bible
ra
🌐 Language
English
Español
Français
Deutsch
Português
Italiano
Nederlands
Русский
中文
日本語
한국어
العربية
Türkçe
Tiếng Việt
ไทย
Indonesia
All Languages
Home
/
Swahili
/
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
/
Acts 2
Acts 2
Swahili SWC02 (BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002)
← Chapter 1
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 3 →
1
Wakati siku ya Pentekoste ilipotimia, wanafunzi walikuwa wamekusanyika wote pamoja wakibaki kwenye nafasi moja.
2
Mara moja uvumi uliokuwa kama upepo unaovuma kwa nguvu sana ukashuka kutoka mbinguni. Nao ukajaa ndani ya nyumba yote walimokuwa wakiikaa.
3
Kisha wakaona mufano wa ndimi za moto zikitokea, nazo zikasambaa na kushuka juu ya kila mumoja wao.
4
Wote wakapewa Roho Mutakatifu na kuanza kusema kwa luga mbalimbali kwa kadiri Roho alivyowawezesha kusema.
5
Katika Yerusalema kulikaa Wayuda wamoja waliotoka katika inchi zote za dunia, nao walikuwa watu wenye kuogopa Mungu.
6
Wakati waliposikia ile fujo, wakakusanyika kwa uwingi. Wote wakapigwa na mushangao, kwa sababu kila mumoja wao aliwasikia waamini wakisema katika luga yake ya kuzaliwa.
7
Wakashituka na kushangaa, wakisema: “Hawa wote wanaosema si wazaliwa wa Galilaya?
8
Basi namna gani kila mumoja wetu anawasikia wakisema luga yake ya kuzaliwa?
9
Kati yetu kuna watu wenye kutoka katika inchi hizi: Parti, Medi, Elamu, Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto, Jimbo la Azia,
10
Furigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kurene. Vilevile kuna wageni waliotoka Roma,
11
kati yao kuna Wayuda na watu waliofuata dini ya Kiyuda, na kuna watu wa inchi ya Krete na ya Arabia. Hata hivi tunawasikia hawa wote wakisema habari za matendo makubwa ya Mungu katika luga zetu za kuzaliwa!”
12
Wote wakashituka na kushangaa, wakaulizana: “Maana ya mambo haya ni nini?”
13
Lakini wengine waliwachekelea waamini, wakisema: “Watu hawa wamelewa kabisa.”
14
Basi Petro akasimama pamoja na wale mitume wengine kumi na mumoja na kuanza kusema kwa sauti kubwa mbele ya watu: “Ninyi Wayuda, nanyi wote munaokaa Yerusalema, musikilize vizuri, mutege sikio kwa maneno nitakayowaambia.
15
Watu hawa si walevi kama munavyozani, kwa sababu ingali tu saa tatu ya asubui.
16
Lakini jambo hili ni lile lililosemwa na nabii Yoeli.
17
‘Mungu anasema: Katika siku za mwisho, nitashusha Roho wangu juu ya watu wote; wana wenu na wabinti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono nao wazee wenu wataota ndoto.
18
Hakika katika siku zile nitashusha Roho wangu juu ya watumishi wangu, wanaume na wanawake, nao watatabiri.
19
Nami nitafanya maajabu juu katika mbingu na vitambulisho chini katika dunia: kutakuwa damu, moto na moshi mwingi.
20
Jua litatiwa giza, mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Bwana, ile siku kubwa na ya utukufu.
21
Halafu watu wote watakaoomba kwa jina la Bwana ataokolewa.’
22
“Ninyi wanainchi wenzangu Waisraeli, musikilize maneno haya: Yesu wa Nazareti alikuwa mutu aliyetambulishwa wazi na Mungu mbele yenu kwa njia ya vitambulisho, miujiza, na maajabu aliyofanya katikati yenu kama munavyojua ninyi wenyewe.
23
Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.
24
Lakini Mungu alimufufua, akimufungua toka vifungo vya lufu, kwa sababu haikuwezekana afungwe na lufu.
25
Kwa maana mufalme Daudi alisema hivi juu yake: ‘Nilikuwa nikimwona Bwana mbele yangu saa zote; yeye ni karibu nami, kusudi nisitikisike.
26
Ni kwa hiyo moyo wangu unafurahi, ulimi wangu unashangilia, nami ninakaa na matumaini,
27
maana hautaniachilia kubaki katika kuzimu, hautakubali mutumishi wako mutakatifu apate kuoza.
28
Umenionyesha njia za uzima, utanijaza furaha nitakapokuwa karibu nawe.’
29
“Wandugu, inanipasa kuwaambia kwa uhodari juu ya babu yetu mukubwa Daudi. Yeye alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lingali hata leo.
30
Lakini kwa sababu alikuwa nabii, alijua kwamba Mungu amemwahidi kwa kiapo kwamba atamutawalisha mumoja wa wazao wake kwa kurizi ufalme wake.
31
Daudi aliona kwa mbali yale yatakayotokea, ni kwa sababu hii alisema maneno haya juu ya ufufuko wa Kristo: ‘Hakuachiliwa kubaki katika kuzimu, wala mwili wake haukuoza.’
32
“Mungu alimufufua huyo Yesu, na sisi wote tuko washuhuda wa jambo hili.
33
Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.
34
Maana Daudi mwenyewe hakupanda mbinguni, lakini alisema: ‘Bwana wetu Mungu alimwambia Bwana wangu: Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu,
35
mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako, wakuwe kama kiti cha kupumzishia miguu.’
36
“Kwa hiyo watu wa taifa la Israeli wajue hakika kwamba yule Yesu muliyemutundika juu ya musalaba, Mungu amemufanya kuwa Bwana na Masiya!”
37
Nao watu waliposikia maneno hayo, wakachomwa katika mioyo yao na kuwaambia Petro na mitume wengine: “Wandugu zetu, tufanye nini?”
38
Petro akawajibu: “Mugeuke toka katika zambi zenu, na kila mumoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo, na Mungu atawasamehe zambi zenu. Hivi mutapokea zawadi ya Roho Mutakatifu.
39
Kwa maana ahadi hii ya Mungu ilitolewa kwenu, kwa watoto wenu na kwa wote wanaokaa mbali, ndio wote ambao Bwana Mungu wetu atakaowaita.”
40
Petro akazidi kusema maneno mengine ya kuwaonya na kuwatia moyo, akisema: “Mujiokoe toka kati ya kizazi hiki kipotovu!”
41
Siku ile watu waliosadiki mafundisho ya Petro, wakabatizwa. Na kadiri ya watu elfu tatu wakaongezeka katika kundi la wanafunzi.
42
Nao walikuwa wakijitoa kufuata mafundisho ya mitume, kuishi katika ushirika wa kindugu, kumega mukate na kuomba.
43
Kila mumoja wao akaingiwa na woga, nao mitume walifanya maajabu na vitambulisho vingi.
44
Na wanafunzi wote waliishi katika umoja na katika ushirika wa vitu vyao vyote.
45
Waliuzisha mali zao na vyote walivyokuwa navyo na kugawanya kati yao kufuatana na mahitaji ya kila mutu.
46
Kila siku walikuwa wakikusanyika pamoja katika hekalu, nao walikula chakula pamoja katika nyumba zao kwa furaha na katika unyenyekevu.
47
Nao walisifu Mungu na kufurahiwa na watu wote. Na kila siku Bwana aliongeza katika kundi la waamini watu waliokuwa wakiokolewa.
← Chapter 1
Jump to:
Chapter 1
Chapter 2
Chapter 3
Chapter 4
Chapter 5
Chapter 6
Chapter 7
Chapter 8
Chapter 9
Chapter 10
Chapter 11
Chapter 12
Chapter 13
Chapter 14
Chapter 15
Chapter 16
Chapter 17
Chapter 18
Chapter 19
Chapter 20
Chapter 21
Chapter 22
Chapter 23
Chapter 24
Chapter 25
Chapter 26
Chapter 27
Chapter 28
Chapter 3 →
All chapters:
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28