mbali na muji na kumuzika.
7
Kulipopita karibu saa tatu, muke wake akafika pasipo kujua mambo yaliyotokea.
8
Petro akamwuliza: “Uniambie, hii ndiyo jumla ya feza mulizopata mulipouzisha shamba lenu?” Akamujibu: “Ndiyo, ni hii.”
9
Halafu Petro akamwambia: “Namna gani mulipatana kwa kumupima Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale wanaotoka kumuzika mume wako wamefika hapa kwenye mulango, nao watakupeleka vilevile.”
10
Mara moja Safira akaanguka chini mbele ya Petro na kufa. Halafu wale vijana wakaingia ndani, wakamukuta amekwisha kufa. Basi wakamubeba mbali na muji na kumuzika kule karibu na mume wake.
11
Halafu, kanisa lote na wote waliosikia habari ile wakashikwa sana na woga.
12
Mitume walifanya maajabu na vitambulisho vingi katikati ya watu. Waamini wote walizoea kukusanyika katika Baraza wanaloliita La Solomono.
13
Na hapakukuwa hata mutu mumoja asiyekuwa mwamini aliyesubutu kujiunga nao, lakini hata hivi wanafunzi walisifiwa sana na watu.
14
Hesabu ya watu waliomwamini Bwana, wanaume na wanawake, ilizidi kuongezeka sana.
15
Na kufuatana na mambo yote yaliyotokea, watu waliwapeleka wagonjwa katika barabara, wakiwalalisha juu ya mikeka na vipoyi kusudi Petro atakapopita, kivuli chake kipate tu kufika kwenye wamoja wao.
16
Watu wengi vilevile kutoka miji inayokuwa pembeni ya Yerusalema walikusanyika, wakiwaleta wagonjwa na watu wanaoteswa na pepo, na wote wakaponyeshwa.
17
Halafu Kuhani Mukubwa na washiriki wake wote, ndio watu wa chama cha Wasadukayo, wakawaonea mitume wivu.
18
Basi wakafunga mitume na kuwapeleka ndani ya nyumba kubwa ya kifungo.
19
Lakini usiku malaika wa Bwana akafungua milango ya kifungo, akawaondosha mitume mule na kuwaambia:
20
“Mwende ndani ya hekalu na mutangaze kwa watu maneno yote yanayoelekea uzima mupya.”
21
Na sawa vile walivyoambiwa, asubui mapema wakaingia ndani ya hekalu, na kuanza kuwafundisha watu. Kuhani Mukubwa na wale washiriki walipofika, wakawakusanya wasimamizi wote wa Waisraeli kwa kufanya mukutano wa Baraza Kubwa. Nao wakawatuma watu kwenye kifungo kwa kuwaleta mitume.
22
Lakini wale walinzi waliotumwa walipofika, hawakuwakuta mitume ndani ya kifungo. Basi wakarudi na kutoa habari hii:
23
“Tulikuta kifungo kimefungwa vizuri na waaskari walinzi wakichunga milango. Lakini wakati tulipofungua milango hatukuona mutu ndani.”
24
Mukubwa wa walinzi wa hekalu na wakubwa wa makuhani waliposikia habari hii, wakakuwa na wasiwasi sana, wakijiuliza ni nini itakayotokea.
25
Halafu mutu mumoja akakuja, na kuwaambia: “Wale watu muliowatia ndani ya kifungo wako katika hekalu wakiwafundisha watu.”
26
Basi mukubwa wa walinzi wa hekalu akaenda pamoja na watumishi wake, akawaleta mitume. Lakini hawakuwakamata kwa kinguvu kwa sababu waliogopa watu wasiwatupie mawe.
27
Walipokwisha kuwaleta, wakawasimamisha mbele ya Baraza Kubwa. Naye Kuhani Mukubwa akaanza kuwasambisha,
28
akiwaambia: “Tuliwakataza kwa nguvu musifundishe tena kwa jina la mutu huyu. Na sasa mumeeneza mafundisho yenu katika Yerusalema yote, nanyi munataka kutubebesha lazima ya kifo chake.”
29
Petro na mitume wengine wakajibu: “Inatupasa sisi kumutii Mungu kuliko watu!
30
Mungu wa babu zetu alimufufua Yesu, yule ninyi muliyemwua kwa kumutundika juu ya musalaba.
31
Mungu alimupa utukufu na kumwikalisha na mamlaka karibu naye na kumuweka kuwa Mutawala na Mwokozi. Na hivi Waisraeli wataweza kugeuka toka zambi zao na Mungu atawasamehe.
32
Na sisi ni washuhuda wa mambo hayo, naye Roho Mutakatifu ambaye Mungu aliwapa wale wanaomutii, anayashuhudia vilevile.”
33
Wajumbe wa lile Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kutaka kuwaua mitume.
34
Lakini Mufarisayo mumoja, jina lake Gamalieli, aliyekuwa mwalimu wa Sheria na aliyeheshimiwa sana na watu wote, akasimama katika baraza na kuamuru mitume wapelekwe inje kwa muda.
35
Kisha akawaambia watu wa baraza: “Ninyi wanainchi wenzangu Waisraeli, muangalie vizuri jambo hili munalotaka kuwatendea watu hawa.
36
Haijapita siku nyingi kulitokea mutu mumoja aliyeitwa Teuda. Akajidai kuwa mutu mukubwa, na karibu watu mia ine walijiunga naye. Lakini akauawa na wanafunzi wake wote wakasambazwa na kutosemekana tena.
37
Nyuma yake, katika siku zile walipofanya hesabu ya watu, kulitokea Yuda wa jimbo la Galilaya. Huyo naye aliwavuta watu wengine kwa kumufuata. Lakini yeye vilevile aliuawa na wanafunzi wake wote wakasambazwa.
38
Na sasa mimi ninawashauria ninyi, musiwafuatilie watu hawa, muwaache wajiendee. Kwa maana ikiwa mupango huu na hii kazi yao vimeanzishwa na mwanadamu, sherti vitaharibika.
39
Lakini ikiwa vimeanzishwa na Mungu, hamutaweza kuwazuiza. Basi mujiangalie vizuri musikuje kuonekana kuwa munapigana na Mungu!”
40
Wajumbe wa baraza wakakubali shauri la Gamalieli. Halafu wakawaita mitume, wakawapiga fimbo na kuamuru wasifundishe tena kwa jina la Yesu. Kisha wakawaacha kwenda.
41
Basi mitume wakatoka katika baraza, wakifurahi sana kwa sababu walistahili kuzarauliwa kwa kuteswa kwa ajili ya Yesu.
42
Na kila siku, katika hekalu na katika nyumba mbalimbali, hawakuacha kufundisha na kuhubiri Habari Njema kwamba Yesu ni Kristo.
← Chapter 4
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 6 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28