bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 9
Acts 9
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 8
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 10 →
1
Katika siku zile zile, Saulo aliendelea na vitisho vikali vya kuwaua wanafunzi wa Bwana. Siku moja akamwendea Kuhani Mukubwa
2
na kumwomba amwandikie barua za kumutambulisha katika nyumba za kuabudia za muji Damasiki. Katika barua hizo, Saulo alipewa ruhusa kwamba akiona watu wanaofuata Njia ya Bwana, ikiwa wanaume au wanawake, awafunge na kuwapeleka Yerusalema.
3
Alipokuwa katika safari karibu kufika Damasiki, kwa rafla mwangaza toka mbinguni ukamuzunguka.
4
Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”
5
Naye akauliza: “Wewe ni nani, Bwana?” Na Bwana akajibu: “Mimi ni Yesu unayemutesa.
6
Lakini simama, uingie katika muji, na mule watakuambia jambo unalopaswa kufanya.”
7
Nao watu waliosafiri pamoja na Saulo wakasimama na kubaki kimya kwa ajili ya mushangao, kwa maana walisikia sauti lakini hawakuona mutu.
8
Saulo akasimama wima, na ingawa macho yake yalikuwa wazi hakuweza kuona kitu. Halafu wakamushika mukono na kumwongoza mpaka ndani ya muji Damasiki.
9
Akabaki muda wa siku tatu pasipo kuona, naye hakukula wala kunywa kitu.
10
Na kule Damasiki kulikuwa mwanafunzi mumoja wa Yesu jina lake Anania. Bwana akamutokea katika maono, akamwita akisema: “Anania!” Naye akamwitikia, akisema: “Bwana, mimi niko hapa.”
11
Bwana akamwambia: “Kwenda katika barabara wanayoita ‘Yenye Kunyooka,’ uingie ndani ya nyumba ya Yuda, na mule umutafute mutu wa muji wa Tarso anayeitwa Saulo, utamukuta akiomba.
12
Yeye ameona katika maono mutu mumoja anayeitwa Anania, akiingia ndani ya nyumba na kuweka mikono juu yake kusudi apate kuona tena.”
13
Anania akajibu: “Bwana, nimekwisha kusikia watu wengi wakisema habari za mutu huyo, wakieleza mabaya aliyowatendea watu wako watakatifu wanaokuwa Yerusalema.
14
Na hata huku yuko na mamlaka aliyopewa na wakubwa wa makuhani kusudi afunge wote wanaoomba kwa jina lako.”
15
Lakini Bwana akamwambia: “Kwenda tu, kwa maana nimemuchagua mutu huyu kwa kunitumikia, kusudi atangaze jina langu kwa mataifa, kwa wafalme na kwa Waisraeli.
16
Nami nitamwonyesha mateso ya namna gani atakayopaswa kupata kwa ajili yangu.”
17
Basi Anania akaenda. Alipofika ndani ya nyumba ambamo Saulo alikuwa, akaweka mikono juu yake na kumwambia: “Ndugu Saulo, Bwana Yesu aliyekutokea katika njia ulipokuwa ukikuja huku, amenituma kusudi upate kuona tena na kujazwa na Roho Mutakatifu.”
18
Na pale pale vitu vilivyokuwa kama magamba vikaanguka toka ndani ya macho ya Saulo, naye akapata tena kuona. Halafu akasimama na kubatizwa.
19
Kisha akakula chakula, na kupata nguvu tena. Saulo alikaa siku chache pamoja na wanafunzi waliokuwa Damasiki.
20
Na bila kukawia akaanza kuhubiri katika nyumba za kuabudia, akitangaza kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
21
Wote waliomusikia walishangaa, wakisema: “Si mutu huyu ndiye aliyewatesa vikali kule Yerusalema watu wanaoomba kwa jina la Yesu? Hakika amefika huku nako kusudi awafunge watu kama hao na kuwapeleka kwa wakubwa wa makuhani.”
22
Lakini Saulo akazidi kuhubiri na uwezo, akawashinda Wayuda waliokaa Damasiki akihakikisha wazi kwao kwamba Yesu ndiye Kristo.
23
Na kulipokwisha kupita siku nyingi, Wayuda wakafanya shauri la kumwua Saulo,
24
lakini Saulo akavumbua shauri lile. Nao walichunga milango ya kuingilia ndani ya muji ule muchana na usiku kusudi wamwue,
25
lakini siku moja usiku wanafunzi wa Saulo wakamutwaa, wakamuweka ndani ya kitunga na kumutelemusha na kamba inje ya ukuta.
26
Saulo alipofika Yerusalema, alijaribu kujiunga na wanafunzi wengine, lakini wote walimwogopa, kwa sababu hawakusadiki kwamba amekwisha kugeuka mwanafunzi.
27
Basi Barnaba akamutwaa na kumupeleka kwa mitume. Akawaelezea namna Saulo alivyomwona Bwana katika njia na jinsi Bwana alivyosema naye. Akawaelezea vilevile namna Saulo alihubiri kwa jina la Yesu pasipo woga katika Damasiki.
28
Saulo akakaa pamoja nao, akaenda huku na huko katika muji Yerusalema akihubiri kwa jina la Yesu pasipo woga.
29
Vilevile alisemezana na kubishana na Wayuda waliosema kigriki, lakini wao walitafuta njia ya kumwua.
30
Wandugu walipopata habari ile, wakamupeleka mbali katika muji Kaisaria, na kutoka kule wakamutuma aende katika muji Tarso.
31
Wakati ule, kanisa lilikuwa na amani katika Yudea yote, Galilaya na Samaria. Vilevile lilizidi kupata nguvu na kuendelea kumwogopa Bwana, nalo liliongezeka kwa musaada wa Roho Mutakatifu.
32
Petro alipokuwa akipita fasi zote katika majimbo yale, siku moja akawatembelea wanafunzi walioishi katika muji wa Luda.
33
Kule akamwona mutu mumoja mwenye ugonjwa wa kupooza aliyeitwa Ainea aliyeshindwa kutoka ndani ya kitanda kwa muda wa miaka minane.
34
Petro akamwambia: “Ainea, Yesu Kristo anakuponyesha. Simama, ujitandikie kitanda chako wewe mwenyewe.” Na mara moja Ainea akasimama.
35
Nao wakaaji wote wa Luda na bonde la Saroni walipoona jambo hilo wakamugeukia Bwana.
36
Katika muji wa Yopa kulikuwa mwanafunzi mumoja mwanamuke aliyeitwa Tabita. (Katika kigriki ni “Dorika,” maana yake “Pongo”.) Mwanamuke huyu alikuwa akifanya matendo mengi mema na kuwasaidia wamasikini.
37
Katika siku zile akapata ugonjwa, naye akakufa. Walipokwisha kunawisha maiti yake, wakailalisha ndani ya chumba cha gorofi.
38
Na kwa kuwa muji Luda ulikuwa karibu na muji Yopa, wanafunzi walikuwa wamesikia kwamba Petro yuko kule. Kwa hiyo wakatuma kwake wajumbe wawili kwa kumwambia: “Tunakusihi, ufike huku kwetu bila kukawia.”
39
Mara moja Petro akaenda pamoja nao. Naye alipofika wakamupeleka ndani ya chumba cha gorofi. Wajane wote wakamuzunguka Petro, wakilia na kumwonyesha kanzu na nguo zote Dorika alizowashonea wakati alipokuwa angali muzima.
40
Petro akawaamuru watu wote waende inje, akapiga magoti na kuomba. Kisha akaelekea ile maiti na kusema: “Tabita, simama!” Halafu Tabita akafungua macho, na wakati alipomwona Petro akaamuka na kuikaa.
41
Petro akamushika mukono na kumusimamisha wima. Kisha akawaita wanafunzi na wajane, akamupeleka mbele yao akiwa muzima.
42
Na habari hii ikaenea katika muji wote wa Yopa, kwa hiyo watu wengi wakamwamini Bwana.
43
Petro akakaa siku nyingi huko Yopa kwa fundi mumoja wa kutengeneza vitu vya ngozi, aliyeitwa Simoni.
← Chapter 8
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 10 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28